Saturday, March 6, 2021

NAIBU WAZIRI SILINDE ATOA MIEZI MIWILI BARIADI, ITILIMA KUKAMILISHA MABWENI

 

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI ametoa miezi miwili kuanzia sasa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Itilima kukamilisha ujenzi wa mabweni katika  shule ya sekondari Bariadi, Nyasosi na Itilima ili wanafunzi waliokusudiwa kukaa katika mabweni hapo wapate huduma tarajiwa kwa wakati.

 

Silinde ametoa agizo hilo wakati alipotembelea shule hizo wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 Mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua ujenzi wa majengo ya miundombinu ya elimu ikiwemo mabweni, mabwalo na vyumba vya madarasa.

 

Amesema Serikali haitatoa fedha nyingine kukamilisha mabweni, mabwalo na madarasa ambayo bado hayajakamilika na haitakubali yabaki magofu  hivyo ni jukumu la Halmashauri husika kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo hayo ili wanafunzi waliokusudiwa kutumia wapate haki yao.

 

“Nimeridhishwa na kiwango cha ujenzi wa madarasa na thamani ya fedha inaonekana ninawapongeza sana, kuhusu mabweni mhakikishe yanakamilika na ninaahidi kurudi tena hapa mwezi Mei kuja kukagua kuona namna mlivyotekeleza, yasipokamilika ninawaambia wazi nitawavua madaraka wakuu wa shule na maafisa Elimu sekondari,” alisema Silinde.

 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Bi.Elizabeth Gumbo ameahidi kukamilisha ujenzi wa bweni shule ya sekondari Itilima ifikapo Aprili 30, 2021 huku Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bw. James John akiahidi kukamilisha bweni la Shule ya sekondari Nyasosi tarehe hiyo hiyo na Mkurugenzi wa Mji wa Bariadi,Melkizedeck Humbe ameahidi kukamilisha ujenzi Mei 15, 2021.

 

Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi amesema shule ya Sekondari Itilima ilipokea shilingi milioni 80 kwa ajili ya ujnezi wa bweni ambapo amebainsha kuwa baadhi ya sababu zilizopelekea mradi huo kutokamilika kwa fedha hiyo ni pamoja na aina ya udongo uliopo katika eneo la Ujenzi kuhitaji msingi mrefu na imara uliotumia fedha nyingi tofauti na makadirio pamoja na kupanda kwa bei za vifaa vya ujenzi.

 

Pamoja na changamoto hizo Kilangi amesema Serikali wilayani humo itahakikisha Bweni la Shule ya Sekondari Itilima linakamilika kwa wakati ili kuwawezesha wanafunzi kupata huduma iliyokusudiwa kwao.

 

Naye Mkuu wa Wilaya ya  Bariadi Mhe. Festo Kiswaga amewaagiza wataalam wa Halmashauri zote mbili za Wilaya ya Bariadi kuhakikisha wanakamilisha majengo yote yaliyoletewa fedha na serikali huku akimhakikishia Naibu Waziri kuwa mabweni ya Bariadi sekondari na Nyasosi sekondari yatakamilika kwa wakati.

 

Katika hatua nyingine Kiswaga amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya hiyo kumpelekea taarufa ya fedha zote za miradi zinazoingia ili kamati ya ulinzi na usalama iweze kujua na kuweka utaratibu wa kuzisimamia na kuhakikisha zinatekeleza miradi kulingana na maelekezo ya Serikali.

MWISHO 

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde akizungumza na viongozi na baadhi ya watendaji wa Wilaya ya Bariadi wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.


Mkuu wa Shule ya Sekondari Kanadi (mwenye karatasi mkononi) iliyopo wilaya ya Itilima akimuongoza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye skafu) kuelekea katika vyumba vya madarasa vilivyojengwa kupitia fedha za mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.


Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye skafu) wakati alipotembelea Shule ya Sekondari Itilima ili kujionea maendeleo ya Ujnezi wa bweni shuleni hapo wakati wa ziara ya naibu Waziri huyo Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu. 

Mkuu wa Shule ya Sekondari Itilima wilayani Itilima, Mwl. Flora Shimbi (mbele kulia)  akimuongoza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye skafu) naviongozi wengine kuelekea katika bweni lililojengwa kupitia fedha za mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu. 

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde(kulia) akielekea kukagua jengo la bweni katika Shule ya sekondari Bariadi wilayani Bariadi wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu. 

Baadhi ya madarasa yaliyojengwa kupitia fedha za mradi wa lipa kulingana na matokeo katika shule ya sekondari Kanadi wilayani Itilima mkoani Simiyu
Baadhi ya samani kama zinavyoonekana katika vyumba vya madarasa vilivyojengwa katika shule ya sekondari Kanadi wilayani Itilima
 
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Kanadi wilayani Itilima wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (hayupo pichani) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.
Baadhi ya viongozi na watendaji wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (hayupo pichani) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu
Baadhi ya wanafunzi wakiwa katika baadhi ya madarasa (pichani) yaliyojengwa katika Shule ya sekondari Itilima wilayani Itilima.

Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akiwasilisha taarifa ya Mkoa kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David (kulia) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde akizungumza na viongozi na baadhi ya watendaji wa Wilaya ya Itilima wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.

Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya itilima na wanafunzi wa shule ya sekondari Kanadi wilayani Itilima wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (hayupo pichani) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde akizungumza na viongozi na baadhi ya watendaji wa Wilaya ya Bariadi wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu. 
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (wa pili kushoto) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.


Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (hayupo pichani) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.
Baadhi ya watumishi na viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi wakielekea katika jengo la Bweni linaloendelea kujengwa katika shule ya sekondari ya Bariadi Mjini Bariadi kupitia fedha za mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R), kwa ajili ya kumsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (hayupo pichani) wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye suti nyeusi) akikagua ujenzi wa Bweni linaloendelea kujengwa katika shule ya sekondari Nyasosi wilayani Bariadi kupitia fedha za mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R), wakati wa ziara yake Machi 05, 2021 mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya elimu. 

Sehemu ya jengo la Bweni linaloendelea kujengwa katika shule ya sekondari Nyasosi wilayani Bariadi kupitia fedha za mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R)

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!