Friday, August 9, 2019

VITA DHIDI YA UVUVI HARAMU YAONGEZA KIASI CHA SAMAKI WAKUBWA ZIWA VICTORIA


Waziri wa  Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina amesema mapambano dhidi ya uvuvi haramu yamechangia kuongezeka kwa kiasi cha samaki wakubwa ambapo kwa sasa upatikanaji wake ni asilimia 5.2 kutoka asilimia 0.3 ya awali kabla ya operesheni kuanza.

Ameyasema hayo Agosti 07, 2019 wakati akitembelea mabanda ya wizara ya mifugo na uvuvi kwenye maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.

Aidha, amesema kuwa katika upambanaji dhidi ya uvuvi haramu kiwango cha samaki wazazi katika Ziwa Vikitoria kimeongezeka na kuvuka kiwango kinachotakiwa hadi kufikia asilimia 5.2 kutoka asilimia 0.3 hali iliyopelekea kupungua kwa samaki katika Ziwa hilo ambapo uhitaji wa samaki wazazi ni angalau  asilimia 3.2 .

“ uvuvi haramu ulipelekea kuongeza kwa kiwango cha samaki wachanga ndani ya ziwa … karibia ziwa lote lilikuwa na samaki wachanga kwa kiwango cha asilimia 96.6% ambapo kwa sasa kimeshuka na kufikia 62.8% jambo hili  lilipekea kupungua samaki wakubwa” alisema waziri mpina .

Ameongeza kuwa hali hiyo ilipelekea serikali kutumia kiasi cha shilingi bilioni 56 kwa ajili ya kuagiza samaki wa vitoweo nje ya nchi ambapo kimeshuka na kufikia bilioni 11 ambapo kiasi cha bilioni 40 kimeokolewa na samaki aina ya sangara waliopo katika Ziwa Victoria limefikia tani 555 kutoka 417.

Katika hatua nyingine Waziri wa mifugo na uvuvi Luhaga Mpina amesema kuwa wizara hiyo imejipanga kutatua changamoto ya chakula cha  mifugo hususani cha samaki ambacho kimekuwa kikiagizwa kutoka nje ya nchi, huku akiwahakikishia wadau wa mifugo na uvuvi kuwa serikali   imejipanga kutafuta soko la uhakika ili wavuvi waweze kufuga na  kuuza kwa urahisi.
MWISHO
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina akipewa maelezo juu ya teknolojia ya ufgaji wa samaki kupitia matanki, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(wa nne kushoto) akipewa maelezo juu ya mfano wa teknolojia ya ufugaji wa samaki kupitia vizimba ambayo hufanyika ziwani, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(mwenye miwani) akipewa maelezo juu ya zana bora za kilimo zinazouzwa na Kampuni ya AGRICOM, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye Maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.



Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(wa pili mbele) akielekea kwenye eneo la malisho ya mifugo, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye Maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina akiangalia ng,ombe wanaofugwa kisasa, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye Maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(mwenye miwani) akipewa maelezo namna mashine ya kuandaa chakula cha mifugo inavyofanya kazi, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye Maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(wa nne kushoto) akipewa maelezo juu ya mfano wa teknolojia ya ufugaji wa samaki kupitia vizimba ambayo hufanyika ziwani, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(wa nne kushoto) akipewa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa na wataalam wa ofisi yake, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(wa nne kushoto) akipewa maelezo kuhusu huduma zinazotolewa na wataalam wa ofisi yake, wakati alipotembelea mabanda ya mifugo na uvuvi kwenye maonesho ya nane nane Kitaifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!