Wednesday, February 22, 2017

WANARIADHA WA KIMATAIFA  KUSHIRIKI MASHINDANO YA KILI -MARATHON
Na Stella Kalinga

Wanariadha wawili wa Kimataifa kutoka katika jimbo la Hanover  Nchini Ujerumani wanatarajia kushiriki  mashindano ya riadha ya Kilimanjaro Marathon yatakayofanyika  Februari 26 mwaka huu, Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni moja kati ya ushirikiano baina ya Ujerumani na Tanzania.

Akifungua mafunzo ya siku moja ya makocha na walimu wa michezo  mbalimbali kutoka  mikoa minne ya kanda ya Ziwa ,Rais wa Shirikisho la Riadha Nchini ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka aliwataja wanariadha hao kuwa ni Christin Kulgemeyer na Stephan Immega ambao watakuwa chachu ya kuwatia moyo wanariadha wengine wa  Kitanzania 
.
Mtaka alibainisha kuwa licha ya kushiriki mashindano hayo,wanariadha hao watapata fursa ya kuona Mlima Kilimanjaro ikiwa ni moja kati ya kuitangaza Tanzania na vivutio vyake.

Aidha katika ufunguzi huo Mtaka  aliwataka makocha na viongozi wa michezo mbalimbali kutoka mikoa ya Simiyu,Mwanza,Mara na Shinyanga kuyatumia mafunzo hayo vizuri ili kujenga mtazamo chanya wa kimichezo katika mikoa ya kanda ya Ziwa.

Aliongeza kuwa viongozi hao wanapaswa kutambua kuwa riadha inakuwa ni moja kati ya njia ya kuitangaza nchi kwa Mataifa nyingine ikiwa ni pamoja na kujenga ushirikiano baina ya Mkoa wa Simiyu na jimbo la Hanover Nchini Ujerumani.

“Kupitia wanariadha hawa imekuwa faraja kuona  Tanzania riadha inakuwa ni sehemu ya kuitangaza nchi yetu, kwa sababu hawa wanariadha wametoka Ujerumani kuja kushiriki mashindano ya Kilimanjaro Marathoni mwaka huu 2017, ikiwa ni pamoja na kuwa sehemu ya ushirikiano kati ya Mkoa wa Simiyu na Jimbo la Hanover Ujerumani” alisema

Hata hivyo wanariadha hao wameonyesha kufurahishwa na kuanzishwa kwa ushirikiano wa kimichezo baina ya nchi yao na Mkoa wa Simiyu kwani wanaamini watajifunza mengi kutokana na kubadilishana uzoefu na kuifanya micheczo kuwa na nafasi kubwa Duniani.

Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akifungua mafunzo ya Makocha na Walimu wa Michezo mbalimbali kutoka Mikoa ya Simiyu, Mwanza, Mara na Shinyanga.
Mwanariadha wa kike Christin Kulgemeyer lutoka Ujerumani anayetarajiwa kushiriki Kilimanjaro Marathon akizungumza na Makocha na Walimu wa Michezo mbalimbali kutoka Mikoa ya Simiyu, Mwanza, Mara na Shinyanga walio katika mafunzo mjini Bariadi.
Mwanariadha wa kiume kutoka Ujerumani Stephan Immega anayetarajiwa kushiriki Kilimanjaro Marathon akizungumza na Makocha na Walimu wa Michezo mbalimbali kutoka Mikoa ya Simiyu, Mwanza, Mara na Shinyanga walio katika mafunzo mjini Bariadi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi inayoshughulikia Michezo Nchini Ujerumani, Lowest Saxon Sports Association (LSB), Ndg .Reinhard Rawe akizungumza Makocha na Walimu wa Michezo mbalimbali kutoka Mikoa ya Simiyu, Mwanza, Mara na Shinyanga walio katika mafunzo mjini Bariadi.
Baadhi ya Makocha na Walimu wa Michezo mbalimbali kutoka Mikoa ya Simiyu, Mwanza, Mara na Shinyanga walio wakimsikiliza Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati akifungua  mafunzo kwa washiriki hao mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!