Friday, February 23, 2018

MAKAMU WA RAIS AKITAKA CHUO KIKUU HURIA KUONGEZA UDAHILI KUSAIDIA TANZANIA KUFIKIA UCHUMI WA KATI


Makamu wa Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amekitaka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kuongeza  ubora na kupanua wigo wa udahili wa wanafunzi  kwenye programu za sasa ili kuendana na Sera Tanzania ya viwanda na kufikia Uchumi wa kati ifikapo 2025.
Ushauri huo ameutoa katika mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha TANZANIA  yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Makamu wa Rais amesema kuwa ili kuweza kufikia TANZANIA ya viwanda na kufikia uchumi wa kati 2025 lazima udahili wa wanafunzi katika vyuo vikuu ufikie kiwango cha angalau  asilimia 23.
“Naungana na Mhe.Rais kuwaomba muisaidie nchi yetu kuongeza kiwango cha udahili wa wananchi wake kwa haraka na kwa kasi itakayotuwezesha kufikia lengo la kuwa nchi ya Uchumi wa kati ifikapo 2025” alisema

“Kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia kiwango kidogo cha udahili katika elimu ya juu ni sifa ya msingi ya Uchumi wa chini na wa kimaskini, Uchumi wa kati na wa Viwanda hauwezi kufikiwa na kuwa endelevu pasipokuwa na kiwango cha udahili katika elimu ya juu  cha angalau asilimia 23” alisema Makamu wa Rais.

Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe.William Ole Nasha amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania katika maendeleo ya sekta ya elimu nchini kwa kuwa kimekuwa mtekelezaji mkuu wa malengo na mikakati ya Serikali kwa upande wa ujifunzaji kwa njia za masafa.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Profesa Elifas Bisanda amesema tangu Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kianzishwe idadi ya wahitimu imefikia 38, 993 baada ya mahafali ya 34 idadi hiyo imeongezeka kufikia 39,934, jambo ambalo limechangia  kukuza rasilimali watu hapa nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema kufanyika kwa  mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania mkoani humo kutakuwa chachu na kutaleta mwamko mpya wa elimu kwa wananchi Mkoani humo.

“Tuliona tuwaalike wanafunzi ili kujenga hamasa kwao, tulialika kamati zetu za shule, madiwani, walimu na wananchi wote wa Simiyu ili washuhudie tukio hili tukiamini kuwa kwa kuona tukio hili kila mmoja atatamani kuwa hivyo kesho,  kama siyo yeye basi awe  mwanaye au ndugu yake” alisema Mtaka.

Jumla ya wahitimu 941 kutoka Tanzania bara na Zanzibar na nchi jirani  walihudhurishwa mbele ya Mkuu wa Chuo Kikuu Huria  Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda na kutunukiwa  Astashaha, stashahada, shahada, shahada za uzamili , ambapo miongoni mwa hao 941 wahitimu saba walitunukiwa  shahada ya uzamivu(PhD).


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki matembezi ya mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania pamoja na Mkuu wa chuo hicho Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda (kulia) kuelekea  Uwanja wa Halmashauri ya  Mji wa Bariadi kwenye sherehe za mahafali hayo zilizofanyika Mjini Bariadi Mkoa  wa Simiyu.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Huria Tanzania Profesa Rwekaza Mukandala wakati wa mahafali ya 34 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu. .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Baadhi ya Wahitimu waliohitimu katika Mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu. .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Baadhi ya Wahitimu waliohitimu katika Mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu. .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wahitimu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na wananchi wa Mkoa wa Simiyu katika Mahafali ya 34 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Wahitimu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na wananchi wa Mkoa huo katika Mahafali ya 34 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani humo.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Prof.Elifas Bisanda akizungumza na Wahitimu wa Chuo hicho na wananchi wa Mkoa wa Simiyu katika Mahafali ya 34 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani humo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan(kulia),  Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Prof.Elifas Bisanda(kushoto) Mkuu wa chuo hicho Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda (katikati) wakishangilia jambo katika Mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan( wa nne kulia),  akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi wa Chuo Kikuu huria cha Tanzania na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya Mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu(kulia) Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!