Wednesday, March 15, 2017

Viongozi na Watendaji Watakiwa kutowabugudhi Wafanyabiashara

Na Stella Kalinga

Serikali imewataka viongozi wa kisiasa pamoja na watendaji wa Serikali kutotumia vibaya madaraka yao kwa kuwanyanyasa na kuwasumbua wafanyabishara hasa wazawa waliowekeza ndani ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda akiwa mkoani Simiyu, wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji wa mkoa pamoja na Tovuti ya Mkoa.

Profesa Mkenda amesema viongozi hao wanatakiwa kuwajengea wafanyabiashara mazingira rafiki yatakayowawezesha kufanya biashara zao kwa amani ili kuweza kukuza uchumi wa Taifa na kuongeza ajira kwa vijana.

Aidha, amewasihi viongozi wote wa Serikali ngazi za Mikoa na wilaya hapa nchini  kujivunia uwepo wa wajasiriamali na wafanyabiashara wakubwa ambao ni wazawa kwani wao ni chachu ya kuongezeka kwa ajira za vijana.

Amesema kuwa si vyema wafanyabishara kutukanwa, kutolewa lugha zisizokuwa sahihi na kuonekana kama wana uadui na Serikali, badala yake watengenezewe mazingira mazuri  ili waweze kulipa kodi na kufuata sheria na taratibu za nchi.

“ Hawa wafanyabishara hasa wazawa na wajasiliamali tuwaone kama wenzetu, ndugu zetu na watu muhimu, kwani wameajiri vijana wetu, wanalipa kodi ili nchi ipate maendeleo, lakini wanatekeleza kauli mbiu ya Rais , Tanzania kuwa nchi ya viwanda, tuwathamni” alisema Adolf.

Mbali na hilo Katibu Mkuu huyo amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatenga maeneo kwa ajili ya wawekezaji wakubwa na wadogo kwa ajili ya kujenga viwanda.

Awali akiongea katika Mkutano huo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa ili Tanzania iweze kufanikiwa katika azma yake ya kuwa na viwanda lazima Serikali iwekeze kwanza katika utafiti wa fursa zilizopo.

Mtaka amesema kuwa kuwekeza katika utafiti kutasaidia kutoa uthubutu wa kufanya na kutenda mambo mbalimbali yatakayoifanya nchi kuwa na uchumi wa kati na kuwaletea wananchi maendeleo.

“ Nchi hii tusingelihitaji kuona wakuu wa mikoa kuwa wabobezi katika kila sekta na badala yake wawaache wataalam na watafiti wafanye kazi zao kitaalamu ili kuepuka mvurugano wa shughuli za kimaendeleo ndani ya nchi” amesema Mtaka.

Kwa upande wake Mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Dk Gratian Bamwenda, amesema kukamilika kwa utafiti huo ambao umetoa mwongozo wa uwekezaji mkoani Simiyu kutatoa fursa kwa wananchi na wafanyabishara kutambua fursa na kuwekeza.


Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu ambao umezinduliwa rasmi leo ni matokeo ya Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala Kiuchumi na Kijamii (ESRF) katika halmashauri zote sita za mkoa wa Simiyu chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP); umebainisha takribani fursa 26 za uwekezaji katika sekta zote muhimu mkoani humo.
Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda(wa pili kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(wa pili kulia) wakionesha Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu kwa wadau wa Maendeleo wa Mkoa huo mara baada ya uzinduzi uliofanyika Machi, 15, Mjini Bariadi.
Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakiwa wameshika nakala za Mwongozo wa Uwekezaji ikiwa ni maandalizi ya kufanya uzinduzi wa mwongozo huo Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katika) akizungumza jambo na Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda(kuhoto) na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa kiuchumi na Kijamii(ESRF),Dkt.Tausi Kida (kulia)wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu uliotokana na Utafiti wa Taasisi hiyo.
Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Viongozi, watendaji na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu (hawapo pichani) wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani humo.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa kiuchumi na Kijamii(ESRF),Dkt.Tausi Kida akizungumza na Viongozi, watendaji na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu (hawapo pichani) wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani humo.
Mbunge wa Jimbo la Itilima ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Mkoani Simiyu, Mhe.Njalu Silanga akichangia jambo katika mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu Uliofanyika leo Mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko akichangia jambo katika mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu Uliofanyika Mjini Bariadi.
 Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi, Mhe. Mashimba Ndaki akichangia jambo katika mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu Uliofanyika Mjini Bariadi.

Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP) Hawa Dabo akizungumza na Viongozi, watendaji na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu ( baadhi hawapo pichani) wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani humo.
Kaimu Afisa TEHAMA wa Sekretarieti ya Mkoa, Bw.Edgar Mdemu(kushoto)  akimuonesha  Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda(wa pili kushoto) na viongozi wengine Tovuti ya Mkoa wa Simiyu, inayotambulika kwa anuani ya www.simiyu.go.tz kabla ya kuizindua leo Mjini Bariadi.
Baadhi ya Viongozi wakimsikiliza Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda( hayupo pichani) katika mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu Uliofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda( hayupo pichani) katika mkutano wa Uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Simiyu Uliofanyika Mjini Bariadi.
Katibu mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyuna baadhi ya wadau wa maendeo wa mkoa huo mara baada ya uzinduzi wa Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa huo Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!