Saturday, October 6, 2018

WAZIRI MKUU MAJALIWA MGENI RASMI MAONESHO YA SIDO KITAIFA SIMIYU


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Maonesho ya Kwanza ya Viwanda vidogo (SIDO)  ambayo Kitaifa yatafanyika mkoani SIMYU katika Viwanja vya nane nane Nyakabindi, kuanzia tarehe 23-28 Oktoba, 2018.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka  katika kikao cha maandalizi ya maonesho  hayo kilichowashirikisha baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na mameneja wa Shirika la Viwanda vidogo (SIDO) kutoka mikoa ya Simiyu, Dodoma ,Mwanza, Kagera ,Mara, Shinyanga na Arusha.

Mtaka amewakaribisha wananchi wa mkoa mwenyeji Simiyu Watanzania wote kwa ujumla kuja kushiriki maonesho ya SIDO yatakayobebwa  na Kauli Mbiu “Pamoja Tujenge Viwanda Kufikia Uchumi wa Kati” na kubainisha kuwa mkoa wa Simiyu unaamini kuwa maonesho hayo yatakuwa ni maonesho darasa, mahali ambapo watu watajifunza na kufanya biashara.

Ameongeza kuwa maonesho ya SIDO yanabeba ajenda ya Serikali ya awamu ya tano na matamanio ya Mhe. Rais ya kuwa na Tanzania ya Viwanda na kuifikisha  nchi katika Uchumi wa Kati, hivyo akaawaalika wadau wote wenye teknolojia mbalimbali kushiriki maonesho haya.

“Ninawaalika wadau wote wenye teknolojia mbalimbali waweze kushiriki maonesho haya , nayaalika makampuni, taasisi na mashirika yenye vitu vinavyoweza kuwafaa wajasiriamali na Watanzania ambao wangehitaji kuwekeza kwenye viwanda, waweze kuleta teknolojia zao”

“Ninawaaalika Wajasiriamali wote kushiriki maonesho haya maana yatatoa nafasi kila mjasiriamali kujifunza kwa mwenzake, kupata elimu na kubadilisha ujuzi ili waweze kuzalisha bidhaa bora zaidi” alisema Mtaka.

Aidha, ametumia mkutano huo kuzialika taasisi za fedha ili ziweze kujitangaza kwa wajasiriamali nao wakaona ni namna gani wanaweza kupata mitaji, huku akisisitiza na kuzialika taasisi za kitaaluma na vitivo vya uhandisivya Vyuo vikuu  pamoja na mashirika mbalimbali ya Kimatifa yanayofanya kazi hapa nchini.

Akizungumzia ada ya ushiriki Mtaka amesema wajasiriamali wenye mahitaji maalum watashiriki bure, wajasiriamali wadogo watashiriki bila kulipia gharama yoyote isipokuwa watalipa shilingi elfu kumi (10,000/=)  kwa ajili ya sare, wajasiriamali wa kati watachangia shilingi laki mbili (200,000/=) taasisi, makampuni na mashirika ambayo hayapo katika makundi la wajasiriamali wadogo , wa kati na wadhamni watatakiwa kuchangia shilingi milioni mbili (2000,000/=) kama ada ya ushiriki.

Kwa upande wa udhamini Mtaka amesema kuwa kwa taasisi, mashirika au kampuni zilizo tayari kudhamini maonesho hayo,  kiwango cha juu kitakuwa shilingi milioni thelethini (30,000,000/=), kiwango cha kati shilingi milioni kumi  (10,000,000/= ) na kiwango cha chini kitakuwa milioni tano (5,000,000/=)  huku akisisitiza kuwa  wadhamini hawa watambuliwa kwa vyeti na watapewa kipaumbele cha mgeni rasmi kutembelea mabanda yao.

Jumla ya  wajasiriamali wadogo, wa kati na wakubwa 1000 wanatarajia kushiriki Maonesho haya ya Viwanda Vidogo SIDO Kitaifa pamoja na taasisi, mashirika na makampuni ya Umma na binafsi yatashiriki pia.
MWISHO

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa




Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na waandishi wa habari na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi  ya Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) Kitaifa,yatakayofanyika mkoani SIMYU katika Viwanja vya nane nane Nyakabindi, kuanzia tarehe 23-28 Oktoba, 2018. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na waandishi wa habari na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi  ya Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) Kitaifa,yatakayofanyika mkoani SIMYU katika Viwanja vya nane nane Nyakabindi, kuanzia tarehe 23-28 Oktoba, 2018 .
Baadhi ya  waandishi wa habari na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi  ya Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) Kitaifa,yatakayofanyika mkoani SIMYU katika Viwanja vya nane nane Nyakabindi, kuanzia tarehe 23-28 Oktoba, 2018 , wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ,katika mkutano uliofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi  ya Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) Kitaifa,yatakayofanyika mkoani SIMYU katika Viwanja vya nane nane Nyakabindi, kuanzia tarehe 23-28 Oktoba, 2018 , wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ,katika mkutano uliofanyika           Mjini Bariadi.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!