Thursday, February 9, 2017

MHANDISI WA UJENZI MKOA ASIMAMISHWA KAZI

    Na Stella Kalinga
Mhandisi wa Ujenzi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Simiyu, Deusdedit Mshuga amesimamishwa kazi kwa kukabiliwa na mashtaka matatu.

Akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa, Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg. Jumanne Sagini amesema Mhandisi huyo anashtakiwa kwa kushindwa kutekeleza majukumu aliyopewa kwa kiwango cha kuridhisha.

Amesema akiwa mtumishi wa umma kinyume na kipengele cha 8 cha sehemu"A" ya jedwali la kwanza la kanuni za Utumishi wa Umma, Tangazo la Serikali Na.168/2003; mtumishi huyo alishindwa kuandaa makadirio ya gharama za ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa yenye uhalisia.

Aidha , Aliandaa makadirio ya Tsh46,106,456,000 yaliyosomwa mbele ya Mhe. Rais tarehe 11 Januari,2017 ambayo ni ya juu kuliko uhalisia. 

Shtaka la pili linalomkabili  ni kufanya uzembe mkubwa wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kazi iliyopewa kinyume na kipengele cha 13 cha sehemu "A" ya jedwali la kwanza la Kanuni za Utumishi wa Umma,Tangazo la Serikali na 168/2003;

Alitaja (1) kuandaa makadirio ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa Tshs.46,106,456,000 hali iliyosababisha Mhe Rais kusomewa taarifa ya gharama zisizo na uhalisia na(2) Kuandaa michoro ya taswira (3 D)isiyoendana na michoro halisi ya Hospitali ya Mkoa iliyooneshwa mbele ya Mhe.Rais

Shtaka la tatu ni kufanya kazi kwa kukiuka maadili ya taaluma yake wakati wa utekelezaji ya kazi aliyopewa kinyume na kipengele cha 14 cha Sehemu "A" ya Jedwali la kwanza la Kanuni za Utumishi wa Umma, Tangazo la Serikali Na.168/2003:- kwa (1) Kuandaa makadirio ya shilingi 46,106,456,000 ya gharama za ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa bila kuzingatia mita za mraba za eneo, michoro na kusababisha gharama kubwa zisizo  na uhalisia
(2) Kuandaa makadirio ya shilingi 3,009,640,000 yasiyo na uhalisia ili kugharamia ujenzi wa majengo ya msingi kuwezesha Hospitali kuwa "functional" kwa kupiga simu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Katibu Tawala wa Mkoa, Ndg..Jumanne Sagini  ametoa wito kwa  watumishi wa  Umma mkoani humo kutekeleza majukumu waliyopewa kwa bidii, weledi na uadilifu ili kuepuka makosa ambayo husababisha watumishi kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

“Nikiwa kama mwajiri nimesikitishwa na kufadhaishwa na wataalam walioajiriwa ngazi ya mkoa kuishauri Sekretarieti ya Mkoa na kuzisimamia Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuzishauri kitaalam, kutenda matendo yanayodhihirisha  upungufu wa weledi, kushindwa  kutekeleza majukumu na uzembe mkubwa” alisema.

Naye Mkuu wa Mkoa huo,Mhe. Anthony Mtaka amesema gharama zilizowasilishwa awali na wataalam hazikuwa na mchanganuo toshelevu na makisio hayakuwa na uhalisia, hivyo amemwomba radhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli,  kwa taarifa za upotoshaji zilizotolewa na wataalam wakati wa ziara yake Mkoani humo.

“....kuna vitu vingine vilivyopachikwa kwenye ramani, wenye taaluma yao walipokutana ili kujustify hiyo bilioni 46.1 walishindwa kujustify kwenye ramani, kwa hiyo hatukuwa na uhalisia; baada ya mapitio  ya kazi zote ilionekana Hospitali ya Mkoa wa Simiyu inaweza kujengwa kwa gharama ya bilioni 11.4  mule mule alimosema Rais” alisema Mtaka.

Makadirio ya awali ya Ujenzi wa Hospitali ya Mkoa yalikuwa ni shilingi bilioni 46.1 na gharama hii haikukubaliwa na Mhe.Rais na badala yake akaagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kutembelea TBA Makao Makuu, ili kujifunza na kuona jinsi walivyoweza kujenga majengo ya hosteli ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam  kwa gharama ndogo ya shilingi bilioni 10 na akaahidi kutoa bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo.
 
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa huo wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya awali ya uchunguzi wa  gharama za ujenzi wa Hospitali ya Mkoa
Baadhi ya Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa huo, Ndg.Jumanne Sagini wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya awali ya uchunguzi wa  gharama za ujenzi wa Hospitali ya Mkoa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa huo wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya awali ya uchunguzi gharama za ujenzi wa Hospitali ya Mkoa

1 comment:


  1. Hello.
    Mimi ni Mr Rahel binafsi wakopeshaji mkopo ambao hutoa maisha wakati nafasi ya mkopo kwa watu binafsi, makampuni ya biashara, bima, nk Je, katika shida yoyote ya kifedha au katika haja ya mkopo wa kuwekeza au unahitaji mkopo kulipa bili yako kutafuta hakuna zaidi kama sisi ni hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani. Sisi kutoa kila aina ya mkopo katika dhehebu lolote fedha kwa kiwango cha 2% bila fee.I upfront wanataka kutumia kati hii kubwa ya kukufahamisha kwamba tuko tayari kukusaidia kwa aina yoyote ya mkopo kutatua kwamba tatizo.Kama yako ya kifedha ndiyo basi kupata nyuma sasa kupitia barua pepe (rahelcohranloan@gmail.com) kwa maelezo zaidi, wewe ni sana makala.

    ReplyDelete

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!