Saturday, March 6, 2021

NAIBU WAZIRI SILINDE ARIDHISHWA UJENZI WA BWALO, MADARASA SEKONDARI YA ANTHONY MTAKA BUSEGA

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde ameridhishwa na namna mradi wa ujenzi wa bwalo, vyumba viwili vya madarasa, maabara na matundu ya vyoo ulivyotekelezwa kwa viwango katika Shule ya Sekondari Anthony Mtaka iliyopo kata ya Lamadi wilayani Busega Mkoani Simiyu.

 

Silinde ameyasema hayo leo Machi 06, 2021 shuleni hapo alipotembelea mradi huo wakati wa ziara akikamilisha ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya shule ikiwemo mabweni, mambwalo, madarasa na matundu ya vyoo.

 

“Nimeisikiliza hii ripoti iliyosomwa na Mkuu wetu wa shule, nimekagua madarasa, maabara nimekagua na bwalo la chakula kwa kweli mmejenga kwa viwango vinavyoridhisha kikubwa zaidi mmekuwa na usimamizi mzuri wa fedha za serikali, kwa  kazi iliyofanyika hapa hiyo milioni 42 iliyosomwa hapa kama bakaa mnaweza mkaitumia kukamilisha madarasa mengine yaliyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi,” alisema.

 

Ameongeza kuwa Ofisi ya Rais TAMISEMI imedhamiria kudhibiti mapato na matumizi ya fedha za Serikali huku akiwataka watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwa wazalendo na waadilifu katika usimamizi wa fedha za serikali na kuhakikisha wanapopewa fedha kwa aajili ya utekeelzaji wa miradi watekeleze kwa mujibu wa maelekezo wanayopewa.

 

Aidha, Silinde amesema lengo la Serikali ya awamu ya tano ni kuboresha miundombinu ya elimu kwa ajili ya kuboresha mazingira ya utoaji elimu kwa watoto wa Kitanzania na ndiyo maana sasa hivi imejikita katika ujenzi wa mabweni bora, madarasa bora, mabwalo bora, maabara za kisasa na matundu ya vyoo bora na kuahidi kuwaondoa kwenye nafasi zao wale wote wenye nia ya kuikwamisha serikali.

 

Naye Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe. Simon Songe ameishukuru Serikali kwa fedha ilizotoa kwa jili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu wilayani Busega na kuahidi kuendelea kuzisimamia fedha hizo ili ziweze kutimiza azma ya serikali ya kuwaletea wananchi maendeleo.

 

Songe ameongeza kuwa wilaya ya Busega ina mahitaji ya shule 44 za sekondari zilizopo zikiwa 20 na ambazo zinatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni zikiwa nne, hivyo ameomba Serikali itakapoombwa fehda kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za wananchi katika ujenzi wa shule hizo itoe kipaumbele kwa wilaya hiyo ili kufikia lengo la kuwa na shule 44 za sekondari.

 

Kwa upande wao wanafunzi wa shule ya sekondari Anthony Mtaka wanaishukuru serikali kwa kuwajengea madarsa, bwalo na maabara jambo ambalo wamekiri kuwa litachangia katika kuboresha mazingira yao ya kujifunzia.

 

“Tunaishukuru serikali kutujengea maabara ambayo itatusaidia sana kufanya mazoezi ya vitendo hususani kwa wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi lakini na madarasa tuliyongewa tunashukuru pia maana yamepunguza msongamano darasani,” alisema George Daud kiranja Mkuu Anthony Mtaka sekondari.

 

“Pamoja na kutujenge madarasa maabara na vyoo mimi ninaishukuru serikali kwa kutujengea bwalo ambalo tutalitumia kwa matumizi mbalimbali zaidi ya kulia chakula, tutalitumia kufanyia mikutano na midahalo; hili litakuwa mkombozi maana tulikuwa tunafanyia vikao vyetu na midahalo chini ya miti,” alisema Sarah Mathias mwanafunzi shule ya sekondari Anthony Mtaka.

