Saturday, May 8, 2021

WAZAZI WENYE WATOTO WALIO MADARASA YA MITIHANI WAPUNGUZIENI KAZI: RC MTAKA

 Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa rai kwa wazazi na walezi wenye watoto walio katika madarasa ya mitihani ya Taifa kuwapunguzia kazi ili wanafunzi hao waweze kupata muda wa kujiandaa na mitihani hiyo na hatimaye waweze kufanya vizuri katika mitihani yao. 

Mtaka ameyasema hayo Mei 06, 2021 Mjini Bariadi wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na ofisi yake kwa ajili ya waumini wa dini na Kiislamu walio katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ambayo pia iliwahusisha viongozi na watendaji mbalimbali wa Serikali mkoani  Simiyu.

“Matarajio yangu ni kuhakikisha kuwa mkoa huu unabaki kuwa miongoni mwa mikoa mitano inayofanya vizuri kwenye elimu nchini, kwenye malengo yetu ya mwaka huu ni kuona tunatoka kwenye nafasi ya tano, kwenda nafasi ya tatu na kufikia nafasi ya kwanza ili kufikia hapo tuna kazi ya kufanya; niwaombe wazazi na walezi wote wa mkoa wa Simiyu wenye watoto wa madarasa ya mitihani wawapunguzie kazi ili wapate muda wa kujisomea na kufanya matayarisho ya mitihani yao ya Taifa,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka amewataka wazazi kutowaruhusu wanafunzi kwenda katika minada kufanya biashara badala yake wahakikishe wanafunzi wote wanahudhuria masomo, “ Hii habari ya kuona watoto (wanafunzi) minadani hapana, kila mmoja awe mzazi na mlezi minada ni kwa ajili ya wazazi kufanya biashara siyo mahala kwa watoto kupeleka bidhaa maana minada yetu mingi inafanyika siku za kazi”

Kwa upande wake Sheikh wa Mkoa wa Simiyu Mahamudu Kalokola amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Simiyu kwa futari na kushiriki katika shughuli mbalimbali zinasowahusu Waislamu ikiwa ni pamoja na kushiriki katika ujenzi wa msikiti mkuu wa Bariadi , huku akiwataka Waislamu wote mkoani Simiyu kuendelea kuiombea nchi na kudumisha amani iliyopo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya mkoa wa Simiyu,Askofu Marco Maduhu ametoa rai kwa wananchi mkoani Simiyu kuendelea kushirikiana na kuthaminiana bila kujali tofauti za dini zao.

Naye Katibu wa CCM mkoa wa Simiyu, Bi. Haula Kachwamba amewatakia heri Waislamu wote walio katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuwaombea waweze kumaliza mfungo huo salama.

MWISHO

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na baadhi ya waislamu, viongozi na wananchi wa mkoa wa Simiyu, Mei 06, 2021 Mjini Bariadi katika futari maalum aliyoiandaa kwa ajili ya Waislamu waliofunga na baadhi ya makundi ya watu mkoani hapa.

Baadhi ya Waislamu wakiwa katika hafla maalum ya futari Mei 06, 2021 Mjini Bariadi, iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  kwa ajili ya Waislamu waliofunga na baadhi ya makundi ya watu mkoani hapa.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka( wa pili kulia) akisalimiana na Sheikh wa Mkoa wa Simiyu Mahamudu Kalokola Mei 06, 2021 Mjini Bariadi katika futari maalum aliyoiandaa kwa ajili ya Waislamu waliofunga na baadhi ya makundi ya watu mkoani hapa.

Muimbaji maarufu wa Kaswida Bi. Arafa Abdillah Salum akiimba katika hafla maalum ya futari Mei 06, 2021 Mjini Bariadi, iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  kwa ajili ya Waislamu waliofunga na baadhi ya makundi ya watu mkoani hapa.



TAZAMA PICHA MBALIMBALI KATIKA HAFLA MAALUM YA FUTARI MEI 06, 2021 MJINI BARIADI, ILIYOANDALIWA NA MKUU WA MKOA WA SIMIYU, MHE. ANTHONY MTAKA  KWA AJILI YA WAISLAMU WALIOFUNGA NA BAADHI YA MAKUNDI YA WATU MKOANI HAPA. 













 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!