Wednesday, December 16, 2020

TANROADS SIMIYU KUTUMIA BILIONI 11.4 UJENZI WA BARABARA NA MADARAJA

 

Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Simiyu umepanga kutumia kiasi cha shilingi bilioni 11.4 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na madaraja.

 

Hayo yamebainishwa na Meneja wa TANROADS mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Albert Kent wakati akiwasilisha taarifa katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Simiyu, kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 Mjini Bariadi.

 

“Bajeti iliyopangwa kwa mkoa wa Simiyu ni shilingi bilioni 11.44 na kuna ongezeko kidogo mwaka jana tulikuwa na bilioni 10.9; tumepanga kufanya kazi kwenye barabara zenye urefu wa kilomita 923.6 pamoja na madaraja mawili,” alisema Mhandisi Kent.

 

Kwa upande wake Mratibu wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), Dkt. Eng. Philemon Msomba amesema katika mwaka wa fedha 2019/2020 TARURA imetengeza kilometa 690.31 za barabara huku bajeti ya mkoa ikiwa bilioni 5. 056 na katika mwaka wa fedha 2020/2021 TARURA imeingia mikataba 18 yenye jumla ya shilingi 3,048,528,759/=

 

Dkt. Msomba ameongeza  kuwa jumla ya kiasi cha shilingi milioni 750 kimeidhinishwa kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ya Mwadobana na Ngashanda kwa mwaka wa fedha 2020/2021

 

Mbunge wa Jimbo la Meatu, Mhe. Leah Komanya akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa amesema “Ninaiomba Serikali katika bajeti zijazo ipandishe hadhi kipande cha barabara ya Mwabuzo-Igunga, ili tuweze kuleta maana ya kuunganisha barabara hii katika kuinua uchumi wa wananchi wa wilaya ya Meatu.”

 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesisitiza usimamizi wa miradi ya barabara huku akiitaka TANROADS kuona uwezekano wa kutenga bajeti kwa ajili ya  ujenzi wa mzani wa kisasa katika eneo la Malampaka kwa kuwa ni eneo litakalopitiwa na reli ya kisasa (SGR).

 

TANROADS Mkoa wa Simiyu ina jukumu la kutunza na kuendeleza barabara zenye urefu wa kilometa 923.65 barabara kuu ikiwa ni kilometa 334.33, barabara za mkoa kilometa 521.62 na barabara moja ya wilaya yenye urefu wa kilometa 67.7; ambapo TARURA inahudumia mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 4,038.16.

MWISHO

Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Albert Kent akiwasilisha taarifa ya wakala huo katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa, kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 mjini Bariadi.

Mratibu wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini  (TARURA) Mkoa wa Simiyu, Dkt.Eng. Philemon Msomba akiwasilisha taarifa ya wakala huo katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa, kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga wakifuatilia hoja zilizokuwa zikiwasilishwa na wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 Mjini Bariadi.

Mbunge wa Maswa Mashariki, Mhe. Stanslaus Nyongo akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa, kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Simiyu, wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Simiyu, wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Simiyu, wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 mjini Bariadi.

Baadhi ya wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Simiyu, wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika jana Desemba 15, 2020 mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!