Thursday, December 9, 2021

Kuna Watu Wengi wa Maana Kaburini Kuliko Tuliobaki



“Kipo wapi kizazi kile ambacho kijana alihitaji kuwa na jembe, panga na shoka kuvamia msitu kuanza kuzalisha? 
Leo wazee wanataka kuwezeshwa kwasababu ni wazee, kina mama wanataka kuwezeshwa kwasababu ni wanawake, sasa na vijana nguvu kazi inazungumza kuwezeshwa vilevile kama wazee na kina mama. 

Ukiangalia majengo yaliyojengwa miaka 20 ya kwanza ya uhuru tukiwa na wahandisi wachache bado yapo, yanafanyiwa usafi tu lakini kuta bado imara.Lakini zama hizi za milenia ambazo tuna wahandisi wengi mpaka wanakosa kazi, kuna majengo hayafiki miaka 10 kabla ya kuanza kupasuka.Kifupi tuna watu wengi wa maana kaburini kuliko tuliobaki na maisha.Na hii ndio changamoto ya kizazi cha milenia leo.

Raia kwenye nchi masikini tunapumzika saa nyingi kuliko wa nchi tajiri.." RC - Kafulila akizungumza na wanachuo miaka 60 ya Uhuru.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!