Saturday, October 27, 2018

NAIBU WAZIRI MABULA ATOA WITO WANANCHI SIMIYU KUCHANGAMKIA FURSA YA NYUMBA ZA SHIRIKA LA NYUMBA

Naibu waziri wa ardhi ,nyumba na maendeleo ya makazi Mhe.Angelina Mabula ametoa wito kwa wakazi wa mkoa wa SIMIYU kutumia fursa za nyumba za makazi zinazotarajiwa kujengwa katika eneo la Isanga Mjini Bariadi na Shirika la Nyumba la Taifa


Wito huo ameutoa mkoani Simiyu alipokutana na wadau mbalimbali katika kongamano la ujenzi wa nyumba za makazi mkoani Simiyu lililohudhuriwa na viongozi wa serikali mkoani humo wakiongozwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa mkoa wa Simiyu,wakuu wa wilaya wakurugenzi, makatibu tawala wilaya, wakuu wa idara na watumishi wa kada mbalimbali kutoka halmashauri zote, wafanyabiashara na viongozi wa vyama vya wafanyakazi lengo likiwa ni kuangalia aina ya nyumba zitakazojengwa na Wateja watarajiwa.

Mabula amesema azma ya wizara ya ardhi ,nyumba na maendeleo ya makazi ni kumwezesha kila mtanzania kunufaika na nyumba zinazojengwa na shirika hilo, huku akisisitiza Taasisi nyingine zinazohusika na uwekaji wa miundombinu muhimu kuanza utaratibu wa kuweka miundombinu hiyo ili kuwapunguzia gharama wanunuzi.

“ Tunatarajia taasisi zinazohusika ziwe zimeshaanza kupeleka huduma huko, wakati NHC wanaanza kujenga nyumba zao pale gharama itakuwa iko chini kwa sababu hivi vitu vingine vitakuwa vimewekwa na taasisi nyingine na kazi yao itakuwa ni kurudiisha fedha zao kupitia bili za umeme, maji”

“Awali nyumba za NHC zilikuwa zikilalamikiwa kuwa ni za gharama kubwa kutokana na wao kufanya kazi zote wao wenyewe, ujenzi wa nyumba na uwekaji wa miundombinu ya maji , umeme, barabara, viwanja vya michezo na huduma nyingine, lakini tunamshukuru Mhe. Rais alishatoa maelekezo kwa wizara na mamlaka husika kuhakikisha wanaweka miundombinu ya huduma zote muhimu mahali ambapo NHC wanajenga nyumba zao” alisema.

Wakitoa maoni yao baadhi ya wadau wametoa ushauri kwa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuona namna ya kujenga nyumba zenye gharama nafuu zaidi ili wananchi wengi hususani wale wenye kipato cha chini waweze kunufaika na mradi huu.

“Ninaiomba Serikali kuangalia upya gharama za nyumba za makazi zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) ili kuwawezesha watumishi na wananchi wengi kumudu gharama za kununua nyumba hizo kwa kuwa wengi ni wenye vipato vya chini, pia benki zinazowakopesha wananchi wanaonunua nyumba hizo zitoe mikopo kwa masharti ambayo hayatawaumiza wakopaji” alisema Mbunge wa Itilima, Mhe. Njalu Silanga.

“Ninashauri Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuona haja ya kuwa na mpango mkakati wa kuboresha makazi ya wakulima ambao wamejiunga na Vyama vya Ushirika vya Msingi(AMCOS) ili vyama hivyo, benki pamoja na NHC waje namna   kujenga nyumba zenye bei nafuu zaidi na kundi kubwa zaidi liweze kunufaika” alisema Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa kwa kuwa chachu ya Maendeleo ya makazi bora nchini, huku akibainisha kuwa Shirika hilo linaweza kuona namna ya kufanya kazi na Halmashauri mkoani humo katika kukabiliana na changamoto ya makazi kwa watumishi.

Wakizungumza katika Kongamano hilo Wawakilishi wa taasisi za fedha zikiwemo Benki za NMB, CRDB na Azania Bank  wamesema wamejipanga katika utoaji wa mikopo ya nyumba kwa wale walio tayari na wenye vigezo vinavyotakiwa.
MWISHO

Naibu waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula akizungumza na wadau mbalimbali katika Kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wadau mbalimbali katika Kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi.



Naibu waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula(kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka katika Kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Kutoka kushoto Kaimu Mkurugenzi Mauzo na Masoko wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)  Itandula Gambalagi, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka na Naibu waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula wakiteta jambo katika Kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Sagamiko akichangia hoja katika Kongamano lililohusu  ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika  Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Mshauri wa Jeshi la Akiba Mkoani Simiyu, akichangia hoja katika kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani akichangia hoja katika semina kuhusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, ambayo imefanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Baadhi ya viongozi na wadau mbalimmbali mkoani Simiyu wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi mkoani Simiyu, lililofanyika Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga  akichangia hoja katika Kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Mmoja wa Wafanyakazi wa Benki ya NMB akichangia hoja katika kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Meneja  wa  Benki ya NMB Bariadi  akichangia hoja katika kongamano lilohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau  mbalimbali.
Mmoja wa Watumishi wa Benki ya CRDB akiwasilisha mada katika Kongamano lililohusu  ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Naibu waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Mkoa wa Simiyu baada ya kufungua kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika hilo katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera  akichangia hoja katika kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Naibu waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Wakuu wa Idara Mkoa wa Simiyu baada ya kufungua kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika hilo katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.
Naibu waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Mhe. Angelina Mabula(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Wakurugenzi, Makatibu Tawala wa Wilaya na Makatibu Tawala Wasaidizi Mkoa wa Simiyu, baada ya kufungua Kongamano lililohusu ujenzi wa nyumba Makazi zinazotarajiwa kujengwa na Shirika hilo katika Mji wa Bariadi, lililofanyika Oktoba 26, 2018 Mjini Bariadi na kushirikisha wadau mbalimbali.








0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!