Tuesday, February 18, 2020

ASKARI WAASWA KUEPUKA VITENDO VINAVYOLITIA DOSARI JESHI LA POLISI


Askari mkoani Simiyu wameaswa kulinda hadhi ya jeshi la polisi kwa kujiepusha na vitendo viovu vinavyolitia dosari jeshi hilo.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati akizungumza na askari wa mkoa huo Februari 17, 2020 ambapo amevitaja vitendo hivyo kuwa ni pamoja na kutoa siri za jeshi, kuomba rushwa, utapeli na kushiriki kuharibu ushahidi katika baadhi ya kesi.

“Ni jambo la aibu kwa askari kushiriki katika uhalifu,  kutoa siri za jeshi na kugeuka kuwa mtoa taarifa kwa wahalifu, ipendeni kazi yenu muepuke mambo yanayodhalilisha jeshi na mjenge tabia ya kuonyana ili mlinde heshima ya jeshi letu,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka ametoa wito kwa askari mkoani Simiyu kujiendeleza kielimu ili waweze kupata sifa za kulitumikia jeshi katika nafasi mbalimbali huku akiwaeleza umuhimu wa kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo Mkoani humo kwa lengo la kutengeneza kipato cha zaida.

Katika hatua nyingine  Mtaka ametoa wito kwa viongozi wa Jeshi la Polisi kutenda haki kwa askari walio chini yao ikiwemo kutoa nafasi ya kuwapandisha vyeo askari wanaostahili  kwa wakati uliopo ili kuwapa motisha katika kazi yao.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, SACP Henry Mwaibambe amesema kuwa katika Awamu hii ya tano hakuna kisingizio kwa askari kushindwa kufanya kazi zao kwa kutofuata taratibu.

“Ilikuwa siyo rahisi sana kumkamata tajiri , lakini sasa hivi Watanzania wote tuko hali moja hakuna cha huyu ni nani na yule ni nani; sasa hivi mtu akifanya hivyo ni mapungufu yake binafsi tunafanya kazi kwa kufuata taratibu za jeshi pasipo kuingiliwa na mtu yeyote, sisi tuliokaa muda mrefu kwenye jeshi la Polisi tunajua kazi nzuri inayofanywa na Mhe. Rais,” alisema Mwaibambe.

Mwaibambe ameongeza kuwa askari kama watumishi wa umma wengine wanapaswa kujiepusha na masuala yanayoleta malalamiko kwa wananchi huku akisisitiza kuwa hawatasita kuwachukulia hatua askari watakaoshindwa kufanya kazi kwa uadilifu.

Kwa upande wao askari wamesema watafanya kazi kwa kufuata sheria na taratibu huku wakiomba Serikali ya Mkoa iweze kuwasaidia upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya kujenga makazi yao binafsi na maeneo ya kuweka uwekezaji wao.
MWISHO

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na askari wa Jeshi la Polisi mkoani humo katika kikao kilichofanyika Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Baadhi ya askari Polisi mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka katika kikao kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, SACP Henry Mwaibambe akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kulia) azungumze na askari wa Jeshi la Polisi Mkoani hapa katika kikao kilichofanyika Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
 Askari wa Jeshi la Polisi, Koplo Abdallah Manzi akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na askari hao, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) akiteta jambo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, SACP Henry Mwaibambe na  Mkuu wa Upepelezi Mkoa wa Simiyu, SSP Israel Makongo, mara baada ya kumalizika kwa kikao chake na askari polisi, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
 Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na askari wa Jeshi la Polisi mkoani Simiyu,  kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja baadhi ya maafisa na askari wa jeshi la polisi mkoani humo, mara baada ya kumalizika kwa kikao chake na askari polisi, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Baadhi ya askari wa jeshi la polisi mkoa wa Simiyu wakiimba wimbo wa uadilifu kabla ya kikao chao na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani), kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja baadhi ya maafisa na askari wa jeshi la polisi mkoani humo, mara baada ya kumalizika kwa kikao chake na askari polisi, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Askari polisi H.864 DIC Yassin akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na askari hao, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, SACP Henry Mwaibambe(kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) na Mkuu wa Upepelezi Mkoa wa Simiyu, SSP Israel Makongo, mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Mkuu wa Mkoa  na askari polisi, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(wa tatu kushoto walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi naUsalama ya Mkoa huo, mara baada ya kikao cha Mkuu wa Mkoa na askari polisi, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kikao cha Mkuu wa Mkoa na askari polisi, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) katika picha ya pamoja  na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, SACP Henry Mwaibambe(kushoto) na  Mkuu wa Upepelezi Mkoa wa Simiyu, SSP Israel Makongo, mara baada ya kumalizika kwa kikao chake na askari polisi, kilichofanyika  Februari 17, 2020 Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!