Saturday, October 6, 2018

BALOZI KAZUNGU: NINGEPENDA NIONE TAKWIMU ZA BIASHARA, UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA KENYA ZIKIONGEZEKA


Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu amesema angependa kuona  katika kipindi chake atakachokuwepo hapa nchini akiiwakilisha nchi ya Kenya ushirikiano wa kiabishara katika Kenya na Tanzania na unaimarika na takwimu za biashara, viwanda na uwekezaji kati ya nchi hizo zikiongezeka mara dufu.

Balozi Kazungu ameyasema hayo wakati alipotembelea Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance (Alliance Ginnery LTD), kilichopo Kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Oktoba 05, 2018 katika ziara yake mkoani Simiyu.

Balozi Kazungu amesema ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji hususani katika viwanda, kati ya Tanzania na Kenya ukiendelea kuimarika zaidi utachangia kuongeza ajira, kuwatoa wananchi katika umaskini pamoja na kuimarika kwa uchumi wa nchi hizo pia.

“Baada ya miaka minne kazi yangu kama ikiisha hapa, naomba nione takwimu za viwanda, biashara, uwekezaji kati ya Tanzania na Kenya zinaongezeka mara dufu, nafasi za kazi kwa watu wetu zinapatikana na watu wetu wanaondokana na umasikini; kukua kwa Tanzania kuwe ndiyo kukua kwa Kenya hilo ndiyo ombi letu” alisema Mhe. Balozi Kazungu.

Aidha, Mhe. Kazungu ametoa wito kwa  wananchi wa Tanzania na Kenya kuepuka migogoro ya kibiashara ambayo kwa namna moja au nyingine inaweza kuchangia katika kushuka kwa biashara kati ya nchi hizo, huku akiwataka waandishi wa habari kuwa makini na kijiridhisha kabla kuandika habari za kibiashara kwani zisipoandikwa kwa usahihi zinaweza kuchochea migogoro ya kibiashara.

Aidha, Balozi Kazungu amemhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kuwa atakuwa mstari wa mbele kuzungumza na wawekezaji nchini Kenya ili waje kuwekeza, ambapo amebainisha kuwa Sekta binafsi na Shirikisho la watu wenye viwanda hapa nchini wameshaanza kuzungumzia masuala hayo na wenzao wa Sekta binafsi Kenya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu , Mhe. Anthony Mtaka amemwomba Balozi Kazungu kuwaalika wawekezaji kutoka nchini Kenya na kubainisha kuwa mkoa uko tayari kutoa ardhi bure kwa wawekezaji watakaojenga viwanda vinavyojibu mahitaji ya mkoa, hususani katika kuongeza thamani ya zao la pamba, mazao yatokanayo na mifugo kama ngozi na nyama.

Mtaka amesema Mkoa wa Simiyu una uwezo wa kuzalisha pamba zaidi ya kilo milioni 400 na hadi sasa umezalisha kilo milioni112 ambazo ni zaidi ya asilimia 50 ya pamba yote nchini; hivyo katika kuiongezea thamani pamba hiyo kiwanda kikubwa cha kuzalisha bidhaa zaidi ya 20 za afya zitokanazo na pamba

