Wednesday, February 20, 2019

OMBI LA WANANCHI SIMIYU LA ENEO LA MALISHO LAPOKELEWA NA SERIKALI, LAAHIDIWA KUFIKISHWA KWA RAIS MAGUFULI

Mwenyekiti wa Timu  maalum ya mawaziri wanane ya kupitia maeneo yenye migogoro  kati ya  wananchi na maeneo ya Hifadhi, Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo na Makazi Mhe. Wiliam Lukuvi amepokea ombi la wananchi  wa wilaya tatu za mkoa wa Simiyu wanaoishi katika vijiji vinavyopakana na Pori la Akiba la Maswa  la kupewa eneo lenye urefu wa kilometa kumi, kwa ajili ya malisho na kuahidi kulifikisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua zaidi.


Mhe. Lukuvi ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Vijiji vinavyopakana na pori la akiba la Maswa  katika mkutano wa hadhara  uliofanyika Mji mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu.
Awali akijibu baadhi ya kero zilizowasilishwa na Mwananchi wa Wilaya ya Meatu, Bw. Deusdedith Martin  Waziri Lukuvi amesema timu hiyo imezisikia kero hizo na akaahidi kuwasilisha taarifa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na kubainisha kuwa taarifa rasmi ya majibu ya kero zao itatolewa.

Aidha, Waziri  Lukuvi amewahakikishia wananchi kuwa zoezi la kupima eneo la mita 500 kutoka kwenye mpaka wa Pori la Akiba la Maswa kuelekea kwenye vijiji vinavyopakana na Pori hilo (Buffer zone)  katika Wilaya za Meatu, Itilima na Maswa limesimamishwa mpaka litakapotolewa maelekezo.

“Hapa kulikuwa na zoezi la kupima mita 500 kutoka kwenye mpaka wa Pori la Akiba la Maswa kuingia kwa wananchi, maana yake ni kwamba kuna wananchi wengi na vijiji vingi vingeathirika ili vipishe ‘buffer zone’, ingawa ni kwa mujibu wa sheria lakini ‘buffer zone’ ile ingekula maeneo ya vijiji kwa hiyo zoezi hilo limesimamishwa”

“Zoezi hili limesimamishwa kwa mujibu wa maelekezo ya Mhe Rais baada ya kuona watu wengi maskini ambao walipaswa kupisha maeneo ya hifadhi;...... vile vile kuanzia sasa zoezi lolote la kutambua mipaka litakalofanywa na watu wa Maliasili ni lazima liwe shirikishi” alisema Waziri Lukuvi.

Awali akiwasilisha taarifa kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Meatu, Bw. Deusdedit Martin aliomba Timu ya Mawaziri wanane kuwasaidia katika kutatua changamoto ya ubadilishaji wa mpaka kati ya Pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyopakana, Uvamizi wa tembo katika mashamba na makazi ya watu na kukatazwa kwa wananchi kulima katika eneo la mita 60 kutoka kwenye kingo za mito.

Kwa upande wake Waziri wa Maji, Mhe. Prof.  Makame Mbarawa amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Simiyu upatikanaji wa uhakika wa  maji  kupitia mradi mkubwa wa Ziwa Victoria, ambapo amesema kwa sasa mradi upo  katika hatua ya kumtafuta mkandarasi.

Naye  Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe.Omari Mgumba akieleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha inatoa viatiifu kwa wakulima ambapo amesema hadi sasa zaidi ya chupa milioni saba zimeshasambazwa kwa wakulima katika mikoa inayolima pamba hapa nchini.

Timu ya Mawaziri wanane inayoongozwa na Waziri Lukuvi pia inajumuisha mawaziri kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Maliasili na Utalii, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Maji na Manaibu Waziri kutoka Wizara ya Kilimo na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira.
MWISHO
Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane wa kisekta, Mhe. William Lukuvi akizungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri nane wa kisekta anayoiongoza kutembelea mpaka wa Pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.
Wananchi wa Wilaya ya Meatu wakiwapungia mikono Timu ya Mawaziri nane wanaopitia maeneo  yenye migogoro katika wananchi na hifadhi, wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Meatu Mji mdogo  Mwandoya mara baada ya timu hiyo kutembelea na kujionea mpaka wa pori hilo, Februari 19, 2019

Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane, Mhe. William Lukuvi akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mjini Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, mara baada ya Timu ya mawaziri wanane wanaopitia maeneo yenye migogoro kati ya wananchi na  hifadhi,  mara baada ya timu hiyo kutembelea na kujionea mpaka wa pori la Akiba la Maswa, Februari 19, 2019
Bw. Deusdedit Martin akiwasilisha taarifa ya mapendekezo ya wananchi kwa Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane, Mhe. William Lukuvi wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, mara baada ya timu hiyo kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019
Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane, Mhe. William Lukuvi(wa pili kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo (katikati) na Mjumbe wa NEC, Mhe. Gungu Silanga(wa pili kulia), baada ya mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, mara baada ya timu hiyo kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.(kushoto) Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba na (kulia) Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi.
Meneja wa Pori la Akiba la Maswa, Bw.Lusato Masinde akijibu baadhi ya hoja kutoka kwa Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane, Mhe. William Lukuvi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu hiyo kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019
Baadhi ya wajumbe wa timu ya mawaziri wanane wa kisekta, Kutoka kulia Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina, Waziri wa Nchi, OR-TAMISEMI, Sulemani Jafo, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira,Mussa Sima na Waziri wa Maji, Pro. Makame Mbarawa wakiwa katika mkutano wa Hadhara Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu hiyo kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi(kushoto) akifurahia jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika mkutano wa Hadhara Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri nane wa kisekta ikiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.
Wasanii  kutoka wilayani Meatu wakitoa burudani katika mkutano wa Hadhara Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri wanane wa kisekta ikiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.
Bw. Peter Ndekeja mwananchi kutoka wilayani Meatu akitoa malalamiko yake kwa Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane wa kisekta, Mhe. William Lukuvi wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, mara baada ya timu hiyo kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri wanane wa kisekta ikiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.


Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane, Mhe. William Lukuvi akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mjini Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, mara baada ya Timu ya mawaziri wanane wanaopitia maeneo yenye migogoro wananchi na hifadhi, mara baada ya timu hiyo kutembelea na kujionea mpaka wa pori la akiba la Maswa, Februari 19, 2019

Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakifuatilia Mkutano wa hadhara uliofanyika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri wanane wa kisekta ikiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Meatu wakifuatilia Mkutano wa hadhara uliofanyika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri nane wa kisekta ikiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.
Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Mussa Sima na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani, wakifurahia jambo katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri wanane wa kisekta ikiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.



Mwenyekiti wa Timu ya Mawaziri wanane wa kisekta, Mhe. William Lukuvi akiteta jambo na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi(kushoto) katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Mji Mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu, baada ya timu ya mawaziri wanane wa kisekta ikiongozwa na Mhe.Lukuvi kutembelea mpaka wa pori la Akiba la Maswa na Vijiji vinavyolizunguka, Februari 19, 2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!