Wednesday, July 14, 2021

TANZANIA INAJENGA SGR KWA GHARAMA NAFUU- KAFULILA.

 


 Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akiwa na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi. Prisca Kayombo wakati wa kikao na Waandishi wa habari.


 
Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Simyu wakiwa katia mkutano na waandishi wa Habari.

Kuanzia kulia Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi.Prisca Kayombo, Mkuu wa Mkoa Mhe. David Kafulila na Meneja Mradi  Ujenzi wa reli ya kisasa Mwanza- Isaka Eng. Machibya Masanja wakiwa katika kikao na waandishi wa habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.


Hayo ameleza jana RC KAFULILA wakati akifungua kampeni ya kuhamasisha uelewa wa wananchi kuhusu mradi wa SGR kipande cha Mwanza - Isaka( 341km), kitakachojengwa kwa gharama ya Tsh.3trn sawa na $1.3bn. 


Mhe.Kafulila amempongeza Rais kwa kuendeleza ujenzi huo kwa kasi zaidi na kusema kuwa gharama hii ni nafuu kulinganisha na Kenya na hata Ethiopia na hivyo inathibitisha usimamizi madhubuti wa fedha za Serikali.

 " Hii inazidi kuthibitisha ripoti ya jukwaa la kimataifa kuhusu uchumi- World Economic Forum 2019 kuonesha kwamba Tanzania ni nchi ya 29 katika nchi 186 duniani katika usimamizi thabiti wa matumizi ya fedha za umma".

 Mhe.Kafulila amesisitiza wananchi kujitokeza kwenye kampeni hiyo iliyoanza jana na itakamalizika  alhamisi ili kupata uelewa zaidi wa mradi. Amewahakikishia fidia kulipwa kwa mujibu wa sheria na zaidi kuwaomba wachangamkie fursa za biashara wakati wa ujenzi hususan eneo la Malampaka ambapo kambi kubwa ya ujenzi zinajengwa. Amesisitiza Shirika la reli kutoa upendeleo kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Simiyu kwa kazi ambazo zipo ndani ya uwezo.

Mwisho

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!