Thursday, February 23, 2017

RC MTAKA ASEMA WAKUU WA SHULE HAWATASIMAMISHWA KUTOKANA NA MATOKEO MABAYA PEKEE.

Na Stella Kalinga
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo haitawasimamisha kazi walimu wakuu na wakuu wa shule kutokana na matokeo mabaya ya shule zao, isipokuwa kwa uthibitisho wa taarifa za wadhibiti ubora wa elimu kuwa hawafai kushika nyadhifa hizo.

Mtaka ameyasema hayo leo ktk ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili ya kuboresha utendaji kwa wajumbe wa kamati za Shule za Msingi mkoani humo ktk ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Bariadi

Amesema suala la matokeo ya mitihani ya kitaifa kuwa mabaya lawama hazipaswi kwenda kwa walimu pekee kwa kuwa wazazi, kamati za shule, walimu na wanafunzi kila mmoja ana wajibu wake.

"Kuna wanafunzi wameshindikana hawawatii walimu, wazazi nao wanatetea ubovu wa watoto wao, halafu wakifeli mwalimu asimamishwe, hii haitawezekana kabisa; kwa nini  kamati za shule zisiwajibishwe" alihoji Mtaka.

Amesema ikiwa taarifa za wadhibiti ubora wa elimu zitaonesha kuwa mwalimu Mkuu au Mkuu wa shule amefanya kazi ktk kiwango kinachomfanya  apoteze sifa za kuwa katika nafasi yake, Wakurugenzi wa Halmashauri ambao ndio mamlaka yao ya nidhamu watawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria za utumishi wa Umma.

Ameongeza kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri wanapaswa kuwawezesha wadhibiti ubora kupita na kukagua shule zote, ili taarifa zao ziwe kichocheo cha kuchukua hatua kwa walimu wakuu,wakuu wa shule na kamati za shule.

Wakati huo huo Mtaka ameishauri Wizara yenye dhamana na Elimu kuacha utaratibu wa kufanya mabadiliko ya mara kwa mara ya mitaala ya Elimu ili kudhibiti ubora wa elimu hapa nchini.

Kwa upande wake Mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu(ADEM) Ndg.Adam Mnyavanu amesema  mafunzo hayo yatasaidia kutatua changamoto ya wazazi kutotambua nafasi yao katika elimu na kupitia kamati za shule wazazi watatambua wajibu wao katika maendeleo ya elimu.

Vile vile Mnyavanu ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kutenga fedha za kuwawezesha wadhibiti ubora kutekeleza majukumu yao ipasavyo katika bajeti za Halmashauri na kuhakikisha fedha hizo zinatumika kama ilivyokusudiwa kwa lengo la kuinua ubora wa elimu.

Mafunzo kwa wajumbe wa kamati za shule yaliyofadhiliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la EQUIP Tanzania, yamehusisha pia wataalam wa elimu ngazi ya Mkoa na wilaya na yamelenga kuwaelimisha wajumbe hao juu ya muundo wa kamati za shule, majukumu yake, namna wajumbe wanavyopatikana na umuhimu wa kamati hizo katika Maendeleo ya Elimu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akifungua mafunzo ya kuboresha utendaji wa Wajumbe wa Kamati za Shule za Msingi Mkoani humo ambayo yamefanyika leo Mjini Bariadi .
Baadhi ya Washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akifungua mafunzo ya kuboresha utendaji wa Wajumbe wa Kamati za Shule za Msingi Mkoani humo ambayo yamefanyika leo Mjini Bariadi .
Mkufunzi kutoka Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu(ADEM) Ndg.Adam Mnyavanu akizungumza na wataalam wa Elimu na wajumbe wa Kamati ya Shule za Msingi katika mafunzo yaliyofanyika Mjini Bariadi.
Mkufunzi kutoka Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu(ADEM) Ndg.Adam Mnyavanu akizungumza na wataalam wa Elimu na wajumbe wa Kamati ya Shule za Msingi katika mafunzo yaliyofanyika Mjini Bariadi.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (wa kwanza kushoto kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa  mafunzo ya kuboresha utendaji wa Wajumbe wa Kamati za Shule za Msingi Mkoani humo ambayo yamefanyika leo Mjini Bariadi



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!