Thursday, October 4, 2018

BALOZI WA KENYA AFANYA ZIARA SIMIYU KUJIONEA FURSA ZA UWEKEZAJI


Balozi wa Kenya nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu amefanya ziara mkoani Simiyu Oktoba 03, 2018 na kuzungumza na viongozi wa mkoa huo, ambapo ameeleza kuwa moja ya malengo ya ziara yake ni kufahamu Mipango na Fursa za Uwekezaji zilizopo mkoani Simiyu, ili aweze kuzungumza na wawekezaji nchini Kenya kuwekeza mkoani humo.

Balozi Kazungu amesema nchi ya Kenya ndiyo inaongoza kuwekeza nchini Tanzania ukilinganishwa na  nchi nyingine za Afrika ambapo hadi sasa imewekeza takribani dola za Kimarekani bilioni 1.6 hapa nchini.

“ Nimekuja hapa ili tufahamiane  vizuri, nijue mipangilio yenu, fursa za uwekezaji ziko wapi ili tuweze kuzungumzana wenzetu wakaja kuwekeza, Kenya ni nchi inayoongoza kwa kuwekeza nchini Tanzania, hadi sasa imewekeza takribani dola bilioni 1.6 ” alisema Balozi Kazungu.

Aidha, ameomba ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya uendelee kuimarishwa kwa lengo la kuzifanya  nchi hizi kuwa shina la viwanda na uwekezaji na kuwa wanufaika wa soko la pamoja la Afrika hali itakayochangia kuimarisha uchumi wa nchi hizo.

Pamoja na ushirikiano katika masuala ya uwekezaji na viwanda Balozi Kazungu amesisitiza masuala ya ujirani mwema, upendo na ushirikiano wa kindugu baina ya nchi hizo mbili.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo inakaribisha sekta binafsi  na iko tayari kutoa ardhi bure kwa wawekezaji walio tayari kuwekeza Simiyu katika maeneo yanayojibu  mahitaji ya mkoa na nchi kupitia malighafi zinazolishwa ndani ya mkoa na ndani ya nchi.

“Kwa mtu aliye tayari kujenga kiwanda kinachojibu mahitaji yetu kama mkoa hasa kitakachutumia malighafi tulizonazo mfano atakayewekeza kwenye viwanda vya kusindika nyama, viwanda vya kutengeneza bidhaa za ngozi, pamba na yeyote atakayewekeza kwenye viwanda vyenye malighafi inayozalishwa hapa nchini, tutampa ardhi bure” alisema

Mtaka amemweleza Balozi Kazungu kuwa mkoa huo pia uko tayari kutoa  ardhi bure kwa wawekezaji walio tayari kuwekeza kwenye ujenzi wa vyuo ikiwemo vya ufundi na utalii ili kuwajengea vijana ujuzi .

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema mafanikio ya Mkoa huo yanayopelekea kufanya  vitu vikaonekana ikiwa ni pamoja na kuwa na Mwongozo wa Uwekezaji ni ushirikiano uliopo kati ya viongozi, watendaji, wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwepo Taasisi za Serikali na binafsi, sekta binafsi, madhehebu ya dini pamoja na wananchi
.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery kilicjopo Bariadi, Bw. Boaz Ogola ambaye ni Mwekezaji kutoka nchini Kenya amemweleza Balozi kuwa Tanzania ni nchi yenye amani na  mahali sahihi kwa uwekezaji, hivyo  akatoa wito kwa  Mhe. Balozi kuwaalika Wafanyabiashara kutoka Kenya kuja kuwekeza Simiyu na Tanzania kwa ujumla
MWISHO


Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu akisaini kitabu cha katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,  mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani humo, Oktoba 03, 2018(kushoto) Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(katikati) Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka.

Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka(kulia)  , mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani humo, Oktoba 03, 2018.
Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka(kulia) ,  mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani humo, Oktoba 03, 2018.
 Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akisalimiana na  Balozi wa Kenya nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu, mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018. 
Balozi wa Kenya nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu, akisalimiana na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.
 Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Itilima wa Simiyu Mhe.Benson Kilangi, mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018. 


Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu akisaini kitabu cha katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,  mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani humo, Oktoba 03, 2018(kushoto) Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(katikati) Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka (katikati) akitoa maelezo ya Mkoa kwa Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu(kulia), ambaye alifika mkoani humo kwa ziara ya kikazi Oktoba 03, 2018
Kutoka kulia Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery  kilichopo Bariadi, Bw. Boaz Ogola wakiteta jambo, wakati wa ziara ya Balozi huyo mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.
Kutoka kushoto  Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, wakimuonesha jambo Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu katika Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara ya Balozi huyo mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018. 
Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Mhandisi. Wilbert Siogopi , mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani humo, Oktoba 03, 2018.
 Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka(katikati) akizungumza  na  Balozi wa Kenya nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu, mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018. 
Kutoka kulia Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery  kilichopo Bariadi, Bw. Boaz Ogola wakiteta jambo, wakati wa ziara ya Balozi huyo mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.
Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu , Mjini Bariadi  wakati wa ziara yake mkoani humo, Oktoba 03, 2018.
 Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery  akizungumza na Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu wakati wa ziara ya Balozi huyo mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.
Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu ( wa pili kulia)  akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa mkoa wa Simiyu mara baada ya kuhitimisha ziara yake mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.
 Kutoka kulia Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery  kilichopo Bariadi, Bw. Boaz Ogola wakiteta jambo, wakati wa ziara ya Balozi huyo mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.


Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchambua Pamba cha Alliance Ginnery  akizungumza na Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu wakati wa ziara ya Balozi huyo mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.


Baadhi ya viongozi na waandishi wa habari mkoani Simiyu wakisikiliza Balozi wa Kenya  nchini Tanzania,  Mhe. Dan Kazungu Mjini Bariadi, wakati wa ziara ya Balozi huyo mkoani Simiyu, Oktoba 03, 2018.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!