Saturday, July 8, 2017

WANANCHI WAHIMIZWA KUPENDA BIDHAA ZINAZOZALISHWA NCHINI

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2017 Ndg. Amour Hamad Amour ametoa wito kwa wananchi kupenda na kuthamini bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.

Amour ametoa wito huo wakati alipokuwa akitoa ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mara baada ya kuweka jiwe la Msingi Mradi wa kiwanda cha kuongeza thamani ya mazao Kilimo cha BUSEGA MAZAO LIMITED katika kijiji cha Mwanangi wilayani Busega.

Amesema wananchi watakapotumia bidhaa zinazozalishwa hapa nchini watasaidia kuongeza uzalishaji kutokana na kuwepo kwa soko la uhakika kwa viwanda na hatimaye kuongeza uchumi wa nchi.

Ameongeza kuwa wawekezaji wanapaswa kuzalisha bidhaa bora ambazo zitakidhi vigezo vya kiushindani sawa sawa na zile zinazotoka nje ya nchi ili kupunguza uingizwaji wa bidhaa za nje na kulifanya Taifa kuongeza pato lake.

“.....bidhaa ambazo zinazotoka nje zinapoingia hapa ndani zinakuwa na bei ndogo kuliko zinazozalishwa hapa nchini, ni  kwa sababu bado hatujajipanga kuzalisha kiushindani, sasa tuzalishe bidhaa zenye ushindani ili kuweza kuua soko la bidhaa ambazo zinatoka nje tuweze kukuza uchumi wa Taifa letu” alisema.

Aidha, amesema mwekezaji wa kiwanda cha BUSEGA MAZAO LIMITED atakapoanza uzalishaji  atoe kipaumbele cha ajira kwa wananchi wa wilaya ya Busega na ahakikishe wanafanya kazi katika hali ya usalama na kupewa haki na maslahi yao kama inavyostahili.

Kiongozi huyo wa Mwenge wa Uhuru 2017  pia amewataka wakazi wa Wilaya ya Busega na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla kuhakikisha kuwa wanazalisha kwa wingi mazao yote yanayotakiwa katika kiwanda hicho ukiwepo mpunga na mahindi kwa kuwa kitatoa soko la uhakika na kupelekea ongezeko la pato la mtu mmoja mmoja.

Akisoma taarifa ya mradi wa kiwanda hicho,Ndg. Lazaro Japhet kutoka BUSAGA MAZAO LIMITED amesema Kiwanda hicho kitawasaidia wakulima kupata soko, kuhifadhi na kuongeza mazao yao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe.Tano Mwera amesema Serikali wilayani humo iko tayari kushirikiana na wawekezaji ambao watakuwa tayari kuwekeza katika wilaya hiyo.

Sambamba na hayo Ndg.Amour Hamad Amour amewataka wananchi kufanya kazi kwa bidii, kulinda rasilimali za nchi na kuendelea kupambana na rushwa, dawa za kulevya, malaria na UKIMWI ili kuweza kufikia Tanzania ya Uchumi wa Kati.

Akizungumza na wananchi na wanafunzi katika Shule ya Sekondari Mkula Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2017 amesisitiza wanafunzi wa shule za sekondari kuwa na Klabu za wapinga rushwa, mapambano dhidi ya dawa za kulevya, malaria na UKIMWI ili waweze kufikia malengo yao.


Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Busega umepitia jumla ya miradi 9 katika sekta ya Elimu, Afya, Maji,Utawala Bora, Viwanda na Maendeleo ya jamii, yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.5.



Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour(wa tano kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa watumishi katika Kiwanda Cha BUSEGA MAZAO LIMITED mara baada ya kuweka jiwe la msingi la kiwanda hicho wilayani Busega

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe.Tano Mwera akipokea mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Salome Mwakitalima tayari kwa kuanza kuukimbiza katika Wilaya yake.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akikagua moja ya vyumba vinne vya madarasa vilivyofunguliwa na Mwenge wa Uhuru katika Shule ya Sekondari Mkula wilyani Busega.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akipanda mti katika Shule ya Sekondari Mkula Wilayani Busega.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akizindua Klabu ya Wapinga Rushwa katika Shule ya Sekondari Mkula Wilayani Busega
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour(kulia) na Mkuu wa Wilaya wakishangilia baada ya Klabu ya Wapinga rushwa kuzinduliwa katika Shule ya Sekondari Mkula.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amourakiangalia moja ya miundombinu ya maji katika Mradi wa Maji wa Lukungu kabla ya kufungua mradi ambao utaanza kwa kuwahudumia takribani wananchi 4022.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akifungua mradi wa Maji wa Lukungu wilayani Busega ambao utaanza kwa kuwahudumia wananchi 4022 na kufikia mwaka 2030 utawahumia wananchi 11,500.
Lazaro Japhet akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kuongeza thamni ya azaoya kilimo cha BUSEGA MAZAO LIMITED kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour(hayupo pichani) kabla ya kuwekwa kwa jiwe la msingi la kiwanda hicho.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akimtwisha ndoo ya maji Mkimbiza Mwenge Kitaifa Salome Mwakitalima mara baada ya kufungua mradi wa Maji wa Lukungu wilayani Busega.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akikata utepe kabla ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda cha kusindika nafaka cha BUSEGA MAZAO LIMITED wilayani Busega.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akiweka jiwe la Msingi kiwanda cha kuongeza thamani ya mazao BUSEGA MAZAO LIMITED wilayani Busega.
Baadhi ya viongozi na wananchi wilaya ya Busega wakimfuatilia Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour(hayupo pichani) akikagua Kiwanda cha BUSEGA MAZAO LIMITED kabla kuweka jiwe la msingi.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe.Tano Mwera akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mwanangi kabla ya kumkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour kutoa ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 baada ya kuweka jiwe la msingi la kiwanda cha BUSEGA MAZAO LIMITED.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akizungumza na kikundi cha wanawake wajasiriamali wakionesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wa Mwaka 2017 ,Ndg.Amour Hamad Amour akizungumza na kikundi cha wanawake wajasiriamali wakionesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!