Thursday, May 7, 2020

CUAMM WATOA MSAADA VIFAA KINGA KUSAIDIA KUKABILIANA NA CORONA SIMIYU


Shirika lisilo la kiserikali la Doctor with Africa CUAMM linalofanya kazi na Mkoa wa Simiyu kama mdau wa Afya katika masuala ya UKIMWI na Huduma za Afya ya Mama na mtoto limetoa msaada wa vifaa kinga (viambukuzi) kwa ajili ya kuunga mkono Serikali katika kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Akikabidhi msaada huo  Mei 06, 2020 mjini Bariadi kiongozi kutoka CUAMM Bi. Barbara Andreuzizi amesema  Vifaa kinga hivyo vina thamani ya shilingi  milioni nne ambapo amebainisha kuwa Shirika hilo pia limetoa msaada mafuta na gari litakalotumiwa na wataalam wa afya kutoa elimu ya tahadhari ya maambukizi ya Virusi vya Corona katika mkoa  wa Simiyu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini ameshukuru CUAMM kwa kutoa msaada huo ambao ni sehemu ya makubaliano ya wadau wa afya na serikali mkoani humo katika kukabiliana na Corona na kuiagiza Timu ya mkoa ya usimamizi wa huduma za afya kuhakikisha vifaa hivyo vinapelekwa haraka katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa wakati.

“Tatizo la COVID 19 liliporipotiwa kama mkoa tulikutana na wadau tukakubaliana  kujiandaa namna ya kukabiliana nalo katika maeneo ya utoaji elimu, vifaa kinga na vifaa tiba, tunawashukuru sana CUAMM kwa vifaa kinga hivi ambavyo naamini vitasaidia timu zetu za usimamizi wa Afya(CMT) za Wilaya na vituo vya kutolea huduma za afya,” alisema Sagini.

Aidha, Sagini amewataka wataalam wa afya ngazi ya  Mkoa wakiongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa kusimamia mafuta na gari lililotolewa na CUAMM kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na kuhakikisha linafanya kazi iliyokusudiwa na elimu inawafikia wananchi inavyostahili mpaka maeneo ya vijijini.

 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange Simiyu inaendelea na jitihada mbalimbali kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona ambapo amewashukuru CUAMM kutoa msaada wa vifaa kinga vitakavyosaidia  katika utoaji wa huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kutoa wito kwa wadau wengine kuendelea kuunga mkono na wananchi kuendelea kuchukua tahadhari.

Naye Mratibu wa Mpango wa kukabiliana na Maambukizi ya Virusi vya Corona Dkt. Khamis Kulemba amesema msaada wa vifaa kinga, mafuta na gari kwa ajili ya kutoa elimu ni muhimu sana kwa kipindi hiki, ambapo amebainisha kuwa wataalam wa afya watashirikiana na Shirika hilo kuhakikisha elimu ya tahadhari ya Corona inawafikia wananchi na vifaa kutumika ipasavyo.
MWISHO

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kushoto)akipokea msaada wa vifaa kinga(viambukuzi) kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona,  kutoka Shirika lisilo la kiserikali la Doctors with Africa CUAMM uliowasilishwa na Bi. Bi.Barbara Andreuzizi, Mei 06, 2020 Mjini Bariadi.



 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kushoto)akipokea msaada wa vifaa kinga(viambukuzi) kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona,  kutoka Shirika lisilo la kiserikali la Doctors with Africa CUAMM uliowasilishwa na Bi. Bi.Barbara Andreuzizi, Mei 06, 2020 Mjini Bariadi.



 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akitoa shukrani mara baada ya kupokea msaada wa vifaa kinga(viambukuzi) kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona, kutoka Shirika lisilo la kiserikali la Doctors with Africa CUAMM uliowasilishwa na Bi. Bi.Barbara Andreuzizi, Mei 06, 2020 Mjini Bariadi.


 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange akizungumza kabla ya makabidhiano ya msaada wa vifaa kinga( viambukuzi)  kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona vilivyotolewa na Shirika lisilo la kiserikali la Doctors with Africa CUAMM kwa mkoa wa Simiyu na kukabidhiwa kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini  na  Bi.Barbara Andreuzizi, Mei 06, 2020 Mjini Bariadi.


 Mratibu wa Mpango wa kukabiliana na Corona Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba akizungumza kabla ya makabidhiano ya msaada wa vifaa kinga( viambukuzi)  kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona, vilivyotolewa na Shirika lisilo la kiserikali la Doctors with Africa CUAMM;  kati ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini  na Bi. Barbara Andreuzizi, Mei 06, 2020 Mjini Bariadi.


Vifaa kinga(viambukuzi) vilivyotolewa na shirika lisilo la kiserikali la CUAMM kwa mkoa  wa Simiyu katika kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!