Thursday, August 22, 2019

RC MTAKA AMPONGEZA JPM KUWA MWENYEKITI SADC, ATOA WITO KWA WAWEKEZAJI VIWANDA VYA DAWA, VIFAA TIBA










Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, MHE. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini  mwa Afrika (SADC), ambapo pia ametoa wito kwa wawekezaji kuwekeza kwenye viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini, ili kuiwezesha Bohari ya Dawa (MSD) ambayo ni mzabuni wa dawa na vifaa tiba wa nchi za SADC kupunguza uagizaji wa dawa na vifaa tiba nje ya nchi.

Mtaka ametoa pongezi hizo Agosti 21, 2019 wakati akifunga mkutano wa siku tatu wa Menejimenti ya Bohari ya Dawa (MSD) na mameneja wa Kanda za Bohari ya Dawa (MSD) uliofanyika kwa lengo la kufanya tathmini ya utendaji.

Mtaka amesema Bohari ya Dawa kama mzabuni wa dawa na vifaa tiba katika nchi za SADC wanapaswa kutumia fursa ya Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa SADC kwa kuhimiza wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza kwenye ujenzi wa viwanda vya dawa na vifaa tiba.

“Nampongeza Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na Pongezi nzuri kwa Mhe. Rais ni pale ambapo nchi yetu ambao pia tuna faida ya kuwa mzabuni wa dawa na vifaa tiba kwenye SADC; tutapata Watanzania wengi watakaochangamkia fursa ya kuwekeza na kutumia nafasi ya Tanzania kuwa Mwenyekiti wa SADC tukiwa na Idadi ya watu wengi kwenye soko la dawa na vifaa tiba” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka ameongeza kuwa Kiwanda cha Vifaa tiba kinachotarajiwa kujengwa mkoani Simiyu   


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifunga mkutano wa Menejimenti ya Bohari ya Dawa MSD Agosti 21, 2019  iliyofanyika kwa lengo la kufanya tathmini ya utendaji ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu

Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurian Bwanakunu akizungumza na wajumbe wa menejimenti ya MSD katika Mkutano wao maalum wa tathmini ya utendaji ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Bohari ya Dawa(MSD), Victoria Mwanri Elangwa  akitoa taarifa ya yaliyofanyika katika Mkutano wao maalum wa tathmini ya utendaji ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu mkutano amabo umehitimishwa na Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka Agosti 21, 2019.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi na Mameneja wa Kanda wa Bohari ya Dawa (MSD) baada ya kufunga Mkutano wao maalum wa tathmini ya utendaji ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Bohari ya Dawa(MSD), Victoria Mwanri Elangwa akimweleza jambo Mkuu wa Mkoa wa  Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka Agosti 21, 2019 baada ya kufungwa kwa Mkutano maalum wa tathmini ya utendaji wa Menejimenti ya MSD ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Bohari ya Dawa(MSD), Victoria Mwanri Elangwa akimweleza jambo Mkuu wa Mkoa wa  Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka Agosti 21, 2019 baada ya kufungwa kwa Mkutano maalum wa tathmini ya utendaji wa Menejimenti ya MSD ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

Mmoja wa Wakurugenzi katika Bohari ya Dawa(MSD) akitoa taarifa wakati wa kufunga Mkutano maalum wa tathmini ya utendaji wa Menejimenti ya MSD ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa mkoa wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurian Bwanakunu(wa pili kulia) na Wajumbe wengine wa Menejimenti ya MSD baada ya kufungwa kwa Mkutano maalum wa tathmini ya utendaji wa Menejimenti ya MSD ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Bohari ya Dawa(MSD), Victoria Mwanri Elangwa akimweleza jambo Mkuu wa Mkoa wa  Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka Agosti 21, 2019 baada ya kufungwa kwa Mkutano maalum wa tathmini ya utendaji wa Menejimenti ya MSD ambao umefanyika kwa muda wa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!