 

Awali akiwasilisha taarifa Mkuu wa Shule ya Sekondari Anthony Mtaka, Mwl. Joseph Kazimoto amesema fedha zilizopokelewa ni shilingi 196, 600,000/= kwa lengo la ujenzi wa bwalo, vyumba viwili ya madarasa, maabara na matundu sita ya vyoo na mara baada ya kukamilisha kazi hizo fedha iliyobaki ni jumla ya shilingi 42,894,100/= .

MWISHO

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde ( mwenye skafu) akielekea kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu ya elimu mara baada ya kuwasili shule ya sekondari Anthony Mtaka wakati wa ziara yake wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.


Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe. Simon Songe  akizungumza na baadhi ya viongozi na watendaji wa Wilaya ya Busega pamoja na watumishi na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Anthony Mtaka wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye skafu kulia) wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.

Sehemu ya mbele ya Bwalo lililojengwa kwa fedha zilizotolewa na serikali kupitia mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) katika shule ya sekondari Anthony Mtaka wilayani Busega.

Sehemu ya mbele ya moja ya chumba cha darasa kati ya viwili vilivyojengwa kwa fedha zilizotolewa na serikali kupitia mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) katika shule ya sekondari Anthony Mtaka wilayani Busega.Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde akikagua maabara iliyojengwa kwa fedha zilizotolewa na serikali kupitia mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) katika shule ya sekondari Anthony Mtaka wilayani Busega wakati wa ziara yake wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Anthony Mtaka iliyopo Kata ya Lamadi wilayani Busega wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde akizungumza alipozungumza  nao shuleni hapo wakati wa ziara yake wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye skafu) akiwa na viongozi wengine akielekea kukagua madarasa yaliyojengwa kwa fedha zilizotolewa na serikali kupitia mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) katika shule ya sekondari Anthony Mtaka wilayani Busega wakati wa ziara yake wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.

Mbunge wa Busega Mhe. Simon Songe akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye skafu kushoto) wakati alipotembea kuona maendeleo ya moja ya shule za wilaya ya Busega ambazo zinatarajiwa kukamilishwa ili iweze kusajiliwa ambapo imepewa jina na Mkuu wa Majeshi ya ulinzi  Jenerali Venance Mabeyo iliyopo katika kijiji cha Nyamikoma.

Sehemu ya jengo la Maabara inayojengwa katika shule inayotarajiwa kukamilika na kusajiliwa kwa jina la Mkuu wa Majeshi ya ulinzi  Jenerali Venance Mabeyo iliyopo katika kijiji cha Nyamikoma wilayani Busega.


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenyesuti kushoto) akikagua baadhi ya majengo katika zinatarajiwa kukamilishwa ili iweze kusajiliwa ambapo imepewa jina na Mkuu wa Majeshi ya ulinzi  Jenerali Venance Mabeyo iliyopo katika kijiji cha Nyamikoma.
Baadhi ya vyumba vya madarasa yanayojengwa katika shule inayotarajiwa kukamilika na kusajiliwa kwa jina la Mkuu wa Majeshi ya ulinzi  Jenerali Venance Mabeyo iliyopo katika kijiji cha Nyamikoma wilayani Busega.

Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe. Simon Songe  akizungumza na baadhi ya viongozi na watendaji wa Wilaya ya Busega pamoja na watumishi na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Anthony Mtaka wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde (mwenye skafu kulia) wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde ( mwenye skafu) akielekea kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu ya elimu mara baada ya kuwasili shule ya sekondari Anthony Mtaka wakati wa ziara yake wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. David Silinde akizungumza na baadhi ya viongozi na watendaji wa Wilaya ya Busega pamoja na watumishi na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Anthony Mtaka wakati wa ziara yake wilayani humo Machi 06, 2021 iliyokuwa na lengo la kukagua miundombinu ya elimu.

 


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!