Sunday, October 21, 2018

RC MTAKA ATOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI MAONESHO YA SIDO KITAIFA SIMIYU


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wananchi mkoani humo na maeneo mengine nchini kujitokeza kwa wingi kushirikia katika  Maonesho ya Kitaifa ya Viwanda Vidogo (SIDO), yatakayofanyika kuanzia Oktoba 23-28, mwaka huu katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani humo na kubainisha kuwa Maandalizi yote yamekamilika.

.Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Mtaka amesema Maonesho haya yatafunguliwa rasmi siku ya Jumanne Oktoba 23, 2018 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.

Ameongeza kuwa katika maonesho hayo wajasiriamali, waoneshaji wa teknolojia mbalimbali wamealikwa na kusisitiza kuwa hii ni fursa kwa wananchi wa Mkoa wa Simiyu na mikoa mingine kuona ushindani katika uongezaji wa thamani wa mazao mbalimbali na fursa kwa wajasiriamali kujifunza kutoka kwa wenzao.

“ Nitoe wito kwa wananchi wa mkoa wa Simiyu kujitokeza kushiriki maonesho haya maana hii ni fursa kwao ya kuweza kujielimisha katika maeneo mbalimbali ya teknolojia za viwanda hususani viwanda vidogo, lakini pia wajasiriamali watapata nafasi ya kujifunza kutoka kwa wenzao wa maeneo mengine nchini na nje ya nchi” alisema Mtaka.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uwekezaji wa  Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Shoma Kibende amesema tayari wajasiriamali kutoka mikoa mbalimbali wamethibitisha kushiriki  maonesho hayo na baadhi yao wameanza kuwasili.

“Wajasiriamali zaidi ya 1000 kutoka mikoa yote nchini wanatarajia kushiriki maonesho haya na baadhi yao wameshaanza kuwasili, lakini pia kuna taasisi mbalimbali ambazo ni taasisi shirikishi na SIDO, huduma za kupata ubora hii ni fursa pekee kwa Watanzania” alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe amesema zaidi ya wajasiriamali 51 kutoka wilayani humo watashiriki katika kuonesha bidhaa mbalimbali ambazo wametengeneza na kuzalisha kupitia viwanda vidogo.

Naye Meneja wa SIDO Mkoa wa Kagera,Richard Mahela amesema maonesho ya SIDO ambayo ni ya kwanza kufanyika Kitaifa  yatawasaidia wajasiriamali kote nchini kupanua masoko ya bidhaa zao kwa kuwa wameandaa vipeperushi vya bidhaa zao ambavyo  vitasambazwa kwa lengo la kusaidia kuwaunganisha na wanunuzi.

Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) Kitaifa ambayo ni ya kwanza kufanyika ngazi ya Kitaifa yatafunguliwa rasmi Jumanne Oktoba 23, 2018 na kuhitimishwa siku ya Jumapili Oktoba 28, 2018 yakiwa na Kauli Mbiu: PAMOJA TUJENGE VIWANDA KUFIKIA UCHUMI WA KATI”.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe, Anthony Mtaka akizungumza na Waandishi wa Habari(hawapo pichani) , juu ya ufunguzi wa Maonesho ya Viwanda Vidogo Kitaifa, yatakayofanyika Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uwekezaji wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Shoma Kibende akizungumza katika Mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka na Waandishi wa habari(hawapo pichani) juu ya ufunguzi wa Maonesho ya Viwanda Vidogo Kitaifa, yatakayofanyika Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Baadhi ya Waandishi wa Habari na Maafisa na Mameneja wa SIDO wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe, Anthony Mtaka katika mkutano wake na Waandishi wa Habari, juu ya ufunguzi wa Maonesho ya Viwanda Vidogo Kitaifa, yatakayofanyika Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Baadhi ya Mameneja wa SIDO wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe, Anthony Mtaka katika mkutano wake na Waandishi wa Habari, juu ya ufunguzi wa Maonesho ya Viwanda Vidogo Kitaifa, yatakayofanyika Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Seif Shekalaghe  akizungumza katika Mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka na Waandishi wa habari(hawapo pichani) juu ya ufunguzi wa Maonesho ya Viwanda Vidogo Kitaifa, yatakayofanyika Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Meneja wa SIDO Mkoa wa Kagera  Richard Mahela  akizungumza katika Mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka na Waandishi wa habari(hawapo pichani) juu ya ufunguzi wa Maonesho ya Viwanda Vidogo Kitaifa, yatakayofanyika Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Baadhi ya mabanda ya maonesho yakiendelea kuandaliwa kwa ajili ya Maonesho ya Viwanda Vidogo Kitaifa, yatakayofanyika Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!