Saturday, October 10, 2020

WAZAZI, WALEZI WAPUNGUZIENI KAZI WANAFUNZI WA MADARASA YA MITIHANI: RC MTAKA

    Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwapunguzia kazi  wanafunzi wenye madarasa ya mitihani ya Taifa ya darasa la nne, kidato cha pili na kidato cha nne ambayo inatarajiwa kufanyika mwezi Novemba ili waweze kujipatia muda mwingi wa kujisomea kujiandaa na mitihani hiyo. 

Mtaka ameyasema hayo jana  wakati makabidhiano ya Chuo cha Ufundi Kasoli katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi kilichojengwa na mwekezaji Alliance Ginnery Limited na kukabidhiwa kwa Serikali na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Dkt. Maduhu Kazi kwa niaba ya kampuni hiyo na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa niaba ya wananchi. 

“Darasa la saba wameshafanya mtihani wao, watoto wa darasa la nne, kidato cha pili na kidato cha nne waendelee kufanya maandalizi, wazazi na walezi wapunguzieni kazi watoto wote walio kwenye madarasa haya na wakiwa nyumbani wafanye majadiliano ya pamoja,” alisema Mtaka. 

Aidha, Mtaka amewaonya wazazi na walezi wenye nia ya kuwaozesha wanafunzi wa kike waliohitimu elimu ya msingi na kutoa wito kwa jamii yote kuwa walinzi wa watoto wa kike ili waweze kutimiza ndoto zao. 

Mtaka ameishukuru Kampuni ya Allience Ginnery kujenga chuo cha ufundi Kasoli na kutoa wito kwa wasichana na wanawake kijiji cha Kasoli kujitokeza kupata mafunzo ya ushonaji bila malipo katika chuo hicho katika kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba, kabla ya kuanza kwa mafunzo yatakayoanza mwakani kwa mtaala wa Serikali na kuahidi kutoa vyerehani 25. 

Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola amesema Kampuni hiyo imekuwa inajihusisha sana na maendeleo ya jamii katika sekta ya elimu, afya na maji kwa kuwa wao ni sehemu ya jamii, ni wajibu wao  kufanya hivyo na ni sehemu ya maelekezo ya TIC wanayopewa wawekezaji wote.

“Tunashiriki kwenye masuala ya jamii kwa sababu sisi ni sehemu ya jamii, sisi tunashughulika na wakulima na wanaotulimia pamba na kutuuzia kutuwezesha kuendesha kiwanda chetu, siku za nyuma tulijikita kwenye afya, maji na elimu ya msingi na sekondari; tumeona haja ya kujenga chuo cha ufundi ili wanafunzi watakaoshindwa kuendelea na masomo, wapate mafunzo  ya ufundi ili waweze kujitegemea,” alisema Ogola.

Aidha, Ogola amesema pamoja na mafunzo ya ufundi mipango ya baadaye ya kampuni ya Alliance Ginnery kuongeza darasa moja la wakulima kwa lengo la kutoa warsha na mafunzo kwa wakulima ili waweze kulima kilimo chenye tija ili kampuni hiyo iweze kupata malighafi bora kwa ajili ya kiwanda chake cha kuchambua pamba..

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Dkt. Maduhu Kazi ameipongeza na kuishukuru Kampuni ya Alliance Ginnery kujenga chuo cha Ufundi na kutoa wito kwa wawekezaji wengine kuona umuhimu wa kuwafikia wananchi walio katika maeneo yao huku akiahidi kuwa TIC itahakikisha kinakuwa mstari wa mbele kutatua changamoto zinazowakabili wawekezaji. 

“TIC inashirikiana na Serikali hata ngazi ya mikoa na tumejielekeza zaidi kuongeza ufanisi katika shughuli zetu za kuwasaidia wawekezaji masuala ya vibali kwa kushirikiana na Taasisi zinazohusika; pia tumejipanga hata kuwafikia wawekezaji wadogo Watanzania maana baada ya tathmini tumeona eneo hilo kuna mapungufu maana wengi wanadhani sisi tunahusika na wawekezaji wa kigeni tu,” alisema Dkt. Kazi.

Naye Mkazi wa Kijiji cha Kasoli Shamsa Abdallah amesema anaishukuru Kampuni ya Alliance Ginnery kwa kuwajengea chuo cha ufundi na anaamini kuwa kitawasadia kwenye mafunzo ya ushonaji  na mafunzo yanayohusiana na kilimo yatakayowasaidia kujikwamua kiuchumi.

Kampuni ya Alliance Ginnery Limited imejenga majengo ya chuo cha ufundi kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 180, kuchimba kisima cha maji chenye uwezo wa kutoa lita 5000 kwa saa pamoja na kuweka vifaa kama vyerehani, majiko ya gesi  na vifaa mbalimbali vya kujifunzia upishi,vifaa vya kujifunzia uashi na useremala meza na viti vya ofisi.

