Friday, September 11, 2020

KITUO CHA AFYA LUKUNGU CHATAKIWA KUIMARISHA MFUMO WA UKUSANYAJI, USIMAMIZI WA MAPATO

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba ameutaka uongozi wa Kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega kuimarisha ukusanyaji na usimamizi wa mapato (kudhibiti upotevu wa mapato) ili kuongeza mapato yatakayosaidia kununua dawa na kuboresha miundombinu kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Kulemba ameyasema hayo Septemba 10, 2020 katika nyakati tofauti wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi iliyofanyika katika kituo hicho, ambapo moja ya malengo ya ziara ilikuwa ni kukagua mifumo ya ukusanyaji wa mapato na hali ya utoaji wa huduma za afya kwa ujumla wake.

“Imarisheni mfumo wa ukusanayaji mapato nataka wakati ujao mapato yaongezeke mara mbili ya sasa, mkumbuke kuwa kwa kadri tunavyodhibiti upotevu wa mapato ndiyo tutakavyoboresha utoaji wa huduma; tutaweza kununua dawa na kufanya maendeleo ya kituo chetu hali itakayochangia kuongeza ufanisi katika huduma zinazotolewa kwa wananchi,” alisema Kulemba.

Ameongeza kuwa Uongozi wa Kituo hicho unapaswa kuhakikisha kuwa mfumo wa GoT-HOMIS unaohusika na usimamizi na uendeshaji wa vituo vya kutolea huduma za afya unafungwa na kufanya kazi kituoni hapo, ili kudhibiti aina yoyote ya upotevu wa mapato kwa kuwa taarifa ya kila huduma na mapato zitaingizwa katika mfumo huo.

Naye Afisa Afya kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema pamoja na kuimarisha mfumo wa mapato uongozi huo uboreshe mazingira kwa kusafisha mara kwa mara maeneo ya kituo hicho pamoja na kupanda bustani za maua.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi wa idara ya afya wilaya ya Busega, Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya amesema watatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na mganga mkuu wa mkoa ili kutimiza azma ya serikali ya kutoa huduma zinazotakiwa kwa wananchi na kwa wakati.

Baadhi ya wananchi waliopata huduma za matibabu katika kituo cha afya Lukungu wameupongeza uongozi wa kituo kwa namna ulivyoboresha utoaji wa huduma na kuomba hali ya upatikanaji wa dawa iimarishwe zaidi na miundombinu ya kutoa huduma ikiwemo huduma za upasuaji, wodi za kulaza wagonjwa ziongezwe  ili wapate huduma zote kituoni hapo.

“ Kwa upande wa huduma mimi nimehudumiwa vizuri, nimepokelewa vizuri na wauguzi wamenisikiliza baada ya kunisikiliza nimeenda kwenye vipimo na nilivyorudi kwa daktari amenieleza tatizo langu akaniandikia dawa,  nashukuru dawa zote nilizoandikiwa nimepewa,” Mandege William Manyama, mkazi wa Kijiji cha Lukungu.

“Huduma zote nilizokuwa nazihitahitaji nimezipata na nimehudumiwa ndani ya muda mfupi, ombi langu serikali ione namna ya kuongeza huduma hasa za kulaza wagonjwa ili tuipate hapa hapa badala ya kupelekwa kwenye vituo vingine na hospitali,” alisema Daud Moshi mkazi wa Kijiji cha Lukungu.

MWISHO


Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba(katikati) akitoa maelekezo kwa  baadhi ya watoa huduma za afya katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega wakati akiwa katika ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba(kulia) akifanya ukaguzi katika wodi ya wazazi katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega wakati akiwa katika ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba akitoa maelekezo kwa  baadhi ya watoa huduma za afya katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega wakati akiwa katika ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.

Mfamasia wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega akichangia jambo katika kikao kati ya Timu ya Usimamizi wa Huduma za Afya ya Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Busega pamoja na watumshi wa Kituo cha Afya Lukungu wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10, 2020.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba(katikati) akitoa maelekezo kwa  baadhi ya watoa huduma za afya katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega wakati akiwa katika ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.

Baadhi ya wananchi wakisubiri huduma katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega.

Jengo la huduma za wagonjwa wa nje katika Kituo cha Afya cha Lukungu wilayani Busega

Baadhi ya watoa huduma za afya katika kituo cha afya cha Lukungu wakimsikiliza Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba(hayupo pichani) wakati akitoa maelekezo kwa  watoa huduma hao wakati akiwa katika ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.

Afisa Afya katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu  akichangia jambo katika kikao kati ya Timu ya Usimamizi wa Huduma za Afya ya Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Busega pamoja na watumshi wa Kituo cha Afya Lukungu wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10, 2020.

Afisa Afya katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu  akichangia jambo katika kikao kati ya Timu ya Usimamizi wa Huduma za Afya ya Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Busega pamoja na watumshi wa Kituo cha Afya Lukungu wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10, 2020.

Moja ya majengo ya kutolea huduma katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega.

Wodi ya wazazi katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega.



Baadhi ya Maafisa wa Idara ya Afya mkoa wa Simiyu na Wilayani ya Busega na watoa huduma za afya katika kituo cha afya cha Lukungu wakimsikiliza Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba(hayupo pichani) wakati akitoa maelekezo kwa  watoa huduma hao wakati akiwa katika ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.


Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba na Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Busega wakifuatilia kikao cha Idara ya Afya mkoa wa Simiyu na Wilayani ya Busega na watoa huduma za afya katika kituo cha afya cha Lukungu kilichofanyika wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba(kulia) akitoa maelekezo kwa  baadhi ya watoa huduma za afya katika kituo cha Afya Lukungu wilayani Busega wakati akiwa katika ziara ya usimamizi shirikishi katika kituo hicho Septemba 10,  2020.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!