Saturday, October 27, 2018

NAIBU WAZIRI MABULA ASHAURI WIZARA YA VIWANDA KUANZISHA KLINIKI NGAZI YA KANDA KUWASAIDIA WAFANYABIASHARA


Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula ameshauri Wizara ya Viwand, Biashara na Uwekezaji kuona namna ya kuwa na Kliniki za Biashara ngazi ya kanda ili kuwasaidia wafanyabiashara hususani wale wanaoanza, wajasiriamali wadogo na wasiojua taratibu za uendeshaji wa biashara zao kujua na kuwa wafanyabiashara wazuri.

Mhe.Mabula ameyasema hayo mara baada ya kutembelea banda la Maonesho la Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara(TanTrade) katika Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.

Amesema amepongeza Wizara ya Viwanda, Biashara na uwekezaji kubuni Kliniki ya biashara ambayo inachangia kuwandaa wafanyabiashara kufahamu wafanye nini kabla na baada ya kuanzisha biashara na kufanya biashara zao kwa kuzingata sheria, kanuni na taratibu za nchi hii

“Ili mtu awe huru kufanya biashara yake ni lazima zingatie sheria kanuni na taratibu za nchi hii, mtu anapokuja kwenye kliniki hii anaambiwa kabla ya kuanza anatakiwa apitie hatua zipi na aweke mazingira yapi, ili atambulike na TRA anapaswa afanye nini  na mambo mengine mengi na wakizingatia wanachoambiwa hapa hawahitaji kukimbizana na mgambo wa polisi”

“Ninashauri Wizara ya Viwanda ione namna ya kuwa na kliniki za biashara kikanda ili wafanyabiashara wanaoanza, wajasiriamali wadogo na wale wasiojua taratibu waweze kujua taratibu na wawe wafanyabiashara wazuri” alisema Mhe. Mabula.

Afisa Biashara Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara hapa nchini (TanTrade) Bi. Magdalena Shirima amesema hadi kufikia Oktoba 26, 2018 wajasiriamali zaidi ya 60 walioshiriki katika Maonesho ya SIDO Kitaifa wamehudhuria Kliniki hiyo kupata huduma.

Baadhi ya Wajasiriamali waliopata nafasi ya kushiriki na kupata huduma za ushauri wa kibiashara kupitia Kliniki hiyo wamesema imewasaidia kubadili mitazamo dhidi ya biashara zao na kufahamu mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uanzishaji wa biashara, namna ya kutangaza biashara zao na umuhimu wa kusajili biashara zao ili ziweze kutambulika kisheria.

Maonesho haya ya Viwanda Vidogo (SIDO) ni ya kwanza Kitaifa yakiwa na Kauli Mbiu “Pamoja Tujenge Viwanda Kufikia Uchumi wa Kati” ambayo yalianza Oktoba 23, 2018 yatahitimishwa Oktoba 28, 2018.
MWISHO
Naibu Waziri waNyumba na Maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula akizungumza na Watumishi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE) alipotembelea banda la Mamlaka hiyo katika Maonesho ya SIDO Kitaifa Oktoba 26, 2018  yanayoendelea katika  Viwanja vya Nyakabindi Simiyu, ambapo huduma za Kliniki ya Biashara zinatolewa. 

Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula(wa pili kushoto) akiongozwa na viongozi wa Shirika la Kuhudumia viwanda Vidogo (SIDO) kuelekea katika kutembelea mabanda ya maonesho ya Maonesho ya SIDO Kitaifa Oktoba 26, 2018  yanayoendelea katika  Viwanja vya Nyakabindi Simiyu.

Naibu Waziri waNyumba na Maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la maonesho la Kiwanda cha Chaki Maswa Oktoba 26, 2016 wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya maonesho katika ya Maonesho ya SIDO Kitaifa Oktoba 26, 2018  yanayoendelea katika  Viwanja vya Nyakabindi Simiyu.
 Afisa kutoka Shirika la Viwango nchini (TBS) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri waNyumba na Maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula mara baada ya kutembelea banda la maonesho la shirika hilo, wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya maonesho katika ya Maonesho ya SIDO Kitaifa Oktoba 26, 2018  yanayoendelea  katika  Viwanja vya Nyakabindi Simiyu.
Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akipewa maelezo kuhusu mashine mbali za kuongeza thamani mazao mbalimbali wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya maonesho katika ya Maonesho ya SIDO Kitaifa Oktoba 26, 2018  yanayoendelea  katika  Viwanja vya Nyakabindi Simiyu.
Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akiangalia baadhi ya bidhaa za ngozi zilizotengenezwa a wajasiriamali wadogo , wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya maonesho katika ya Maonesho ya SIDO Kitaifa Oktoba 26, 2018  yanayoendelea  katika  Viwanja vya Nyakabindi Simiyu.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!