Wednesday, July 14, 2021

MKUU WA MKOA AELEKEZA WATENDAJI KUPIMWA KWA MIKATABA AIDHA CHMT ITAKAYOSHINDWA KUSIMAMIA AFYA KUVUNJWA

Ku


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akizungumza na Wadau wa Sekta ya afya 


 

Katibu Tawala Bi. Prisca Kayombo akiwatambulisha Viongozi Mbalimbali waliofuatana na mkuu wa mkoa 

                                        


                                        Wadau wa sekta ya afya wakijiandaa na kikao kazi








Wadau wakisikiliza mada wakati wa Kikao kazi

Kufuatia taarifa ya tathimini kuonesha usimamizi duni sekta ya Afya, RC Kafulila amelekeza kuandaliwa mikataba ya usimamizi kati ya RMO na DMOs,  RAS na DEDs na yeye mwenyewe RCs a DCs ili kuhakikisha wilaya na halmashauri zinasimamia sekta ya afya kikamilifu.  

Maelekezo hayo ameyatoa kufuatia tathimini ya usimamizi wa sekta ya afya kuonyesha kuwa kwa muda mrefu usimamizi wa Kamati za Afya Wilaya ( CHMT) ni dhaifu,  wakurugenzi na wakuu wa wilaya hawajawa na msukumo wa kutosha kuhakikisha usimamizi.

Aidha Mhe. Kafulila ameagiza KUVUNJWA kwa Kamati za usimamizi wa huduma ya Afya (CHMT)  itakayoshindwa kusimamia sekta ya afya katika halmashauri husika.  Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo kufuatia taarifa ya tathimini ya robo mwaka kuonyesha kuwa CHMT zote mkoani Simiyu kwa kipindi kirefu  zimekuwa na usimamizi dhaifu hata kusababisha vifo kizembe. 

Katika tathimini hiyo  Bariadi DC ilipata alama C, Busega D, Bariadi mji C, Meatu E , Maswa F huku Itilima ikipata F. Mhe.Kafulila ameelekeza kuwa katika taarifa ya oOktoba, halmashauri itakayopata chini ya alama B, basi CHMT husika itavunjwa na  wengine kuchukuliwa hatua za kiutumishi.

Mwisho

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!