Friday, November 23, 2018

WAFANYABIASHARA WA UTURUKI WAONESHA NIA YA KUWEKEZA KATIKA KIWANDA CHA NGUO SIMIYU

Wafanyabiashara kutoka nchini Uturuki wameonesha nia na dhamira ya kuwekeza katika ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza nguo mkoani Simiyu ambacho kitakuwa na uwezo wa kuajiri watu zaidi ya 4000.


Hayo yamebainishwa katika kikao kati ya Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo ambaye aliambatana na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara wa Uturuki kutoka makampuni saba ya nchi hiyo, katika kikao maalum na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Wakuu wa Taasisi mbalimbali na jumuiya ya wafanyabiashara ya mkoa wa Simiyu, kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi.

Balozi Kiondo amesema Wafanyabiashara hao wanayo azma ya kuwekeza katika kiwanda cha kutengeneza nguo katika mnyororo mzima wa utengenezaji kutoka bidhaa ya awali ya pamba mpaka bidhaa ya mwisho kabisa, ambayo ni nguo kwa ubia(partineship) na Watanzania.

Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS amesema  mpaka sasa ni makampuni sita kutoka nchini humo yameonesha nia ya kuwekeza katika kiwanda cha nguo mkoani Simiyu na akaahidi kwenda kuwashawishi wafanyabiashara wenzake hivyo watakaporudi kwa mara nyingine  makapuni mengi yatakuja kuwekeza katika viwanda vya nguo.

“Nikirudi nyumbani kama kiongozi wa wafanyabiashara nitawashawishi wengine pia waje wawekeze katika viwanda vya nguo,ombi langu kwenu ni kwamba ninahitaji Mfanyabiashara Mtanzania ambaye tutashirikiana naye katika uwekezaji huu(partinership), lakini niwahakikishie tu kuwa katika kiwanda tutakachojenga mashine na vifaa vyote vipo tayari kule Uturuki” alisema  Cengiz.

Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka amewahakikishia wafanyabiashara hao upatikanaji wa soko la uhakika la nguo zitakazotengenezwa, pamoja na upatikanaji wa malighafi kwa kuwa Simiyu ndiyo mkoa unaozalisha zaidi ya asilimia 55 ya pamba yote nchini, ambapo kwa  mwaka 2018 Simiyu imezalisha takribani kilo milioni 131.

Ameongeza kuwa pamoja na uhakika wa soko na malighafi  Simiyu ina viwanda vingi  vya kuchambua pamba, ardhi itatolewa bure, miundombinu muhimu yote ipo, utashi wa kisiasa kwa viongozi wa wilaya upo, hivyo akawatoa hofu wawekezaji hao na kuwaeleza kuwa mkoa utashirikiana nao, huku akiomba waone uwezekano wa kuwekeza katika uongezaji thamani wa mazao ya mifugo kama ngozi na nyama

Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery, Bw. Boaz Ogola amesema wako tayari kushirikiana na mwekezaji huyo, huku akibainisha kuwa kuanzishwa kwa kiwanda hicho kitawasaidia wanaochambua pamba na wakulima kupata faida ikilinganishwa na sasa ambapo zaidi ya asilimia 75 ya pamba inasafirishwa nje ya nchi.

Naye Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu, Mhe. Najlu Silanga ameahidi ushirikiano kwa wawekezaji aho kutoka Uturuki na kuiomba Wizara ya Viwanda, Baiashara na Uwekezaji kuzitambu na kusughuliakia changamoto mbalimbali za wafanyabiashara hapa nchini .

Wakati huo Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda  (TIRDO) Prof. Mkumbukwa Mtambo amepongeza Mkoa wa Simiyu kwa kuzingatia Utafiti na maendeleo katika Viwanda, huku akisisitiza kuwa ili viwanda vinavyoanzishwa viweze kuwa endelevu ipo haja ya kufanya utafiti na maendeleo na akaahidi kuwa Taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Simiyu katika tafiti mbalimbali  za  maendeleo ya viwanda.

MWISHO




Kutoka kulia Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Edwin Mhede wakiteta jambo mara baada ya kumalizika kwa kikao kati ya viongozi na watendaji wa Serikali na ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Mwenyekiti na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi.

Mwenyekiti na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS, 

akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo katika kikao kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi  
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni Mbunge wa Itilima, Mhe. Njalu Silanga akichangia hoja katika viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Mwenyekiti na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery, Bw. Boaz Ogola akichangia hoja katika viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo akizungumza viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali katika kikao kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo unaotarajiwa kufanywa na Wafanyabiashara kutoka nchini Uturuki katika mkoa wa Simiyu.




Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu kushoto)  akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo(wa pili kushoto), na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na  mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS( wa tatu kulia),  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Edwin Mhede( wa pili kulia) na viongozi wa Serikali pamoja na wafanyabiashara wa mkoa huo, mara baada ya kuhitimisha kikao mjini Bariadi kilichofanyika kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera akichangia hoja katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.

Bw. Gungu Silanga mmoja wa wafanyabiashara mkoani Simiyu, akichangia hoja katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akichangia hoja katika kikao cha  viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda(TIRDO), Prof. Mkumbukwa Mtambo, akichangia hoja katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Diwani wa Kata ya Zanzui Wilayani Maswa, Mhe. Jeremia Shigala akichangia hoja katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo  (SIDO) Prof. Sylvester Mpanduji, akichangia hoja katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Kutoka kushoto Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Edwin Mhede, Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini wakionesha nakala za Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Simiyu, baada ya viongozi hao kukabidhiwa mwongozo huo Novemba 22, 2018.
Afisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Kija Kayenze akiwasilisha taarifa ya fursa za uwekezaji katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa taarifa ya mkoa wakati wa ugeni wa Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo aliyembatana na, Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki Bw. Cengiz ERTAS, Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi.
Bw. John Sabo mmoja wa wafanyabiashara mkoani Simiyu, akichangia hoja katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu kushoto)  akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo(wa pili kushoto), Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS (wa nne  kulia),  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Edwin Mhede( wa tatu kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo  (SIDO) Prof. Sylvester Mpanduji(kulia) na viongozi wengine wa Serikali wa mkoa huo, mara baada ya kuhitimisha kikao mjini Bariadi kilichofanyika kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo.




Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akichangia hoja katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza katika kikao cha viongozi wa Mkoa wa Simiyu, baadhi ya viongozi wa Taasisi za Serikali, Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS,  kilichofanyika Novemba 22, 2018 Mjini Bariadi.
Kushoto Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara na mwakilishi wa Wafanyabiashara kutoka Uturuki, Bw. Cengiz ERTAS na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, ( kulia) Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Edwin Mhede wakiteta jambo, mara baada ya kuhitimisha kikao mjini Bariadi kilichofanyika kujadili uwekezaji katika viwanda vya nguo.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!