Friday, March 3, 2017

DC BARIADI:ASKARI WANAOJIHUSISHA NA UJANGILI WACHUKULIWE HATUA

Na Stella Kalinga
Serikali Mkoani Simiyu imetoa wito kwa Taasisi zinazoshughulika na Ulinzi na Hifadhi ya Wanyamapori kuwachukulia hatua askari Wanyamapori wanaojihusisha kwa namna moja ama nyingine  na vitendo vya Ujangili.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Festo Kiswaga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi katika Maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori duniani, yaliyofanyika Mjini Bariadi, ambayo yameenda sambamba na zoezi la upandaji miti katika Hospitali Teule ya Mkoa(Somanda).

Kiswaga amesema baadhi ya askari wanyamapori wamekuwa wakivujisha siri za kukabiliana na majangili hali inayosababisha Serikali kupata hasara kutokana na ujangili kuongezeka na hivyo ameshauri askari hao kuchukuliwa hatua bila kuonewa haya.

 “Upo udhaifu kwa baadhi ya  walinzi na askari ambao tumewapa dhamana ya kulinda wanyamapori, nitoe tu wito kwamba viongozi waandamizi wa taasisi hizi kwa maana ya TANAPA, Vikosi vya kuzuia Ujangili, itakapotokea kiongozi au askari  yeyote ana mahusianao na hawa amabao ni majangili achukuliwe hatua” amesema.

Ameongeza kuwa pamoja na Serikali kuwawezesha askari wanyamapori kwa silaha za kivita ili kupambana na majangili,  upo umuhimu wa kuwaongezea mafunzo na kuona namna ya kuongeza vikosi vya Intelejensia vitakavyosaidia kuwakamata majangili kabla hawajafanya uharibifu katika hifadhi.

Aidha, Kiswaga ameomba Mashirika yasiyo ya Kiserikali kusaidia vikundi na taasisi zinazijitolea kuelimisha jamii kuondokana na ujangili ili elimu hii iwafikie wananchi wote  kwa ajili ya kuwasaidia kuona umuhimu wa kulinda wanyamapori kwa manufaa yao na Taifa wa ujumla.

Vile vile Kiswaga amewashauri wakazi wa Mkoa wa Simiyu kutumia vizuri fursa ya kuwa karibu na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa kujenga hoteli za kitalii, kufanya kazi za sanaa zitazonunuliwa na watalii pamoja na kuanzisha vilabu vya kupinga masuala ya ujangili kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao na ya mkoa kwa ujumla.

Sambamba na hilo amesisitiza wananchi kuendelea kupanda miti ili kukabiliana na hali ya jangwa na mabadiliko ya Tabia nchi na kuiomba Taasisi ya RAFIKI Wildlife Foundation kuona namna ya kuongeza idadi ya miti katika maadhimisho yajayo.

Naye Mkuu wa Kanda ya Serengeti kutoka Kikosi cha Kuzui Ujangili, Ndg. Said Hassan Mkeni amesema Maadhimisho ya Siku ya wanyamapori imeenda sambamba na upandaji miti kwa sababu miti ni chakula cha wanyamapori, vile vile inasaidia kupata mvua na kuhifadhi mazingira.


Kauli mbiu ya Siku ya Wanyamapori Duniani Mwaka 2017 ambayo yamefanyika Mkoani Simiyu kwa Ufadhili wa Shirika lisilo la Kiserikali la RAFIKI Wildlife Foundation ni “ SIKILIZA SAUTI YA VIJANA KWA UHIFADHI” 
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ambaye pia Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe Festo Kiswaga akipanda mti katika Hospitali ya Mkoa wa Simiyu(Somanda), katika maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori iliyofanyika Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe Festo Kiswaga akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ,Hospitali ya Mkoa  na wananchi, katika maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori yaliyofanyika Mjini Bariadi.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Mhandisi.Hatari Kapufi akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ,Hospitali ya Mkoa  na wananchi, katika maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori yaliyofanyika Mjini Bariadi.
Mkuu wa Kanda ya Serengeti kutoka Kikosi cha Kuzui Ujangili, Ndg. Said Hassan Mkeni akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ,Hospitali ya Mkoa  na wananchi, katika maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori yaliyofanyika Mjini Bariadi.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ambaye pia Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe Festo Kiswaga akisaini Kitabu cha Wageni katika Hospitali ya Mkoa wa Simiyu(Somanda), wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori iliyofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Hospitali ya Mkoa wakipanda mti katika Hospitali ya Mkoa wa Simiyu(Somanda), katika maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori iliyofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Hospitali ya Mkoa wakipanda mti katika Hospitali ya Mkoa wa Simiyu(Somanda), katika maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori iliyofanyika Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!