Saturday, May 8, 2021

USIMAMIZI WA TMDA, ELIMU KWA UMMA ZATAJWA KUSAIDIA KUPUNGUZA BIDHAA BANDIA SOKONI

 Usimamizi shirikishi, elimu kwa umma zimetajwa kuwa ni miongozi mwa sababu zilizochangia kupunguza uwepo wa dawa bandia katika mikoa ya kanda ya ziwa, jambo ambalo limechangia soko la bidhaa hizo (dawa) kuwa soko salama. 

Hayo yamebainishwa na Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba, Bi. Sophia Mziray Mei 06, 2021 wakati akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi cha wataalam wa afya na mifugo pamoja na wakaguzi wa dawa , kilichofanyika Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

“Tumeza kulisimamia vizuri soko hili la kanda ya ziwa siyo kama miaka ile ya nyuma kwa sasa hivi soko hili naweza kusema ni soko salama kwa bidhaa hizi, hata zikikutwa sokoni ni chache sana, pamoja na hilo tunawaeleimisha wananchi, suala la udhibiti siyo la taasisi tu, hata wananchi ni wadau wakubwa katika udhibiti na huwa tunapata taarifa kutoka kwa rai wema juu ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanaofanya biashara haramu za dawa, tumewabaini na tumewachukulia hatua,” alisema Mziray.

Akifungua kikao kazi hicho Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Ekwabi Mujungu amesema kufanya kazi bila taarifa (kumbukumbu) ni tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi wa haraka huku akiwataka kupitia kikao kazi hicho kuja na suluhisho la kudumu.

“Mnaohusika si lazima mpaka watu  watoke Dar es salaam kuja kuona dawa bandia fanyeni kazi kwa viapo vyenu,” alisema Mujungu

Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa kikao kazi hicho wameishukuru TMDA kutoa mafunzo ambayo yatawaongezea maarifa na kuwawezesha kutekeleza majukumu yao hususani ya ukaguzi kwa ufanisi.

“Elimu niliyoipata leo itanisaidia sana katika kufanya kaguzi mbalimbali pia imenisaidia kujua kuwa ni jukumu letu wataalam kuwapa elimu wamiliki wa maduka ili wauze bidhaa zilizosajiliwa na wajenge utamaduni wa kukagua bidhaa zao (dawa) na kubaini dawa zilizoisha muda wake ili watumiaji wa mwisho au walaji wasiumizwe kwa kuuziwa dawa zisizofaa” alisema Linah Kirumbi Daktari wa Mifugo Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

MWISHO





0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!