Monday, June 4, 2018

SIMIYU YAKABIDHIWA ZAHANATI NA SHIRIKA LA LIFE MINISTRY


Shirika la Kikristo la Life Ministry limekabidhi Zahanati kwa Uongozi wa Mkoa wa Simiyu ambayo imejengwa katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi.

Akisoma taarifa ya makabidhiano ya zahanati hiyo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe amesema shirika hilo lilipokea zahanati hiyo kutoka kwa wananchi ambao walianza kujenga kwa nguvu zao na kuifikisha hatua ya renta, hadi kufikia hatua za ukamilishaji wa zahanati hiyo Shirika la Life Ministry limetoa kiasi cha Shilingi milioni 71.

Amesema pamoja na zahanati hiyo, shirika hilo limefanya mengi mkoani Simiyu ikiwa ni apamoja na kutoa vifaa tiba Hospitali Teule ya Mkoa vyenye thamani ya shilingi milioni 40, huduma za macho na kutoa miwani bure, kutoa baiskeli zaidi ya 20 kwa walemavu, kugawa vifaa mbalimbali kwa makundi mbalimbali wakiwemo watoto wenye ualbino, kuwezesha vikundi vya bustani zaidi ya 40 katika kilimo cha umwagiliaji kwa njia ya matone na kuchimba visima virefu 12 vyenye thamani ya shilingi milioni 300.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameishukuru Life Ministry kwa msaada wa zahanati hiyo na kuwahakikishia kuwa mara tu itakapokamilika Serikali itahakikisha Zahanati hiyo inafanya kazi na itapeleka watoa huduma za afya ili wananchi waanze kupata huduma.

"Niwakikishie tu kuwa Serikali itahakikisha Zahanati hii inafanya kazi kwa kuleta wataalam na bahati nzuri Serikali imekubali kuajiri watu wa Sekta ya Afya" alisema Mtaka.

Mtaka amesema Taasisi za Dini zimekuwa zikiunga mkono kazi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na akaiomba Life Ministry kuendelea kusaidia katika ujenzi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya, ili kusaidia uboreshaji wa huduma za Afya mkoani Simiyu, kwa kuwa mkoa huo una uhitaji  mkubwa wa vituo vya afya.

" Mkoa wetu tuna asilimia chini ya 40 ya vituo vya Afya, Kama ni jambo ambalo litakuwa ndani ya uwezo wa Taasisi ningeomba muendelee kutusaidia kwenye sekta ya Afya; zipo juhudi za Serikali katika uimarishaji wa sekta ya Afya hususani kwenye ujenzi wa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali lakini washirika kama Taasisi za Dini bado tunawahitaji kwa kuwa mmekuwa mkono wa pili kwenye kuunga mkono juhudi za Serikali" alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa Itubukilo, Diwani wa Kata ya Itubukilo Mhe. Mayanda Makenzi akiishuku Life Ministry kwa kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo ambayo amesema itawaondolea adha wananchi wake kutembea mwendo mrefu kufuata huduma za Afya.

Naye Diwani wa Viti Maalum Mhe. Juliana Lucas amesema ukamilishaji wa zahanati hiyo utawasaidia sana wananchi kupata huduma karibu hususani wanawake ambao watapata huduma za afya ya uzazi na kupata msaada wa karibu wakati wa kujifungua na hivyo kupunguza vifo vya wakina mama na watoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bw. Abdallah Malela amesema Zahanati hiyo ya Itubukilo itafunguliwa rasmi na kuanza kutoa huduma Julai Mosi, 2018.

MWISHO


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akikata utepe kuashiria kupokea Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry katika Kijiji cha Itubukilo Wilayani Bariadi  ambayo ilikabidhiwa rasmi kwa Serikali na Shirika hilo Juni 03, 2018.
Mkuu wa Mkoawa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akifurahia jambo na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Viongozi wa Life Ministry naViongozi wa madhehebu ya Kikristo baada ya makabidhiano ya Zahanati ya Itubukilo kati ya Serikali na Shirika la Life Ministry ambayo imejengwa na Shilika hilo, Juni 03, 2018. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(wa pili kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe(kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Life Ministry Tanzania, Mhandisi. Kapuulya Musomba (katikati) wakati wa hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika hilo katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka na baadhi ya viongozi wa madhehebu ya dini ya Kikristo wakitoka kukagua jengo la Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry Tanzania katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi ambayo ilikqbidhiwarasmi Juni 03, 2018 kwa Serikali ya Mkoa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Utubukilo wilayani Bariadi wakati wa hafla ya makabidhiano ya Zahanati iiliyojengwa na Life Ministry Tanzania Juni 03, 2018.
Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe(kushoto) akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa Zahanati ya Itubukilo ambayo imejengwa na shirika hilo la Kikristo na kukabidhiwa kwa Serikali Juni 03, 2018.
Diwani wa Kata ya Itubukilo, Mhe. Mayanda Makenzi akizungumza na wananchi Kijiji cha Utubukilo wilayani Bariadi wakati wa hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Life Ministry Tanzania Juni 03, 2018.
Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mheAnthony Mtaka, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bw. Abdallah Malela na Katibu wa CCM Wilaya ya Bariadi wakiteta jambo wakati wa makabidhiano ya Zahanati ya Itubukilo na Shrika la Life Ministry.
Viongozi wa Shirika la Life Ministry na viongozi wa Chama na Serikali wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya Pamoja mara baada ya hafla ya makabidhiano ya Zahanati katika Shirika Hilo na Serikali ambayo imejengwa katika Kata ya Itubukilo Wilayani Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya Kikristo na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Itubukilo katika hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry Juni 03, 2018.
Diwani wa Viti Maalum, Mhe. Juliana Lucas akimkabidhi  Mwenyekiti wa Bodi ya Life Ministry Tanzania, Mhandisi. Kapuulya Musomba zawadi ya Kitenge kwa niaba ya waananchi wa Itubukilo kama ishara ya kumshukuru kwa kuruhusu Shirika hilo Kujenga Zahanati ya Itubukilo wilayani Bariadi katika hafla ya makabidhiano ya Zahanati hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe(kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Life Ministry Tanzania, Mhandisi. Kapuulya Musomba (katikati) baada ya hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika hilo katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi, Juni 03, 2018.
Diwani wa Viti Maalum, Mhe. Juliana Lucas akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Mhe. Anthony  Mtaka zawadi ya Kitenge kwa niaba ya wananchi wa Itubukilo kama ishara ya kumshukuru kwa namna anavyopigania maendeleo ya wananchi wake  wakati wa makabidhiano ya Zahanati ya Itubukilo wilayani Bariadi iliyojengwa na Shirika la Kikristo la Life Ministry.
Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya Kikristo, wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Wajumbe kutoka Shirika la Life Ministry wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji chaItubukilo katika hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry Juni 03, 2018. 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!