Thursday, December 10, 2020

KILA MDAU AWE SEHEMU KUUFIKISHA MKOA NAMBA MOJA MITIHANI YOTE KITAIFA: RAS SIMIYU

Katibu Tawala wa Mkoawa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga ametoa wito kwa viongozi, walimu, wazazi na wadau wote wa elimu mkoani hapa kushiriki kikamilifu katika kutekeleza na kuwezesha azma ya mkoa ya kuwa nafasi ya kwanza katika mitihani yote ya  Taifa.

 

Mmbaga ameyasema hayo Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi wakati akifungua kikao cha viongozi, watendaji na wadau wa elimu mkoa cha kutangaza Mkakati wa Mkoa wa kuboresha taaluma kwa mwaka 2021 ambapo alibainisha kuwa endapo kila mdau atatimiza wajibu wake Simiyu itakuwa mkoa bora katika elimu.

“Mkoa wetu kushika nafasi ya kwanza inawezekana kabisa, kama tuliweza kutoka nafasi za mwishoni kabisha tukaingia, kumi bora, sasa hivi tuka katika tatu bora, naamini kwa uweza wa Mwenyezi Mungu tunaweza  kushika nafasi ya kwanza katika mitihani yote ya Taifa,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga amewataka viongozi wa idara ya elimu kuepuka kutumia kauli chafu kwa walimu kwa kuwa zinawakatisha tamaa na kupunguza tija na ari katika utendaji kazi wao badal yake watumie mbinu sahihi za kiuongozi kutatua changamoto wanazoziona kwa walimu.

 Naye Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema ushirikiano, mawasiliano na mahusiano mazuri baina ya walimu, viongozi na wadau wote wa elimu yanasaidia muda mwingi kutumika kufundisha na kusimamiana badala ya kutumika kuzozana, kugoma na kusuluhishana.

Baadhi ya walimu na Maafisa Elimu wa Kata na Halmashauti wamesema wameupokea mkakati huo na kuahidi kutimiza wajjibu wao ili kuweza kufikia malengo ya mkoa na kuboresha taaluma na elimu mkoani Simiyu huku wakitoa maoni mbalimbali namna ya kuboresha zaidi utekeelzaji wa mkakati huo.

“Nashauri mkoa uanzishe mitihani ya pamoja ya madarasa tarajiwa yaani darasa la tatu, darasa la sita, kidato cha kwanza na kidato cha tatu, mitihani hii itusaidia kujua shule zipi zina changamoto gani na itasaidia kuweka mikakati ya kuziwezesha kufanya vizuri kwa kuwa walimu na viongozi wengine watakuwa na mwaka mzima wa kuyaandaa madarasa hayo kabla ya mtihani wa Taifa,” alisema Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Lagangabilili Itilima, Mwede Hongoa.

“Tunaomba Serikali iboreshe makazi ya walimu, walimu wengi hawana nyumba za kuishi maeneo ya shule wengi wanatoka mbali na Shule hivyo wakati tunapohitaji kuwasaidia wanafunzi hasa nyakati za usiku inakuwa vigumu kwao kushiriki kikamilifu,” alisema Mwalimu Flora Shimbi Mkuu wa Shule Itilima Sekondari.

“Serikali ya Mkoa imetoa motisha kwa walimu hasa wanaofanya vizuri na walimu wa mkoa wa Simiyu wamehamasika sana na wanajituma katika kazi yao, tunaomba serikali iendelee kuboresha miundombinu ikiwemo vyumba vya madarasa, madawati na viti ili mazingira yao ya kufundishia yawe bora zaidi,” alisema Mwalimu Oscar Nsolo Mkuu wa Shule Sapiwi Sekondari.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo ameshauri mkoa wa Simiyu kuwa na mfuko wa elimu wa mkoa, ili mfuko huo uweze kusaidia katika ujenzi wa miundombinu ya elimu huku akitoa wito kwa wazazi na wadau wote wa elimu kuona umuhimu wa kuuchangia mfuko huo.

Mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021 umejumuisha mambo muhimu ikiwa ni pamoja na Uwezo wa kujituma kwa viongozi wa elimu, uungwaji mkono na viongozi wa juu,uwajibikaji wa maafisa elimukata na mfumo wa utawala, huduma bora na mawasiliano kwa walimu/wadau wa elimu, utoaji wa motisha na zawadi, ufatiliaji kabambe wa ufundishaji na ujifunzaji, mafunzo kazini,upimaji, miundombinu na samani, kambi za kitaaluma, matumizi ya mitandao ya TEHAMA.

MWISHO

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi kikiwashirikisha walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani hapa.

Baadhi ya Walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani Simiyu, katika kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

 

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akizungumza na walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani Simiyu, katika kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

Mmoja wa walimu akichangia hoja katika kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

Mmoja wa walimu akichangia hoja katika kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya Walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi

Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania Mkoa wa Simiyu, akichangia hoja katika kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya Walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya Walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

Kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka , Katibu Tawala wa Mkoa, Bibi. Miriam Mmbaga na Afisa Elimu wa Mkoa, Mwl. Ernest Hinju wakiteta jambo katika kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya Walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi

Baadhi ya Walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi

Baadhi ya Walimu, viongozi wa Chama na Serikali, viongozi wa elimu na wadau elimu mkoani mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kutangaza mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021, kilichofanyika Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!