Friday, February 14, 2020

WAZABUNI WATAJWA KUCHANGIA UCHELEWESHAJI WA MIRADI

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) nchini Brigedia Jenerali Charles Mbuge  amesema kuwa baadhi ya wazabuni wanaouza vifaa vya ujenzi wamekuwa wakiuza vifaa kwa bei ya juu na kuchelewesha vifaa hivyo pale vinapohitajika, jambo linalopelekea baadhi ya miradi inayotekelezwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi hilo (SUMA JKT) kutokamilika kwa wakati.

Brigedia Jenerali Mbuge ameyasema hayo Februari 13, 2020 mjini Bariadi wakati akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT mkoani Simiyu.

Ameongeza kuwa katika kukabiliana na changamoto hiyo, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limejipanga kuanzisha maduka ya vifaa vya Ujenzi vitakavyouzwa kwa bei ya  jumla ili kuwezesha upatikanaji wa vifaa kwa urahisi, haraka na kwa bei nafuu ikilinganishwa na wazabuni wengine.

“Tatizo moja ninaloliona kwenye utekelezaji wa miradi ni vifaa kuuzwa kwa bei ya juu sana na kucheleweshwa, tumeamua kuwa  na maduka ya vifaa ya jumla; tutatoa maelekezo kwa wakuu wa kanda za ujenzi watatupatia mahitaji yao, ili kuwawezesha kufanya kazi kwa wakati kama tunavyokubaliana na washitiri wetu,” alisema Brigedia Jenerali Mbuge.

Katika hatua nyingine Brigedia Jenerali Mbuge amesema jeshi hilo litaendelea kuwatumia vijana watakaomaliza mafunzo ya JKT katika shughuli zilizopo kwenye miradi inayotekelezwa na Jeshi hilo lengo likiwa kuwawezesha vijana hao kupata kipato na baadaye waweze kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa pekee.

Vile vile ameahidi kuongeza nguvu kazi ya vijana katika mradi inayotekelezwa na SUMA JKT mkoani Simiyu kuongeza kasi na miradi hiyo iweze kukamilika kwa muda uliopangwa, huku akitoa wito kwa Taasisi mbalimbali kuipa kazi SUMA JKT,  ili iendelee kuwa kutoa gawio kubwa kwa Serikali, ambapo amesema mwaka 2018/2019 ilitoa zaidi ya shilingi bilioni moja na mwaka 2019/2020 linatarajia kupanda zaidi kutokana na uwepo wa vyanzo vya kutosha.

Awali akitoa taarifa, Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya miundombinu katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mhandisi Mashaka Luhamba  amesema JKT wanatekeleza miradi minne mkoani Simiyu ukiwemo wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,  wodi ya wazazi Hospitali ya Rufaa ya mkoa, ujenzi  jengo la wizara ya kilimo linalojengwa kwenye viwanja vya maonesho ya Nane nane pamoja na  kiwanda cha Chaki Maswa ( Maswa chalk) .

Aidha mhandisi huyo amebainisha kuwa ujenzi wa jengo la Mkuu wa Mkoa unatekelezwa kwa kipindi cha miezi 18 kwa gharama ya shilingi bilioni 5.7  ambapo ujenzi rasmi ulianza mwezi Mei, 2019 na endapo fedha zitapatikana kwa wakati unatarajiwa kukamilika Novemba,  2020.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema ni vema SUMA JKT ikahuisha uharaka wa kutekeleza miradi kama jamii inavyoutarajia kwa kuwa jamii na Serikali imejenga imani kubwa kwa JKT kutekeleza miradi kwa wakati ikilinganishwa na wakandarasi wengine.

Mtaka ameongeza kuwa miradi inayotekelezwa na SUMA JKT iwe fursa kwa vijana waliopata mafunzo ya JKT na kumaliza mikataba yao ili waweze kupata kipato kitakachowasaidia kwenda kujitegemea na kujiajiri endapo hawataajiriwa.
MWISHO

 Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini Brigedia Jenerali Charles Mbuge akizungumza na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji wa Jeshi  mara baada ya kukagua mradi wa Ujenzi wa wodi ya wazazi  unaendela katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, wakati wa ziara yake Mkoani humo Februari 13, 2020  yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na Shirika la Uzalishaji mali la JKT(SUMA JKT).



