Thursday, June 4, 2020

NANENANE KITAIFA MWAKA 2020 ITAKUWEPO NA ITAFANYIKA SIMIYU: RC MTAKA


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameujulisha Umma wa Watanzania kuwa Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nanenane Kitaifa kwa mwaka 2020 yatakuwepo na yatafanyika katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi na viongozi wakuu wa Kitaifa wanatarajiwa kufungua na kufunga maonesho hayo ambayo yanafanyika kwa mara ya tatu mfululizo.

Mtaka ameyasema hayo leo Juni 03, 2020 katika kikao cha pamoja kati ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega ambaye yuko mkoani Simiyu kwa ziara ya siku mbili.

"Kumekuwa na maswali kwa baadhi ya watu kuhusu Nanenane kuwa itakuwepo au haitakuwepo, nitumie nafasi hii kuwaambia Watanzania kuwa tumepokea taarifa rasmi kutoka Wizara ya Kilimo kuwa sherehe za Nanenane Kitaifa mwaka 2020 zipo na zitafanyika mkoani Simiyu na viongozi wakuu wa Kitaifa watashiriki katika ufunguzi na ufungaji; mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayoandaa sherehe hizi imeanza maandalizi, taasisi za Umma na binafsi pia zimethibitisha kushiriki na nyingine zimeanza maandalizi,” alisema Mtaka.



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiteta jambo na  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati alipowasili Mjini Bariadi kwa ajili ya kuanza ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu, Juni 03, 2020.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!