Monday, January 8, 2018

RC MTAKA AKUTANA NA BALOZI WA CHINA HAPA NCHINI, AAHIDI MENGI KWA MKOA WA SIMIYU






Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amekutana na Balozi wa China Nchini Tanzania Mhe.Wang Ke.

Balozi Wang amefurahishwa na utekelezaji wa Mpango wa Simiyu  wa One Product One Distict-(Wilaya Moja Bidhaa Moja) Maana China kwa sasa wanatekeleza One Belt One Road.

Aidha, ametoa vyerehani 50 kwa Mabinti wa Simiyu ikiwa ni kuunga Mkono juhudi za viwanda vidogovidogo mkoani Simiyu.

Balozi huyo pia amekubali kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kujenga bweni moja la watoto wa kike na  amesema yupo tayari kusaidia ujenzi wa Maktaba ndani ya mkoa

Wakati huo huo amesema atasaidia kompyuta kuunga mkono juhudi za Mkoa kwenye Maendeleo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(ICT) na kusaidia mkoa kupata jimbo rafiki nchini china pamoja na baadhi ya maafisa wa Simiyu kwenda China kupata uzoefu.


Vilevile ameuchagua Mkoa wa Simiyu kuwa mkoa wake wa Kipaumbele katika maeneo mengi ya miradi ya Kilimo,mifugo na uvuvi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akiwa na Balozi wa China hapa Nchini, Mhe.Wang Ke ofisini kwake jijini Dar es Salaam ambapo walizungumza mambo mengi kuhusu maendeleo ya Mkoa wa Simiyu














0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!