Saturday, January 20, 2018

WANUNUZI WA PAMBA WASIO WAAMINIFU WATAJWA KUWA CHANZO CHA WAKULIMA KUCHANGANYA PAMBA NA MAJI

Viongozi na wanachama wa Vyama vya Ushirika wa Mazao -AMCOS Mkoani SIMIYU wamesema chanzo cha wakulima wa Pamba kuchanganya mchanga na mafuta ya kenge kwa madai ya kuongeza uzito katika zao hilo kinatokana na baadhi ya wanunuzi wasio waaminifu  kuwaibia kupitia mizani.

Hayo wameyasema katika majadiliano ya namna ya uendeshaji vya Vyama vya Ushirika na uanzishwaji wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa SIMIYU mjadala ulioandaliwa ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini.

Kikao baina ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka na viongozi na wanachama wa Vyama vya Ushirika wa Mazao -AMCOS chenye lengo la kujadili changamoto zinazowakabili wakulima na uanzishwaji wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa SIMIYU.

Katika mjadala huo wadau hao wamesema udangangifu katika mizani ya kupima uzito wa Pamba umechangia kwa kiasi kikubwa  wakulima kutumia mbinu mbadala za kuongeza uzito

Moses Masalu Mwenyekiti wa chama cha ushirika mhango halmashauri ya mji wa bariadi amesema kuwepo kwa wizi wa pamba katika mizani za kupimia uzito kumesababisha wakulima wengi kutumia mbinu mbadala za kuongeza uzito ili kufidia machungu ya kuibiwa pamba yao na makarani wanapoenda kuuza pamba.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga amesema kuchelewa kuanza kwa msimu wa pamba kunachangia kushuka kwa bei soko la dunia kutokana na kugongana na mataifa mengine katika msimu na hivyo kupendekeza kuanza april badala ya mei na juni.

Kwa upande wake Kaimu Mrajisi Masoko na Uwekezaji Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini, EDMUND MASSAWE amesema nia ya serikali ya kuimarisha ushirika nchini ni kuviwezesha vyama vikuu kununua mazao ya wakulima.

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amewasisitiza viongozi wa  vyama hivyo kuwa waadilifu .

Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa SIMIYU kinatarajiwa kuundwa April mwaka huu kabla ya kuanza msimu wa ununuzi.


Baadhi ya viongozi na wanachama wa Vyama vya Ushirika wa Mazao -AMCOS wakimsikilza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka(hayupo pichani) katika kikao cha kujadili changamoto zinazowakabili wakulima na uanzishwaji wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa SIMIYU
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na viongozi na wanachama wa Vyama vya Ushirika wa Mazao -AMCOS (hawapo pichani)katika kikao cha kujadili changamoto zinazowakabili wakulima na uanzishwaji wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa SIMIYU.




0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!