Wednesday, January 2, 2019

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA UPATIKANAJI WA MAJI, UMEME

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewahakikishia wafanyabiashara mkoani hapa kuwa Serikali itatatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji na umeme kupitia mradi wa maji wa ziwa Victoria, uimarishwaji wa mamlaka za maji na kujengwa kwa vituo vya kupozea umeme.

Mtaka ameyasema hayo wakati ufunguzi wa hoteli ya Sweet Dreams iliyoko Mjini Bariadi na kumpongeza mfanyabiashara John Sabu kwa uwekezaji huo.

Amesema Mkoa unaendelea kuimarisha vyanzo vya maji na mamlaka za maji na kufikia mwaka 2020 maji kutoka Ziwa Victoria yatakuwa yameshafika katika makao makuu ya mkoa, huku akibainisha kuwa tatizo la umeme litatatuliwa na ujenzi wa vituo vya kupozea umeme.

“Sisi tuna mradi mkubwa wa maji wa  Ziwa Victoria ambao (kwa maelezo ya Waziri wa Maji) mpaka mwezi Februari 2019 watakuwa wametangaza zabuni ya ujenzi wa mradi huo ili maji yafike hapa, kwa kuanza mpaka kufikia mwaka 2020 maji yatakuwa yamefika makao makuu ya mkoa”

“Kwenye umeme tumezungumza na watu wa Wizara ya Nishati, tutajengewa (sub-stations) vituo viwili vya kupozea umeme, kwa kuanzia kimoja kitajengwa mwaka huu kwa hiyo tutakuwa na umeme wa uhakika” alisisitiza Mtaka.

Katika hatua nyingine Mtaka amewataka Wakuu wa Wilaya kuwalinda wafanyabiashara wakubwa na wadogo na kuwasaidia kutafsiri sheria, miongozo na taratibu zinazopaswa kuwasaidia kufanya biashara zao katika mazingira mazuri, huku akisisitiza biashara ziendelee kufanyika saa 24.

Kwa upande wao Wafanyabiashara wamempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa kuwaruhusu kufanya biashara saa 24 na wakamuahidi kuwa wataendelea kuwekeza katika ujenzi wa vitega uchumi mbalimbali ikiwemo hoteli za kisasa na kuendelea kuwa walipa kodi waaminifu.

“Tunamshukuru Mhe. Mkuu wa mkoa kwa kuruhusu wafanyabishara tufanye biashara zetu saa 24 tunamuahidi kuwa tutaendelea kufungua biashara mbalimbali kama hoteli  ili kuondoa adha ya malazi kwa wageni wanaofika hapa mkoani, pia tutaendelea kuwa walipa kodi halali wa nchi yetu” Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mhe. Njalu Silanga.

Awali akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa Hoteli ya Sweet Dreams mtoto wa Mmiliki wa hoteli hiyo, Mary John Sabu amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ubunifu na ushawishi wake uliopelekea matukio mengi ya Kitaifa kufanyika mkoani Simiyu, ambayo yamechangia kuongeza mzunguko wa biashara mkoani hapa.
MWISHO
Kutoka kushoto Mfanyabiashara wa Bariadi Bw. John Sabu, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mwenyekiti wa Wafanyabiashara mkoa wa Simiyu, Mhe. Njalu Silanga wakiteta jambo wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) na Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu, Mhe. Njalu Silanga wakiteta jambo wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni Mbunge wa Itilima Mhe. Njalu Silanga akizungumza na wafanyabiashara na viongozi wa mkoa huo, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ( wa pili kushoto) akisalimiana na Bibi. Elizabeth Mlanda mke wa Mfanyabiashara Clement Mlanda  mara  baada ya kutoa pongezi kwa Mfanyabiashara John Sabu anayemiliki Hoteli ya Sweet Dreams, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli hiyo Mjini Bariadi.
Mfanyabiashara kutoka Mjini Bariadi Bw. Yuma akimpongeza Mfanyabiashara John Sabu anayemiliki Hoteli ya Sweet Dreams (aliyeshika kinasa sauti)wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli hiyo Mjini Bariadi.

Sehemu ya Jengo la Hoteli ya Sweet Dreams(ghorofa) iliyopo Mjini Bariadi iliyofunguliwa hivi karibuni.

Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini (kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Tano Mwera wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.


Baadhi ya wafanyabiashara na wadau wa maendeleo wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(hayupo pichani) wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.
Mfanyabiashara John Sabu anayemiliki Hoteli ya Sweet Dreams na mkewe wakiingia katika hafla ya ufunguzi wa Hoteli hiyo Mjini Bariadi.
Watoto wa Mfanyabiashara John Sabu anayemiliki Hoteli ya Sweet Dreams wakiwasilisha risala ya ujenzi wa hoteli hiyo katika hafla ya ufunguzi wa Hoteli hiyo Mjini Bariadi.
Mfanyabiashara John Sabu anayemiliki Hoteli ya Sweet Dreams (kushoto) akizungumza na baadhi ya wafanyabiashara wenzake katika hafla ya ufunguzi wa Hoteli hiyo Mjini Bariadi.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo katika hafla ya ufunguzi wa Hoteli hiyo Mjini Bariadi.


Kutoka kushoto Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga,  Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni Mbunge wa Itilima Mhe. Njalu Silanga na Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini wakiteta jambo wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya JB wakitoa burudani wakati wa wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.
Mfanyabiashara Bw. James Nchubi  akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ( wa pili kulia) mara  baada ya kutoa pongezi kwa Mfanyabiashara John Sabu anayemiliki Hoteli ya Sweet Dreams, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Hoteli hiyo Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi, wafanyabiashara na wadau wakifuatilia masuala mbalimbali katika hafla ya ufunguzi wa Hoteli ya Sweet Dreams Mjini Bariadi.
Sehemu ya Jengo la Hoteli ya Sweet Dreams(ghorofa) iliyopo Mjini Bariadi iliyofunguliwa hivi karibuni.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!