Monday, March 13, 2017

TAARIFA KWA UMMA

 

                               TAARIFA KWA UMMA
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka anawaalika wananchi na wadau wote wa maendeleo katika Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji mkoani Simiyu utakaofanyika tarehe 15 Machi 2017, katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki Mjini Bariadi kuanzia saa 3:00 asubuhi.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ni Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Adolf Mkenda

Mwongozo wa uwekezaji Mkoani SIMIYU unabainisha fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo Mkoani humo na utaongoza uandaaji na utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Mkoa na Halmashauri zake.

Aidha, Mwongozo unakusudia kutekeleza azma ya Serikali ya Tanzania ya Viwanda  kama ilivyofafanuliwa katika Mpango wa pili wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano (2016/2017 – 2020/2021) na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025.

Pamoja na mambo mengine mpango huu unabainisha taarifa mahususi kwa makampuni na watu binafsi kutoka ndani na nje nchi, wenye nia ya kuwekeza  katika maeneo yenye rasilimali nyingi ambazo hazijaanza kutumika (untapped resources) ili kukuza uwezo wa uzalishaji katika sekta zote muhimu Mkoani Simiyu.

Mwongozo huu ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Januari - Februari 2017, katika Halmashauri zote za Mkoa wa Simiyu (Bariadi Vijijini, Bariadi Mjini, Busega, Itilima,Maswa na Meatu) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)

Imetolewa na:
Stella A. Kalinga
Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Simiyu
13 Machi, 2017.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!