Tuesday, March 9, 2021

ZAIDI YA MILIONI 138 ZATOLEWA MIKOPO KWA WANAWAKE SIMIYU

                

Katika mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri sita za Mkoa wa Simiyu zimetoa shilingi 138,030,500/= kwa vikundi 122 vya wanawake kama mikopo kutoka katika asilimia nne ya mapato ya ndani ya halmashauri, kwa ajili ya kuwapatia mitaji ya kuanzisha na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi. 

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa naiba yake na Mwanasheria wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bi, Manahamisi Kawega wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Machi 08, 2021 ambayo kimkoa yamefanyika Wilayani Maswa.

“Halmashauri ya Mji wa Bariadi, imetoa shilingi 10,000,000/= kwa vikundi 25, Halmashauri wilaya ya Bariadi shilingi 48,000,000/= vikundi 37, Busega shilingi 16,000,000/=kwa vikundi 16, Itilima shilingi 12,000,000/= vikundi 12, Maswa shilingi 39,200,000/= vikundi 18 na Meatu shilingi 12,830,500 kwa vikundi 14,” alisema.

Aidha, Mmbaga amewaagiza Wakurugenzi wa Mamalaka za Serikali za Mitaa kuendelea kutenga na kupeleka fedha asilimia nne kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake kwani haina riba kuliko mikopo kutoka taasisi nyingine za kifedha.

Vile vile Mmbaga amesema kauli mbiu ya siku ya wanawake mwaka 2021 “ Wanawake katika Uongozi:Chachu ya kufikia Dunia yenye Usawa” itumike kuwawezesha wanawake kwenye nafasi za uongozi katika mkoa wa Simiyu kwa kuwa jamii bado haijatambua umuhimu wa kumuwezesha mwanamke nafasi za uongozi tunapoelekea kwenye Dunia ya usawa.

Naye Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Bi. Haula Kachwamba ametoa wito kwa viongozi wanawake kufanya kazi kulingana na matarajio ya wanawake huku akisisitiza wahakikishe wanatafuta ufumbuzi wa changamoto za wanawake.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera amewataka wanawake kujiamini na  kujitokeza katika fursa mbalimbali za uongozi katika jamii kwa kuwa viongozi wanawake ni wachache, hivyo kila fursa inapopatikana wasisite kujitokeza ili kuwe na viongozi wengi wanawake katika kuelekea dunia yenye usawa.

Maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Kimkoa yaliambatana na maonesho ya shughuli za wanawake wajasiriamali, uchangiaji damu, kutoa misaada kwa wagonjwa ambapo chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali (TUGHE) walitoa msaada wa mashuka 30 kwenye wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa.

MWISHO

Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Mwanahamisi Kawega(wa pili kushoto) ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kama Mgeni rasmi , akimsikiliza mjasiriamali mwanamke katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa Uwanja wa Nguzo nane Wilayani Maswa alipotembelea mabanda ya maonesho Machi 08, 2021.

Baadhi ya watumishi wanawake kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakiwa wamebeba bango kwenye maandamano ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzo nane Machi 08, 2021.



Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera  akitoa salamu kwa wanawake wa mkoa wa Simiyu wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.
 Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Simiyu,Mama Mariam Manyangu Mwera  akitoa salamu kwa wanawake wa mkoa wa Simiyu wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.
Baadhi ya watumishi wanawake kutoka Ofisi mbalimbali za Mkoa wa Simiyu wakiwa wamebeba bango lenye ujumbe maalum kwenye maandamano ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzo nane Machi 08, 2021.


Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa wakiimba wimbo wenye ujumbe maalum katika maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Machi 08, 2021 ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nugzonane wilayani Maswa.

Baadhi ya wanawake wakikimbia mbio za magunia ikiwa ni sehemu ya burudani katika maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Machi 08, 2021 ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nugzonane wilayani Maswa.


Baadhi ya viongozi na wanawake wa mkoa wa Simiyu wakicheza wimbo maalum  ulioimbwa na baadhi ya walimu wa kike katika maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Machi 08, 2021 ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa.

Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Mwanahamisi Kawega(wa pili kulia) ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kama Mgeni rasmi , akimsikiliza mdau katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa Uwanja wa Nguzo nane Wilayani Maswa alipotembelea mabanda ya maonesho Machi 08, 2021.

Vijana wa sarakasi wakitoa burudani wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.

Kutoka kulia, Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa  Bi. Agnes Alex, Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Mwanahamisi Kawega wakiteta jambo wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021,(wa tatu kushoto) ni  Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu Bi. Haula Kachwamba.
Baadhi ya wanawake wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.
Baadhi ya wanawake wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.

Baadhi ya wanawake wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.

Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Mwanahamisi Kawega(wa pili kushoto) ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kama Mgeni rasmi , akimsikiliza mjasiriamali mwanamke katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa Uwanja wa Nguzo nane Wilayani Maswa alipotembelea mabanda ya maonesho Machi 08, 2021.
Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Mwanahamisi Kawega(katikati) ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kama Mgeni rasmi , akiangalia baadhi ya bidhaa za wajasiriamali mwanamke katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa Uwanja wa Nguzo nane Wilayani Maswa alipotembelea mabanda ya m

Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Mwanahamisi Kawega(wa pili kushoto) ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kama Mgeni rasmi , akimsikiliza mjasiriamali mwanamke katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa Uwanja wa Nguzo nane Wilayani Maswa alipotembelea mabanda ya maonesho Machi 08, 2021.

Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bi. Mwanahamisi Kawega ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga kama Mgeni rasmi , akizungumza na mwanamke katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa Uwanja wa Nguzo nane Wilayani Maswa alipotembelea mabanda ya maonesho Machi 08, 2021.

Baadhi ya watumishi wanawake kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakiwa kwenye maandamano ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzo nane Machi 08, 2021.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa,Bi. Agnes Alex akitoa salamu kwa wanawake wa mkoa wa Simiyu wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.




Baadhi ya watumishi wanawake kutoka Ofisi mbalimbali za Mkoa wa Simiyu wakiwa wamebeba bango lenye ujumbe maalum kwenye maandamano ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzo nane Machi 08, 2021.
Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa akitoa taarifa ya chimbuko la Siku ya wanawake wakati maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzonane wilayani Maswa Machi 08, 2021.
Baadhi ya watumishi wanawake kutoka Ofisi mbalimbali za Mkoa wa Simiyu wakiwa wamebeba bango lenye ujumbe maalum kwenye maandamano ya siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Uwanja wa Nguzo nane Machi 08, 2021.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!