Wednesday, December 22, 2021

MIKOA YOTE IGENI SIMIYU MIKATABA YA UWAJIBIKAJI




Naibu Waziri- TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange, leo amepongeza  Mkoa wa Simiyu kwa ubunifu wa kuanzisha mikataba ya uwajibikaji ambapo Mkuu wa Mkoa David Kafulila amesaini na wakuu wote wa wilaya na kisha Katibu Tawala Mkoa kusaini na wakurugenzi wote wa Halmashauri ambao nao wamesaini na wasimamizi wa sekta ya afya ngazi ya wilaya mpaka vijiji kwa lengo la kupima ufanisi wa kila Kiongozi na mtendaji kuanzia ngazi ya mkoa ( performance contract ) na kutaka mikoa mingine kuiga ili kuongeza tija katika usimamizi majukumu ya Serikali.  

Naibu waziri amesema hayo baada ya kupokea taarifa ya Mkoa wa Simiyu leo kuhusu masuala ya elimu na afya katika ziara yake ya siku moja mkoani simiyu, ambapo imelezwa kuwa ndani ya nusu mwaka  mifumo ya ya mapato GOTHOMICS imeboreshwa na kusababisha ongezeko la mapato kwa asilimia zaidi ya 300%, kutoka makusanyo ya takribani  milioni 200 mpaka zaidi ya milioni 600. 

Aidha mafanikio makubwa ktk usimamizi wa afya za lishe hata kufikia asilimia 92 mwezi Novemba , kiwango ambacho kinategemea kuipaisha simiyu katika tathimini ijayo itakayofanyika Januari 2022. " kwa ufanisi wa asilimia 92% sasa ni wazi tathimini ijayo Januari mkoa utakuwa 3 bora kutoka nafasi ya 23 kitaifa katika tathimini ya mwisho alisisitiza Kafulila. Mwisho.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!