Monday, December 7, 2020

HALMASHAURI ZATAKIWA KUKAMILISHA UTOAJI WA VITAMBULISHO KWA WAZEE KUFIKIA JUNI 2021

Rai imetolewa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani Simiyu kuhakikisha kuwa wanakamilisha zoezi la utoaji wa vitambulisho vya matibabu kwa wazee kufikia mwezi Juni 2021, ili wazee waweze kupata huduma za matibabu katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya kama Serikali ilivyodhamiria.

 

Rai hiyo imetolewa Novemba 4, 2020 Mjini Bariadi na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika uzinduzi wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Simiyu..

“Mkoa kupitia Halmashauri umefanya utambuzi wa jumla ya wazee 68,175 kwa lengo la kuhakikisha kuwa wanapatiwa huduma muhimu, hadi sasa  jumla ya mabaraza 770  ya wazee yameundwa katika ngazi zote ; kuhusu upatikanaji wa vitambulisho vya matibabu bure, jumla ya wazee 18, 911 wamepatiwa vitambulisho hivyo ndani ya mkoa sawa na asilimia 28,’ alisema Kiswaga.

Mabaraza si ya kiitikadi hivyo kila mtu mwenye umri wa miaka sitini na kuendelea ana haki ya kujiunga na kuwa mjumbe wa Baraza la Wazee mahali alipo, huku akiahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Wazee na kukukutana na wazee mara kwa mara ili kuhakikisha kuwa inawasilikiza na mahitaji yao muhimu yanapatikana.

Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa, Bibi.Mwanahamisi Kawega amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itahakikisha inasimamia utekelezaji wa suala la ugawaji wa vitambulisho vya matibabu kwa wazee katika Halmashauri zote ili wazee wote waweze kuvipata kwa wakati.

Aidha Kawega ameongeza kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu itawaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri kuwaalika viongozi wa mabaraza ya wazee kualikwa katika mabaraza ya madiwani ili waweze kuwasilisha kero zao na kupatiwa ufumbuzi.

Naye Meneja Mradi kutoka Shirika la NABROHO SOCIETY FOR THE AGED linalojihusisha na utetezi wa haki za wazee  , Bw. Kubini Nkondo ameipongeza Serikali kwa namna inavyotoa kipaumbele kwa wazee na namna ilivyokomesha mauaji ya wazee.

 

"Wazee wamepitia changamoto nyingi ukizungumzia  hata suala la mauaji ya wazee, takwimu awali zilikuwa juu sana lakini katika utawala huu tunazungumzia mauaji hayo kupungua mpaka kufikia 'digit' (tarakimu) moja, Mkoa wa Simiyu ambao ulikuwa ukitajwa katika Mkoa 10 inayoongoza kwa mauaji ya wazee sasa hivi haitajwi hata tena katika mikoa inayoongoza kwa mauaji hayo," alisema Nkondo.

 

Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Mkoa wa Simiyu, Bw. Lameck Sendo amesema Baraza hilo litaendelea kushirikiana na Serikali katika kushughulikia haki mbalimbali za wazee huku akiomba Serikali kuitungia sheria  Sera ya wazee ya mwaka 2003 ili iweze kutumika katika kuwaongoza pamoja na miongozo iliyopo.

 

Afisa Ustawi wa Jamii Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bw. Daniel Mapunda amesema Mkoa wa Simiyu una takribani wazee 68,175, hivyo kwa mujibu wa Sera ya Wazee ya mwaka 2003 Baraza la Wazee la Mkoa litakuwa ni chombo maalum cha kuwasemea wazee na kushiriki katika maeneo  mbalimbali ya kimaamuzi.

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (wa pili kushoto) akimkabidhi nyaraka mbalimbali Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Simiyu, Bw. Lameck Sendo mara baada ya kuzindua baraza hilo Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Baadhi ya viongozi wa Mabaraza ya Ushauri ya Wilaya za Mkoa wa Simiyu wakifurahia jambo katika kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa na kuzindua baraza hilo.

Baadhi ya viongozi wa Mabaraza ya Ushauri ya Wilaya za Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa na kuzindua baraza hilo.

Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Simiyu, Bw. Lameck Sendo akieleza namna Baraza hilo litakavyofanya kazi mara baada ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kuzindua baraza hilo  Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Daniel Mapunda akitoa ufafanuzi juu ya taratibu zinazopaswa kufuatwa katika Uchaguzi wa Viongozi wa Baraza la Ushauri la Mkoa, katika kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza hilo na kuzindua.

Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Mwanahamisi Kawega akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa na kuzindua baraza hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongzi wa Mkoa wa Simiyu, viongozi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa(waliosimama) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bw. Lameck Sendo(wa pili kulia walioketi), baada ya kuzindua baraza hilo Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Meneja Mradi wa Taasisi isiyo ya Kiserikali inayojishughulisha na utetezi wa Haki za Wazee mkoani Simiyu, Bw. Kubini Nkondo Kubin akizungumza na viongozi wa mabaraza  ya Ushauri ya Wilaya  katika kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa na kuzindua baraza hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu, viongozi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa, Viongozi wa mabaraza ya wilaya (waliosimama) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Mkoa, Bw. Lameck Sendo(wa pili kulia walioketi), baada ya kuzindua baraza hilo Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu, viongozi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa, Viongozi wa mabaraza ya wilaya (waliosimama) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Mkoa, Bw. Lameck Sendo(wa pili kulia walioketi), baada ya kuzindua baraza hilo Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Simiyu, Bw. Lameck Sendo akitoa maelezo ya agenda kumi zinazowahusu wazee katika kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza hilo na kuzindua kazi iliyofanywa na  Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kuzindua baraza hilo, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Maafisa Ustawi wa Jamii na kiongozi wa dini (waliosimama) na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa, Bw. Lameck Sendo(wa pili kulia walioketi), baada ya kuzindua baraza hilo Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa  wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kwa Baadhi ya viongozi wa Mabaraza ya Ushauri ya Wilaya za Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza la Ushauri la Mkoa na kuzinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Baadhi ya viongozi wa Mabaraza ya Ushauri ya Wilaya za Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza la Usahauri la Wazee la Mkoa na kuzindua baraza hilo.

Mwenyekiti wa Baraza la ushauri la Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, akipokea nyaraka za utendaji kazi wa baraza hilo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga baada ya kuzinduliwa kwa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa, Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi.


Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Maafisa Usatawi wa Jamii na kiongozi wa dini (waliosimama) na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa, Bw. Lameck Sendo(wa pili kulia walioketi), baada ya kuzindua baraza hilo Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Baadhi ya Viongozi wa Baraza la Ushauri la Mkoa wa Simiyu

Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Mwanahamisi Kawega, Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Daniel Mapunda na Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa  wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba wakiteta jambo kikao kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi, kwa lengo la kufanya uchaguzi wa Baraza la Ushauri la Wazee la Mkoa na kuzindua baraza hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na baadhi ya viongozi wa mabaraza ya ushauri ya wilaya za mkoa wa Simiyu kabla ya kuzindua Baraza la ushauri la Mkoa kilichofanyika Desemba 04, 2020 Mjini Bariadi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!