Thursday, October 11, 2018

WAFUGAJI SIMIYU KUBORESHA UFUGAJI KUPITIA UHIMILISHAJI


Wafugaji Mkoani Simiyu wanatarajia kuboresha ufugaji wao kupitia Mpango Mkakati wa kuboresha ng’ombe wa asili kwa njia ya  uhimilishaji kwa lengo la kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya mifugo, mpango unaotarajiwa kuanza kutekelezwa mwezi Desemba, 2018.

Hayo yamebainishwa katika kikao cha Wadau wa Mifugo mkoani Simiyu, kilichofanyika Oktoba 10, 2018 mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  mifugo  kwa njia ya Uhimilishaji (Artificial Insermination),chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

Akizungumza katika kikao hicho Mratibu wa Mpango wa Uhimilishaji  kutoka Shirika la Land O’ Lakes, Bw. Joachim Balakana amesema  shirika hilo kwa kushirikiana na mkoa wa Simiyu limelenga kuhakikisha wafugaji wa ng’ombe wa kienyeji na kisasa wanafanya uhimilishaji ili kuboresha mbari za ng’ombe wao na kuongeza tija katika uzalishaji wa maziwa na nyama.

“Uhimilishaji utafanyika kwa kutumia mbegu bora zilizozalishwa hapa nchini katika kituo cha Uhimilishaji Arusha, baada ya ng’ombe wa kienyeji kuhimilishwa tunategemea kupata ng’ombe chotara wa waziwa ambao watakuwa wakitoa maziwa mengi na wa nyama watakaofikia uzito mkubwa ndani ya muda mfupi”alisema Balakana.

Ameongeza kuwa kupitia mpango huu ng’ombe zaidi ya 12,000 wanatarajiwa kuhimilishwa mkoani Simiyu kuanzia Desemba, 2018, huku akibanisha kuwa kutokana na mwitikio mkubwa wa wafugaji na viongozi mkoani humo, ng’ombe zaidi ya hao waliolengwa wanaweza kuhimilishwa na ndani ya muda mfupi matokeo makubwa yakaonekana.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi,Mhe. Festo Kiswaga akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkoa huo una ng’ombe wengi hivyo, uhimilishaji utasaidia kuongeza thamani ya mifugo kwa upatikanaji wa mbegu bora, ambapo ng’ombe wa nyama watakuwa na uzito mkubwa wakiwa na umri mdogo, ngombe wa maziwa kutoa maziwa mengi na ngozi bora pia itapatikana.

Ameongeza kuwa mkoa huo umejipanga kuboresha ufugaji na kuwasaidia wafugaji kuona thamani ya ufugaji, huku akibainisha kuwa upo uhakika wa kuyaongezea thamani mazao ya mifugo hususani maziwa, kutokana na uwepo wa kiwanda cha maziwa wilayani Meatu ambacho kiko katika mpango wa  kupanuliwa ili kukiongezea uwezo katika uzalishaji.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya uboreshaji  mifugo ya mkoa wa Simiyu, Katibu Tawala Msaidizi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Gamitwe Mahaza amesema jumla ya ng’ombe 348 waliozaliwa kwa njia ya uhimilishaji kati ya ng’ombe 1,598,935 waliopo, hivyo mkoa unaendelea kufanya jitihada mbalimbali kuhimiza uhimilishaji katika halmashauri zote mkoani humo.

Dkt. Gamitwe ametaja moja ya juhudi hizo kuwa ni pamoja na kuzielekeza Halmashauri kutenga asilimia 15 ya mapato ya ndani yatokanayo na mifugo kwa lengo la kuanzisha mfuko wa maendeleo wa mifugo, kuzihamasisha halmashauri kununua vifaa vya uhimilishaji na kununua madume bora.

Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa wafugaji na wafugaji wamesema wameupongeza uongozi wa mkoa kwa kufikiri namna ya kuboresha ufugaji kupitia na mpango wa uhimilishaji na wakaeleza kuwa wameupokea mpango huo na kuomba uanze kutekelezwa mara moja ili waweze kuona tija katika ufugaji wao.

“Naishukuru Serikali kuleta mpango huu wa kuhimilisha ng’ombe wetu nimeupokea kwa furaha sana na ninaomba wataalam waje haraka kutuelimisha wafugaji, ili uanze kutekelezwa haraka tupate kuona  faida ya ufugaji, tupate maziwa mengi na ng’ombe wa nyama wenye uzito mkuwa kama mtaalam alivyotueleza” alisema Bw. Mathias Gabriel  Mfugaji kutoka Kijiji cha Mwanegele wilayani Maswa.

“ Nimeupenda mpango wa uhimilishaji ambao utasaidia kuboresha ng’ombe wa kienyeji tulionao sasa, na mimi kama Katibu wa Wafugaji Itilima napendekeza mpango huu utakapoanza uanzie kwangu, ili wafugaji wengine waje wajifunze kutoka kwangu”  Katibu wa Wafugaji Wilaya ya Itilima, Samson Kingi Guma alieleza.

Mpango mkakati wa uboreshaji wa mifugo kwa njia ya Uhimilishaji Mkoani Simiyu unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Mifugo,  Shirika la Land O’ Lakes chini ya Mradi wa Ushirikishwaji wa Sekta ya Umma na binafsi katika utoaji wa huduma za Uhimilishaji (PAID), kwa ufadhili wa Mfuko wa wakfu wa Bill na Melinda Gates.
MWISHO
Mkuu wa Wilayaya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akifungua kikao cha wadau wa mifugo mkoani Simiyu, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka  kilichofanyika Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha ng’ombe wa asili   kwa njia ya uhimilishaji.
Mratibu wa Mpango wa Uhimilishaji  kutoka Shirika la Land O’ Lakes, Bw. Joachim Balakana akizungumza na wadau wa mifugo Mkoani Simiyu katika kikao cha wadau wa mifugo kilichofanyika Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji.

 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga(kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe Enock Yakobo katika kikao cha wadau wa mifugo kilichofanyika Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji. 
Katibu wa Wafugaji Wilaya ya Itilima, Samson Kingi Guma akichangia hoja katika kikao  cha wadau wa mifugo kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji.
 Baadhi ya wadau wa mifugo wakifuatilia uwasilishaji wa mada mbalimbali katika kikao kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji. 


Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa, Mhe. Paul Jidayi akichangia hoja katika kikao  cha wadau wa mifugo kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji.
Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Gamitwe Mahaza taarifa ya hali ya uboreshaji wa mifugo  mkoani humo, katika kikao  cha wadau wa mifugo kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji.
 Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi akichangia hoja katika kikao  cha wadau wa mifugo kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji. 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akichangia hoja katika kikao  cha wadau wa mifugo kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji.
 Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani akichangia hoja katika kikao  cha wadau wa mifugo kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha  ng’ombe wa asili  kwa njia ya uhimilishaji.
Mfugaji kutoka Kijiji cha Mwanegele wilayani Maswa, Bw. Mathias Gabriel  akichangia hoja katika kikao  cha wadau wa mifugo kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha ng’ombe wa asili   kwa njia ya uhimilishaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza  akichangia hoja katika kikao  cha wadau wa mifugo, kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha ng’ombe wa asili kwa njia ya uhimilishaji.
Baadhi ya  wadau wa mifugo mkoani Simiyu, uwasilishaji wa mada mbalimbali katika kikao kilichofanyika  Mjini Bariadi Oktoba 10, 2018 kwa lengo la kujadili Utekelezaji wa Mpango mkakati wa kuboresha ng’ombe wa asili  kwa njia ya uhimilishaji. 


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!