Sunday, August 11, 2019

DKT. BASHIRU: MAJENGO YOTE MAPYA YA CHAMA NA SERIKALI YAWE NA MIUNDOMBINU YA KUVUNA MAJI YA MVUA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt.Bashiru Ally  amewataka wataalam wa ujenzi kuzingatia miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua katika usanifu wa majengo yote ya Chama na Serikali yanayoendela kujengwa hapa nchini, ili kupunguza gharama za uendeshaji zinazotumika kununua/kulipia maji  na kuwa na uhakika wa upatikanaji wa huduma ya maji katika majengo hayo.

Ameyasema hayo Agosti 10, 2019  wakati akikagua maendeleao ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bariadi  na wakati akiweka jiwe la msingi ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Busega mkoani Simiyu.

Amesema ikiwa majengo yote yatakuwa na miundombinu ya kuvuna maji ikiwa ni pamoja na kuwa na matenki imara ya kuhifadhia maji hayo, inapotokea maji yakakatika tunatumia maji yaliyovunwa lakini pia gharama za kuendesha ofisi hususani za kulipia huduma zinapungua.

“Naelekeza nchini nzima majengo yote mapya ya Chama kuanzia yale ya tawi, biashara na ofisi tuyasanifu kwa kuzingatia Miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua, na ndani ya Serikali nimemshauri waziri wa maji kuwa miongoni mwa mambo tunayotakiwa kuyafanya kukabiliana na changamoto ya maji ni ubunifu” alisema Dkt. Bashiru

Kuhusu zao la pamba amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuanzia ngazi ya tawi kuhakikisha wanafuatilia mwenendo wa ununuzi wa zao la pamba na kuwasilisha taarifa kwake lengo likiwa ni kuhakikisha wakulima wanapata haki yao.

“Sasa hivi Chama lazima kiwe mbele ya Serikali kutetea haki za wavuja jasho, nchi nzima machinery (watendaji wote ) ya chama lazima ifuatilie ununuzi wa mazao ya wakulima na mimi nipate taarifa za kila siku; maneno yamesemwa mengi tangu mwezi wa tano, mwezi wa sita na wa saba  tumekaa vikao mwezi huu wa nane ni vitendo” alisema.

Kwa upade wake Mbunge wa Busega Mhe. Dkt. Raphael Chegeni amemshukuru Katibu Mkuu wa CCM Taifa Dkt. Bashiru Ally kwa kuielekeza Serikali kuimarisha usimamizi wa suala la ununuzi wa pamba, ambapo hadi sasa limeanza kupata ufumbuzi kwa wanunuzi kupewa fedha na benki kwa ajili ya kununua pamba kwa wakulima kwa  bei elekezi ya shilingi 1200/=

Akitoa salamu za Serikali Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Busega kutumia faida ya kuwa na Ziwa Victoria kufanya shughuli za uvuvi kwa kutumia vizimba na mabwawa na wakati huo huo amewataka kujihusisha na kilimo cha umwagiliaji ili kujihakishia usalama wa chakula.

Akiwa Wilayani Bariadi, Dkt. Bashiru alitembelea eneo la ujenzi wa Tawi la Chuo cha usimamizi wa Fedha(IFM) kijiji cha Sapiwi na kupongeza viongozi na wananchi wa Kijiji hicho kwa kuwa na matumizi bora ya ardhi ya kijiji chao jambo ambalo limepelekea kijiji  kutoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho ambacho kitawaletea manufaa wao kama jamii ya Sapiwi na Taifa kwa ujumla na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano huo.

Dkt. Bashiru yuko katika ziara yake ya kikazi mkoani Simiyu kwa ajili ya masuala mbalimbali ya Chama na kufuatilia suala la mwenendo wa ununuzi wa pamba.
MWISHO.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally(wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali  baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Ofisi ya CCM Wilaya Busega Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally(wa PILI kulia mbele) akiwa na baaadhi ya viongozi wa Chama na Serikali  akikagua jengo la Ofisi ya CCM Wilaya ya Busega, baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi ofisi hiyo Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega akitoa maelezo juu ya mchoro wa jengo la Ofisi ya CCM Wilaya ya Busega, ambalo liliwejkewa jiwe la msingi na  Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo na Mbunge wa Jimbo la Busega, Dkt. Raphael Chegeni wakifurahia jambo wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019 wilayani humo.



Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.



Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Mbunge wa Jimbo la Busega, Dkt. Raphael Chegeni akizungumza kwa niaba ya wananchi  wakati  wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019 wilayani humo.
Mbunge wa Bariadi, Mhe. Andrew Chenge akizungumza kwa niaba ya wananchi  wakati  wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019 wilayani humo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, James John  akimkabidhi Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally taarifa ya ujenzi wa hospitali ya wilaya Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Moja ya majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Bariadi ambayo yako katika hatua za ukailishaji.
Baadhi ya wananchi wakiwa wanashangilia jambo katika kikao cha ndani cha Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally na viongozi wa Chama na Serikali Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akatoa salamu za wilaya ya Bariadi katika kikao cha  ndani  cha Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally na watendaji na watumishi wa Chama na Serikali wilaya Agosti 10, 2019
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Enock Yakobo  akifurahia jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, wakati  wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiwasilisha taarifa ya Mkoa wa Simiyu, wakati  wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mkuu wa Wilaya ya Busega  , Mhe. Tano Mwera akiwasilisha taarifa ya Wilaya ya Busega, wakati  wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019.
Mjumbe wa NEC  kupitia Mkoa wa Simiyu, Bw. Gungu Silanga akikabidhi Mbunge wa Bariadi shuka za kulalia wagonjwa kwa Mbunge  wa Bariadi, Mhe. Andrew Chenge(kulia) wakati wa Ziara ya Katibu mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally wilayani Bariadi, Agosti 10, 2019.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10, 2019 akipokea maelezo ya namna ya kutunzwa mazingira katika eneo ilipojengwa Ofisi ya CCM Wilaya ya Busega wakati wa ziara yake  Wilayani Busega, Agosti 10, 2019.


Mbunge wa Busega Dkt. Raphael Chegeni  akiwasalimia wananchi na wanachama  Chama cha Mapinduzi. wakati wa Ziara ya Katibu mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally wilayani Busega, Agosti 10, 2019.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.
Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Simiyu kupitia CCM, Mhe. Ester Midimu akisalimia wananchi wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10,2019 wilayani Busega.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, ENOCK Yakobo akitoa neno la shukrani  kwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally baada ya kuzungumza na viongozi wa Chama na Serikali na wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Simiyu kupitia CCM, Mhe. Leah Komanya akisalimia wananchi wakati wa ziaraya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10,2019 wilayani Busega.
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakicheza pamoja na wanakwaya ya Sayuni wilayani Busega wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally Agosti 10,2019 wilayani Busega.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Bariadi.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi  katika Kijiji cha Sapiwi  wilayani Bariadi Agosti 10, 2019 wakati alipotembelea na kujionea hali ya ujenzi wa  Tawi jipya la  Chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) wilayani Bariadi.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka( kushoto)  akimuongoza Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi  katika Kijiji cha Sapiwi  wilayani Bariadi Agosti 10, 2019 wakati alipotembelea na kujionea hali ya ujenzi wa  Tawi jipya la  Chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) wilayani Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali na baadhi ya wananchi Agosti 10, 2019 wakati wa ziara yake wilayani Busega.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!