Saturday, May 8, 2021

RC MTAKA ASHAURI PPRA KUFANYA TATHMINI YA MIRADI ILIYOTEKELEZWA KWA ‘FORCE ACCOUNT’

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa rai kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma(PPRA) kufanya tathmini ya miradi iliyotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano kupitia mfumo wa ‘Force Account’ (Mfumo usiotumia wakandarasi/ wakandarasi katika ujenzi) na baadaye ije na usahauri kwa serikali juu ya namna ya kuboresha matumizi ya mfumo huo hususani katika suala la ubora. 

Mtaka ametoa rai hiyo jana Mei 06, 2021 wakati akifungua mafunzo yaliyoandaliwa na mamlaka hiyo yakiwashirikisha wataalam wa Ununuzi na ugavi, maafisa masuuli na baadhi ya watendaji ili kuwajengea uwezo ili waweze kufanya kazi ya ununuzi wa umma kwa ufanisi ambayo yamefanyika Mjini Bariadi.

“Tusije tukawa na miradi hapa lakini miaka kumi inayokuja tukajikuta kwenye tatizo kubwa, kwa hiyo PPRA ije na ushauri kwa miaka mitano ya ‘Force Account’ pengine mfumo huo ni mzuri zaidi kwenye ujenzi wa miradi ya aina gani,” alisema Mtaka.

Kwa upande wake Afisa mtendaji Mkuu wa PPRA, Mhandisi. Leonard Kapongo amesema katika mafunzo hayo wataalam hao watapata naasi ya kujifunza zaidi kuhusu mfumo huo, utekelezaji wake na ikiwa kuna changamoto walizozibaini wakati wa utekelezaji wa miradi kwenye maeneo yao ili zijadiliwe kwa pamoja na kubainisha kuwa PPRA iko tayari kupokea ushauri.

Aidha, Mhandisi Kapongo amesema wameamua kutoa mafunzo ya masuala ya ununuzi wa ummakwa wataalam hao kwa lengo la kuwafundisho Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka sura namba 410 ambayo ni sheria mama ya mwaka 2010 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2016 ili waweze kufanya kazi za ununuzi kwa ufanisi.

Mhandisi Mpongo amesema pamoja na mkoa wa Simiyu mafunzo hayo yameshatolewa katika mikoa mingine  14 ambayo ni Ruvuma, Njombe, Iringa, Kagera, Shinyanga, Kigoma, Geita, Rukwa, Katavi, Tabora, Mbeya, Songwe, Dodoma na Mara.

 

Naye Mkurugenzi wa Kujenga Uwezo na ushauri wa PPRA, Mhandisi Mary Swai amesema mafunzo hayo yatawasaidia wataalam kuzingatia sheria ya ununuzi wa umma na kuzingatia taratibu katika ununuzi ikiwa ni pamoja na kusimamia mfumo wa ‘force account’ waweze kuhakikisha ubora unaotakiwa unapatikana na thamani ya fedha inaonekana.

MWISHO













0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!