MWISHO

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi (wa tatu kulia) akikata utepe kufungua chuo cha  ufundi Kasoli  iliyojengwa  kwa msaada na Mwekezaji wa Kampuni ya Alliance Ginnery na baadaye kukabidhiwa kwa Serikali jana  katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Sehemu ya majengo ya chuo cha  ufundi Kasoli  iliyojengwa  kwa msaada na Mwekezaji wa Kampuni ya Alliance Ginnery na baadaye kukabidhiwa kwa Serikali iliyopo  katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola akitoa maelezo  kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi  (mwenye skafu) juu ya shule ya ufundi Kasoli iliyojengwa na kampuni hiyo kwa msaada na kuikabidhi kwa serikali, baada ya kukifungua chuo hicho jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi akiyaangalia maji yanayotoka katika kisima kilichochimbwa kwenye shule ya ufundi ya Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali, baada ya kuifungua chuo hicho jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi, Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakifurahia na wananchi katika kijiji cha Kasoli baada ya ufunguzi wa  chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali jana kijijini hapo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto ) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi mara baada ya makabidhiano ya chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni ya Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali, katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola akiwaongoza Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi  (mwenye skafu) na viongozi wengine kukagua chuo cha ufundi ya Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali, baada ya kuifungua shule hiyo jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola akitoa maelezo  kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi  (mwenye skafu) juu ya vifaa mbalimbali vilivyopo katika  chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa na kampuni hiyo kwa msaada na kuikabidhi kwa serikali, baada ya kuifungua chuo hicho jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Kutoka kulia Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga wakuteta jambo baada ya makabidhiano ya chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni ya Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali, katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Kutoka kulia Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga wakiwa katika picha ya pamoja jana baada ya makabidhiano ya chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni ya Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali, katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Wasanii wa kundi la FUTUHI kutoka jijini Mwanza wakitoa burudani katika hafla ya makabidhiano ya shule ya ufundi ya Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni ya Alliance Ginnery na kukikabidhi kwa serikali, katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola akiwaongoza Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi  (mwenye skafu) na viongozi wengine kukagua chuo cha ufundi ya Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni Alliance Ginnery na kukikabidhi kwa serikali, baada ya kukifungua chuo hicho jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.


Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola akitoa maelezo  kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi  (mwenye skafu) juu ya chuo cha  ufundi Kasoli iliyojengwa na kampuni hiyo kwa msaada na kuikabidhi kwa serikali, baada ya kuifungua chuo hicho  jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto ) akiagana na na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi mara baada ya makabidhiano ya chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni ya Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali, katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola akitoa maelezo  kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi  (mwenye skafu) na viongozi wengine  juu ya maeneo mbalimbali ya  shule ya ufundi Kasoli iliyojengwa na kampuni hiyo kwa msaada na kukikabidhi kwa serikali, baada ya kukifungua chuo hicho jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi (mwenye skafu) akifurahia burudani ya nyimbo kutoka kwa msaani Elizabeth Maliganya (mwenye kipaza sauti) wakati wa ufunguzi wa chuo cha ufundi Kasoli 


Sehemu ya majengo ya chuo cha ufundi Kasoli  iliyojengwa  kwa msaada na Mwekezaji wa Kampuni ya Alliance Ginnery na baadaye kukabidhiwa kwa Serikali iliyopo  katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.



Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Kasoli wakifuatilia hafla ya makabidhiano ya shule ya ufundi Kasoli iliyojengwa na mwekezaji kampuni ya Alliance Ginnery  kwa msaada na kuikabidhi kwa serikali, baada ya kukifungua chuo hicho jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Viongozi mbalimbali wa mkoa wa Simiyu wakishangilia baada ya  Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi (wa tatu kulia) kufungua chuo cha ufundi Kasoli  iliyojengwa  kwa msaada na Mwekezaji wa Kampuni ya Alliance Ginnery na baadaye kukabidhiwa kwa Serikali jana  katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi (wa tatu kulia) akipanda mti wa kumbukumbu mara baada ya  kufungua shule ya ufundi Kasoli  iliyojengwa  kwa msaada na Mwekezaji wa Kampuni ya Alliance Ginnery na baadaye kukabidhiwa kwa Serikali jana  katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto ) katika picha ya pamoja  na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi mara baada ya makabidhiano ya chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni ya Alliance Ginnery na kukikabidhi kwa serikali, katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania-TIC, Dkt. Maduhu Kazi, Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakifurahia na wananchi katika kijiji cha Kasoli baada ya ufunguzi wa  chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni Alliance Ginnery na kukikabidhi kwa serikali jana kijijini hapo.
Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola(kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika hafla ya makabidhiano ya Chuo cha ufundi Kasoli iliyojengwa kwa msaada na mwekezaji kampuni ya Alliance Ginnery  na kukikabidhi kwa serikali, baada ya kukifungua shule hiyo jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiyaangalia maji yanayotoka katika kisima kilichochimbwa kwenye shule ya ufundi ya Kasoli iliyojengwa kwa msaada na kampuni Alliance Ginnery na kuikabidhi kwa serikali, baada ya kuifungua chuo hicho jana katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi mkoani Simiyu

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!