“Simiyu tunao uwezo wa kuzalisha zaidi ya kilo milioni 400 za pamba, mpaka sasa tumezalisha kilo milioni 112 ambazo ni zaidi ya asilimia 50 ya pamba yote inayozalishwa hapa nchini; katika kuongeza thamani ya zao la pamba, mwaka huu tutaanza ujenzi wa kiwanda kikubwa kitakachozalisha zaidi ya bidhaa 20 za afya zitokanazo na pamba, kitakachojengwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi(WCF) kwa kushirikiana na wadau wengine na Mkoa wa Simiyu tumetoa ardhi bure” alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa kipaumbele cha pili cha mkoa baada ya kujenga kiwanda hicho ni kuwa na uwekezaji katika viwanda vya nguo(textile industries) ili kupata bidhaa ya mwisho katika zao la pamba, hivyo akaendelea kutoa wito kwa wawekezaji ndani na nje ya nchi kuwekeza katika eneo hili.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Alliance Ginnery Ltd, Bw. Boaz Ogola ambaye ni Mwekezaji kutoka Nchini Kenya amesema lengo la Kampuni hiyo yenye Kiwanda cha kuchambua pamba ni kwenda katika kuongeza thamani ya zao la pamba, ili faida itakayopatikana irudi kwa wakulima kwa kuifanya pamba yao ikanunuliwa kwa bei nzuri itakayowapa motisha ya kuendelea kuzalisha zaidi.
MWISHO
Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (wa pili kushoto) akiangalia mbegu za zao la pamba zinazozalishwa katika Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance (Alliance Ginnery Ltd), kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 05, 2018. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Alliance Ginnery Ltd, Bw. Boaz Ogola ambaye ni mwekezaji kutoka Nchini kenya(wa kwanza kulia), akimuongoza Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (wa pili kulia) na viongozi wengine wa mkoa wa Simiyu, kuelekea katika moja ya majengo ya Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati wa ziara ya Balozi huyo kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018.
Mfanyakazi wa katika Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance (Alliance Ginnery Ltd), kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, akitoa maelezo ya namna mbegu za pamba zinavyoandaliwa kwa Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (aliyeshika mbegu katikati), wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 05, 2018. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiangalia akiangalia mbegu za zao la pamba zinazozalishwa katika Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance (Alliance Ginnery Ltd), kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani humo, wakati ziara ya Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (wa nne kulia) kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018.

Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (wa tatu kushoto) akiangalia pamba iliyochambuliwa katika Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance (Alliance Ginnery Ltd), kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 05, 2018 (kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na (wa pili kushoto) Mkurugenzi wa Kampuni ya Alliance Ginnery Ltd, Bw. Boaz Ogola akitoa maelezo kwa Balozi huyo.
Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (aliyetanguliza mikono kushoto) akiwaeleza jambo viongozi wa mkoa wa Simiyu na viongozi wa Kiwanda ca kuchambua pamba cha  Alliance Ginnery Ltd, wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 05, 2018.
Mfanyakazi wa katika Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance (Alliance Ginnery Ltd), kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, akitoa maelezo ya namna mbegu za pamba zinavyoandaliwa kwa Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (wa tatu kulia), wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 05, 2018.
Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (wa pili kulia) akimweleza jambo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) wakiwa katika Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati wa ziara ya Balozi huyo kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Alliance Ginnery Ltd, Bw. Boaz Ogola ambaye ni mwekezaji kutoka Nchini Kenya(wa pili kulia), akitoa maelezo kwa  Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (katikati) katika moja ya majengo ya Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati wa ziara ya Balozi huyo kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Alliance Ginnery Ltd, Bw. Boaz Ogola ambaye ni mwekezaji kutoka Nchini Kenya(wa pili kulia), akitoa maelezo kwa  Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (katikati) katika moja ya majengo ya Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati wa ziara ya Balozi huyo kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Alliance Ginnery Ltd, Bw. Boaz Ogola ambaye ni mwekezaji kutoka Nchini kenya(kulia), akimuongoza Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (wa pili kulia) na viongozi wengine wa mkoa wa Simiyu, kuelekea katika moja ya majengo ya Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati wa ziara ya Balozi huyo kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018.

Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (kushoto) akiwaeleza jambo baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance katika moja ya majengo hicho kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati wa ziara ya Balozi huyo kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kiwanda cha Kuchambua pamba cha Alliance(Alliance Ginnery Ltd) wakiendelea na kazi katika sehemu ya uzalishaji wa mbegu katika kiwanda hicho kilichopo kata ya Kasoli wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, wakati wa ziara ya Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu(hayupo pichani)  kiwandani  hapo, Oktoba 05, 2018


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!