Wednesday, February 17, 2021

 

WIZARA YA ELIMU YAAHIDI KUTOA FEDHA UJENZI WA CHUO VETA SIMIYU

Na Stella Kalinga, Simiyu RS

Naibu waziri wa Elimu, sayansi na teknolojia, Mhe.Omary Kipanga amesema Wizara hiyo itahakikisha inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA cha mkoa wa Simiyu ili kutimiza azma ya serikali ya kila mkoa na wilaya kuwa na chuo cha Mafunzo ya ufundi stadi (VETA).

Kipanga ameyasema hayo Februari 16, 2021 wakati wa ziara yake iliyolenga kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyuo vya VETA ambapo kwa mkoa wa Simiyu alipata fursa ya kutembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA cha mkoa katika Mtaa wa Bunamhala Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omari Juma Kipanga (katikati) akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wakati alipotembelea Chuo cha Maendelea ya Jamii Bariadi kilichopo Mtaa wa Bunamhala Februari 16, 2021 wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani Simiyu.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!