Monday, October 5, 2020

NMB WASAIDIENI WATUMISHI MIKOPO WAKATI WA DHARURA: RC MTAKA

 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa rai kwa Benki ya NMB kuja na utaratibu utakaowasaidia watumishi wa Umma ambao wamefikia kiwango cha mwisho cha kukopa kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT)  pale wanapobakia na moja ya tatu ya mishahara yao  ili waweze kupata msaada wakati wa dharura.

Mtaka ameyasema Mjini Bariadi  hayo Septemba 30, 2020 katika Warsha maalum ya Teachers’ Day iliyoandaliwa na Benki hiyo na kuwakutanisha walimu wakuu, wakuu wa shule, waratibu wa elimu, maafisa elimu na wadhibiti ubora wa mkoa wa Simiyu.

“Watumishi wengi wamekuwa wanaangukia mikononi mwa wakopeshaji binafsi wenye riba kubwa kutokana na kushindwa kukopesheka baada ya mishahara yao kutoruhusu makato ya mikopo inapofikia moja ya tatu ya mishahara yao kwa mujibu wa BOT, wanapopata dharura kwenye familia zao inawalazimu kukopa huko, benki kubwa kama NMB mje na ‘package’ ya kusaidia hili,” alisema Mtaka


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!