Friday, March 5, 2021

UKAGUZI WA CHUMVI ISIYO NA MADINI JOTO UFANYIKE KUNUSURU AFYA ZA WATU: RAS SIMIYU

 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amewataka wataalam kufanya ukaguzi wa matumizi ya chumvi isiyo na madini joto katika maeneo tofauti mkoani Simiyu ili kuweza kupata uhalisia wa hali ya matumizi ya chumvi hiyo na  matokeo yake yaweze kuwasaidia wataalam kutoa elimu juu ya madhara ya matumizi ya chumvi kwa afya ya watumiaji.

 

Mmbaga ametoa agizo hilo jana Machi 03, 2021 wakati akizungumza na baadhi ya viongozi na wataalam katika kikao cha Kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili utekelezaji wa afua mbalimbali za lishe.

 

“Wataalam wetu wa afya tengenezeni vigezo vya kisayansi vya ukaguzi wa chumvi isiyo na madini joto utakaotupa picha halisi ya mkoa wetu ili taarifa yetu ya ukaguzi ikitoka sisi wenyewe au mtu yeyote tukimweleza aweze kuelewa; siyo tufanye ukaguzi ili ionekane tumefanya kwa kuwa sisi kama viongozi na watalaam tuna hatari kwenye jamii yetu kwamba kuna watu watapoteza maisha na pia tutakuwa na watu ambao hawana uelewa kwa sababu tu ya kutumia chumvi isiyokuwa na madini joto,” alisema

 

Aidha, Mmbaga ametoa wito kwa wataalam kuendelea kutoa elimu kwa wafanyabiashara wa chumvi isiyo na madini joto na kuwashauri badala ya kuimwaga au kuharibu chumvi inayokamatwa baada ya kubainika kuwa inauzwa au kupelekwa kwa watumiaji pasipo kukidhi vigezo vya kiafya.

 

Afisa Lishe wa mkoa wa Simiyu, Dkt. Chacha Magige amesema madhara ya chumvi isiyo na madini joto ni pamoja na wajawazito kujifungua watoto ambao hawajatimiza miezi tisa, watoto kuwa na uwezo mdogo wa kiakili(kufikiri) kwa kuwa chumvi yenye madini joto husaidia katika ukuaji wa ubongo wa watoto wakiwa tumboni, kuharibika kwa mimba na kusababisha goita.

 

Katibu tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akifungua kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati ya lishe ya mkoa wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.
Afisa Lishe wa mkoa wa Simiyu, Dkt. Chacha Magige akiwasilisha taarifa ya mkoa ya hali ya lishe ilivyo kwa wajumbe wa kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021.


Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Aswege Kaminyoge akichangia hoja katika kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati ya lishe ya mkoa wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati ya lishe ya mkoa wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Itilima, Bw. Filbert Kanyilizu akichangia hoja katika kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Boniface Richard akifafanua jambo katika kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Mratibu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa (iCHF) mkoa wa Simiyu, Bi. Salama Rajabu akiwasilisha mada katika kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (wa pili kulia) akisisitiza jambo katika  kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu akichangia hoja katika kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Mratibu wa Mpango wa Kudhibiti Ugonjwa wa Homa kali ya Mapafu (COVID 19), Dkt. Khamis Kulemba akiwasilisha mada katika kikao cha kamati ya lishe ya mkoa kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati ya lishe ya mkoa wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati ya lishe ya mkoa wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika Machi 03, 2021 Mjini Bariadi

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!