Meneja wa  SUMA JKT Kanda ya Ziwa Kapteni Fabian Buberwa akiwaongoza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kushoto) na  Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini  Brigedia Jenerali Charles Mbuge(wa nne kushoto) kuelekea katika eneo la ujenzi wa wodi ya wazazi  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, wakati wa ziara Mkuu huyo wa JKT Mkoani humo Februari 13, 2020  yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT.
 Katibu Tawala Msaidizi seksheni ya Miundombinu katika Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhandisi Mashaka Luhamba akitoa maelezo ya hali ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT Mkoani Simiyu kwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini Brigedia Jenerali Charles Mbuge , wakati wa ziara ya Mkuu huyo wa JKT Mkoani humo Februari 13, 2020  yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT.

 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(wa pili kushoto) akizungumza jambo katika ziara ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT) Brigedia Jenerali Charles Mbuge Mkoani humo Februari 13, 2020  yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT.


Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT)  Brigedia Jenerali Charles Mbuge(kulia) akimkabidhi kalenda Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati akiwa katika zaira ya kikazi  mkoani humo Februari 13, 2020 yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT.
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge(kulia) akimkabidhi kalenda Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati akiwa katika zaira ya kikazi  mkoani humo Februari 13, 2020 yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT, (kushoto) Katibu Tawala Msaidizi seksheni ya Miundombinu katika Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhandisi Mashaka Luhamba, (wa pili kushoto) Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ekwabi Mujungu

 Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge(wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka (wa nne kushoto), wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa na baadhi ya Maafisa wa jeshi hilo waliofuatana naye katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT Mkoani Simiyu Februari 13, 2020.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge wakitoka katika Jengo la Wizara ya kilimo linalojengwa katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Mjini Bariadi, wakati wa ziara ya Mkuu huyo wa JKT ya kukagua miradi ya ujnezi inayotekelezwa na SUMA JKT Mkoani humo, iliyofanyika Februari 13, 2020.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akisalimiana na  Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi kwa lengo la kufanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT Mkoani humo, iliyofanyika Februari 13, 2020.

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge(wa nne kulia) akizungumza na wasimamizi wa miradi ya ujenzi  wa majengo ya Serikali inayotekelezwa  na SUMA JKT Mkoani Simiyu wakati wa ziara yake Februari 13, 2020 mkoani humo yenye lengo la kukagua miradi hiyo.
 Meneja wa  SUMA JKT Kanda ya Ziwa Kapteni Fabian Buberwa(kulia) akitoa maelezo ya hali ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la Wizara ya Kilimo katika Uwanja wa Nanenane Mjini Bariadi mkoani Simiyu kwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini(JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge(wa pili kushoto), wakati wa ziara yake Februari 13, 2020 ya kukagua miradi inayotekelezwa na SUMA JKT Mkoani Simiyu


Baadhi ya mafundi wakiendelea na kazi katika mradi wa ujenzi wa jengola wodi ya wazazi katika Hospitali ya  Rufaa ya mkoa wa Simiyu, mradi ambao unatekelezwa na SUMA JKT.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akiwa na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT), Brigedia Jenerali Charles  Mbuge  alipompokea  mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi kwa lengo la kufanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT Mkoani humo, iliyofanyika Februari 13, 2020. 

 Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini(JKT),  Brigedia Jenerali Charles Mbuge(kulia) akizungumza na baadhi ya viongozi na watendaji  wa Mkoa wa Simiyu (baadhi hawapo pichani) katika kikao kilichofanyika wakati wa ziara yake Februari 13, 2020 mkoani humo yenye lengo la kukagua miradi inayotekelezwa na SUMA JKT Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini (JKT),  Brigedia Jenerali Charles Mbuge akizungumza na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji wa Jeshi  mara baada ya kukagua mradi wa Ujenzi wa Jengo la wodi ya wazazi  unaoendela katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, wakati wa ziara yake Mkoani humo Februari 13, 2020  yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na Shirika la Uzalishaji mali la JKT(SUMA JKT).

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!