Tuesday, February 26, 2019

NAIBU WAZIRI IKUPA ATOA WITO KWA WENYE ULEMAVU KUJIUNGA NA CHF ILIYOBORESHWA


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia  masuala ya watu wenye  ulemavu, Mhe.Stella Ikupa  ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya watu wenye  ulemavu, kuwahamasisha wanachama wao kujiunga na  mfuko  wa afya ya jamii (CHF )ulioboreshwa ili waweze kupata uhakika wa matibabu.

IKUPA ametoa wito huo  wilayani Itilima  katika ziara yake wakati akizungumza na viongozi wa Wilaya, Viongozi wa Vyama vya wenye ulemavu na  baadhi ya wenye ulemavu wenyewe wakati wa ziara yake wilayani humo Februari 25, 2019, ambayo ililenga kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ikiwa ni pamoja na mradi wa Kitalu nyumba na masuala mbalimbali yahusuyo wenye walemavu.

Amesema ni vema viongozi wa vyama na wenye ulemavu wakapena taarifa na kuhamasishani kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii(CHF) ulioboreshwa, ili wapewe vitambulisho waweze kutibiwa kirahisi.

“Mkijiunga na CHF iliyoboreshwa mkapata kadi mtakuwa na uwezo wa kutibiwa muda wowote, kwa hiyo peaneni hizo taarifa mjiunge watu mnaofahamiana muweze kupewa hivyo vitambulisho mpate kutibiwa kirahisi wakati tukiwa tunasubiri ile bima ya afya kwa kila Mtanzania” alisema Mhe. Ikupa.

Katika hatua nyingine amewaagiza maafisa Ustawi wa jamii na maendeleo ya jamii kutoa elimu vijijini kwa  watu wenye  ulemavu kuhusiana na  uundwaji wa vikundi na namna ya kutekeleza miradi mbalimbali.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima,Mhe.  Benson Kilangi  akizungumzia utekelezaji wa mradi wa kitalu nyumba amesema katika awamu ya kwanza jumla ya vijana 20 wamepata mafunzo ya utengenezaji wa vitalu nyumba na kufundishwa stadi mbalimbali za kuendesha kilimo biashara na kuongeza mnyororo wa thamani.

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Festo Kiswaga amesema  miradi ya vitalu katika Mkoa wa Simiyu itatekelezwa kwa viwango na kwa malengo yaliyokusudiwa, huku akibainisha kuwa vitasaidia kuongeza kipato kwa wananchi katika mkoa  na kuwa sehemu ya wananchi kujifunza kilimo bora.

Kwa upande wao viongozi pamoja na watu wenye ulemavu walioshiriki katika ziara hiyo wamemwomba Mhe. Naibu Waziri kushughulikia baadhi ya changamoto zinazowakabili katika maeneo yao.

“Ninaomba Serikali itusaidie tuweze kupata wakalimani wa lugha ya alama ili na sisi walemavu wa kusikia tuweze kupata ujumbe unaokuwa unawasilishwa na viongozi wetu kwenye mikutano na ziara kama hii ya leo hii itatusaidia sana” alisema Mhandi Ntobi Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu wasiosikia Mkoa wa Simiyu.

“NaombaWataalam waje watutembelee kwenye vijiji vyetu na kwenye vyama vyetu watusaidie kutupa elimu ya namna ya kuunda vikundi na namna ya kufanya shughuli zinazoweza kutuongezea kipato” Bw. Seni Jitabo mlemavu wa viungo Mkazi wa Zagayu wilayani Itilima.

Naibu Waziri Ikupa, anaendelea na ziara yake Mkoani Simiyu ambayo itahitimishwa 27 Februari 2019, akiwa wilayani Itilima Naibu waziri ametembelea kitalu nyumba kilichopo Lagangabilili na kituo cha maarifa ya jamii Kanadi, ambako amejionea shughuli mbalimbali za uzalishaji zinazofanywa na vijana.
MWISHO
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akizungumza jambo na Bw. Mhandi Ntobi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Watu wasiosikia Mkoa wa Simiyu, wakati akiwa katika ziara yake Wilayani Itilima Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu( hawapo pichani) mara baad ya kuwasilis Mjini Bariadi kwa ajili ya ziara yake mkoani humo, Februari 25, 2019.
 Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhe. Andrew Chenge akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa( wa pili kulia) alipotembea Ofisi za CCM Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa( katikati kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watumishi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Mkoani Simiyu(NSSF na PSSSF) mara baada ya kutembelea ofisi za mifuko hiyo wakati wa ziara yake mkoani Simiyu , Februari 25, 2019.
Bw. Seni Jitabo ambaye ni mlemavu wa Viungo akiwasilisha baadhi ya changamoto kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(hayupo pichani) wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019
Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye ualbino , akiwasilisha baadhi ya changamoto za kundi hilo kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(hayupo pichani) wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akipokea zawadi ya sabuni kutoka kwa Afisa Vijana wa Wilaya ya Itilima ambaye alimkabidhi kwa niaba ya viongozi wa Wilaya hiyo wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019
Moja ya Kitalu nyumba(green house) ikatika kata ya Lagangabilili wilayani Itilima, kilichotembelewa na  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa wakati wa ziara yake.
Baadhi ya viongozi , watendaji na watu wenye ulemavu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi akitoa taarifa ya Wilaya Februari 25, 2019  kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa,ambaye yupo ziarani mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeketi) akipewa maelezo ya namna sabuni za WIZA zinavyotengenezwa, wakati alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Kata ya Kanadi wakati waziara yake wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akielekea katika Kiwanda cha kutengeneza sabani za WIZA zinazotengenezwa katika Kata ya Kanadi wakati ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019. 


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Wilaya ya Itilima, mara baada ya kukamilisha ziara yake wilayani humo Februari 25, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeketi katikati )akiwa katika picha ya pamoja na wana kikundi wanaojihusisha na utengenezaji wa sabuni za WIZA zinazotengenezwa katika Kata ya Kanadi wakati  wa ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019.
 Sehemu ya Jengo la Kiwanda cha Sabuni Itilima kilichopo Kanadi
Viongozi wa Wilaya ya Itilima wakimkaribisha Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa kwa ajili ya kuanza ziara wilayani humo, Februari 25, 2019.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Kanadi  wilayani Itilima, wakati  wa ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019



Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Kanadi  wilayani Itilima, wakati  wa ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!