Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt.Bashiru Ally amewataka wataalam wa ujenzi kuzingatia
miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua katika usanifu wa majengo yote ya Chama
na Serikali yanayoendela kujengwa hapa nchini, ili kupunguza gharama za
uendeshaji zinazotumika kununua/kulipia maji
na kuwa na uhakika wa upatikanaji wa huduma ya maji katika majengo hayo.
Ameyasema hayo Agosti 10, 2019 wakati akikagua maendeleao ya ujenzi wa
Hospitali ya Wilaya ya Bariadi na wakati
akiweka jiwe la msingi ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Busega mkoani Simiyu.
Amesema ikiwa majengo yote yatakuwa na miundombinu ya kuvuna
maji ikiwa ni pamoja na kuwa na matenki imara ya kuhifadhia maji hayo, inapotokea
maji yakakatika tunatumia maji yaliyovunwa lakini pia gharama za kuendesha
ofisi hususani za kulipia huduma zinapungua.
“Naelekeza nchini nzima majengo yote mapya ya Chama kuanzia yale
ya tawi, biashara na ofisi tuyasanifu kwa kuzingatia Miundombinu ya uvunaji wa
maji ya mvua, na ndani ya Serikali nimemshauri waziri wa maji kuwa miongoni mwa
mambo tunayotakiwa kuyafanya kukabiliana na changamoto ya maji ni ubunifu”
alisema Dkt. Bashiru
Kuhusu zao la pamba amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM) kuanzia ngazi ya tawi kuhakikisha wanafuatilia mwenendo wa ununuzi wa zao
la pamba na kuwasilisha taarifa kwake lengo likiwa ni kuhakikisha wakulima
wanapata haki yao.
“Sasa hivi Chama lazima kiwe mbele ya Serikali kutetea haki za
wavuja jasho, nchi nzima machinery (watendaji wote ) ya chama lazima ifuatilie
ununuzi wa mazao ya wakulima na mimi nipate taarifa za kila siku; maneno
yamesemwa mengi tangu mwezi wa tano, mwezi wa sita na wa saba tumekaa vikao mwezi huu wa nane ni vitendo”
alisema.
Kwa upade wake Mbunge wa Busega Mhe. Dkt. Raphael Chegeni amemshukuru
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Dkt. Bashiru Ally kwa kuielekeza Serikali kuimarisha
usimamizi wa suala la ununuzi wa pamba, ambapo hadi sasa limeanza kupata
ufumbuzi kwa wanunuzi kupewa fedha na benki kwa ajili ya kununua pamba kwa
wakulima kwa bei elekezi ya shilingi
1200/=
Akitoa
salamu za Serikali Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa
wananchi wa Wilaya ya Busega kutumia faida ya kuwa na Ziwa Victoria kufanya
shughuli za uvuvi kwa kutumia vizimba na mabwawa na wakati huo huo amewataka
kujihusisha na kilimo cha umwagiliaji ili kujihakishia usalama wa chakula.
Akiwa
Wilayani Bariadi, Dkt. Bashiru alitembelea eneo la ujenzi wa Tawi la Chuo cha
usimamizi wa Fedha(IFM) kijiji cha Sapiwi na kupongeza viongozi na wananchi wa
Kijiji hicho kwa kuwa na matumizi bora ya ardhi ya kijiji chao jambo ambalo
limepelekea kijiji kutoa eneo kwa ajili
ya ujenzi wa chuo hicho ambacho kitawaletea manufaa wao kama jamii ya Sapiwi na
Taifa kwa ujumla na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano huo.
Dkt.
Bashiru yuko katika ziara yake ya kikazi mkoani Simiyu kwa ajili ya masuala
mbalimbali ya Chama na kufuatilia suala la mwenendo wa ununuzi wa pamba.
MWISHO.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally
akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10,
2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally(wa nne
kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Chama na
Serikali baada ya kuweka jiwe la msingi
ujenzi wa Ofisi ya CCM Wilaya Busega Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake
wilayani Busega.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally(wa PILI
kulia mbele) akiwa na baaadhi ya viongozi wa Chama na Serikali akikagua jengo la Ofisi ya CCM Wilaya ya
Busega, baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi ofisi hiyo Agosti 10, 2019 wakati
wa ziara yake wilayani Busega.
Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Busega akitoa maelezo juu ya mchoro wa jengo la Ofisi ya CCM Wilaya ya Busega,
ambalo liliwejkewa jiwe la msingi na
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo na Mbunge wa Jimbo la Busega, Dkt. Raphael Chegeni wakifurahia jambo wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019 wilayani humo.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM
Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi
ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali
wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na
viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa
ziara yake wilayani Busega.
Mbunge wa Jimbo la Busega, Dkt. Raphael Chegeni
akizungumza kwa niaba ya wananchi
wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa
CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019 wilayani humo.
Mbunge wa Bariadi, Mhe. Andrew Chenge akizungumza
kwa niaba ya wananchi wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt.
Bashiru Ally Agosti 10, 2019 wilayani humo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi,
James John akimkabidhi Katibu Mkuu wa
CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally taarifa ya ujenzi wa hospitali ya wilaya Agosti
10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Moja ya majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Bariadi
ambayo yako katika hatua za ukailishaji.
Baadhi ya wananchi wakiwa wanashangilia jambo katika
kikao cha ndani cha Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally na viongozi wa Chama
na Serikali Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akatoa
salamu za wilaya ya Bariadi katika kikao cha
ndani cha Katibu Mkuu wa CCM
Taifa, Dkt. Bashiru Ally na watendaji na watumishi wa Chama na Serikali wilaya
Agosti 10, 2019
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Enock
Yakobo akifurahia jambo na Mkuu wa Mkoa
wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, wakati wa
Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiwasilisha
taarifa ya Mkoa wa Simiyu, wakati wa
Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mkuu wa Wilaya ya Busega , Mhe. Tano Mwera akiwasilisha taarifa ya
Wilaya ya Busega, wakati wa Ziara ya
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mjumbe wa NEC
kupitia Mkoa wa Simiyu, Bw. Gungu Silanga akikabidhi Mbunge wa Bariadi shuka
za kulalia wagonjwa kwa Mbunge wa
Bariadi, Mhe. Andrew Chenge(kulia) wakati wa Ziara ya Katibu mkuu wa CCM Taifa, Dkt.
Bashiru Ally wilayani Bariadi, Agosti 10, 2019.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti
10, 2019 akipokea maelezo ya namna ya kutunzwa mazingira katika eneo
ilipojengwa Ofisi ya CCM Wilaya ya Busega wakati wa ziara yake Wilayani Busega, Agosti 10, 2019.
Mbunge wa Busega Dkt. Raphael Chegeni akiwasalimia wananchi na wanachama Chama cha Mapinduzi. wakati wa Ziara ya Katibu
mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally wilayani Busega, Agosti 10, 2019.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM
Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi
ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Simiyu kupitia CCM,
Mhe. Ester Midimu akisalimia wananchi wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM
Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10,2019 wilayani Busega.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, ENOCK Yakobo
akitoa neno la shukrani kwa Katibu Mkuu
wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally baada ya kuzungumza na viongozi wa Chama na
Serikali na wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Simiyu kupitia CCM,
Mhe. Leah Komanya akisalimia wananchi wakati wa ziaraya Katibu Mkuu wa CCM
Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10,2019 wilayani Busega.
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakicheza
pamoja na wanakwaya ya Sayuni wilayani Busega wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa
CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10,2019 wilayani Busega.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally
akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10,
2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally
akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi katika Kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Agosti 10, 2019 wakati
alipotembelea na kujionea hali ya ujenzi wa
Tawi jipya la Chuo cha usimamizi
wa fedha (IFM) wilayani Bariadi.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(
kushoto) akimuongoza Katibu Mkuu wa CCM
Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi
ya wananchi katika Kijiji cha
Sapiwi wilayani Bariadi Agosti 10, 2019
wakati alipotembelea na kujionea hali ya ujenzi wa Tawi jipya la
Chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) wilayani Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali
wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na
viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa
ziara yake wilayani Busega.
0 comments:
Post a Comment