Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewataka
viongozi wa Serikali mkoani Simiyu kuisaidia na kuilea Sekta Binafsi ili iendelee
kukua na wahakikishe kuwa maamuzi wanayofanya hayawi vikwazo katika mazingira ya biashara na uwekezaji.
Mtaka
ameyasema hayo wakati akifungua Warsha ya Utetezi na majadiliano katika
kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji
kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu ambayo
imefanyika mjini Bariadi.
Amesema
viongozi wa Serikali mkoani humo wanapofanya maamuzi katika biashara za watu ni
lazima wawe na nia ya dhati ya kuona sekta binafsi inakuwa, ili maamuzi ya
viongozi hao yasiwe vikwazo kwa ukuaji wa Sekta binafsi na mazingira ya
biashara na uwekezaji.
“Sekta
binafsi ni lazima ilelewe anaeilea ni Serikali, Sekta binafsi ni lazima ilindwe
anayeilinda ni Serikali,Sekta binafsi ni lazima isimamiwe anayeisimamia ni
Serikali na Serikali inaisimamia kwa maana ya kuilea ili ifanye vizuri” alisema
Mtaka.
Aidha,
ametoa wito kwa Wakuu wa Wilaya mkoani Simiyu kuendeleza utaratibu wa kukutana
na wafanyabishara ili kupata nafasi ya kujadiliana juu ya fursa mbalimbali za
uwekezaji na namna ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, huku
akisisitiza pia kuendelea kufanyika kwa mabaraza ya biashara ya wilaya.
Katibu
wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo nchini(TCCIA) Mkoa wa Simiyu,
Bi. Christina Matulanya amesema ili kuboresha mazingira ya biashara Serikali
inapaswa kuendelea kuvutia wawekezaji na
kusimamia sheria, sera na kanuni zisipindishwe, huku akiupongeza Mkoa wa Simiyu
kwa kuandaa mwongozo wa uwekezaji.
Katika
hatua nyingine Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Simiyu, Bw.
Charles Mkumbwa ametoa wito kwa wafanyabiashara
kuwa wazalendo, kutoa risiti ipasavyo, kufuata sheria za kodi na akaahidi
kuwapa ushirikiano wafanyabiashara kila wanapohitaji.
Mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule ya biashara, Khalidi Swabiri ambaye alikuwa mwezeshaji wa
warsha hii amesema ni vema mabaraza ya biashara ya wilaya yakafanyika ili
wafanyabiashara wapate muda wa kukutana na viongozi wa Serikali, sekta binafsi
kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika mazingira
ya biashara na uwekezaji na ufumbuzi wake.
Naye
Mkurugenzi wa Bodi ya Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo
nchini(TCCIA), Dkt. Meshack Kulwa
amesema pamoja na kuomba mabaraza ya biashara ya wilaya yafanye kazi,
ameomba TCCIA mkoani Simiyu itafute
viongozi watakaofanya kazi kwa kujituma ili TCCIA Simiyu iweze kuwa imara.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,
Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na viongozi na watendaji wa Serikali na Sekta
binafsi katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya
biashara na uwekezaji kwa viongozi wa
Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu ambayo imefanyika mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa Bodi ya
Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo nchini(TCCIA), Dkt. Meshack Kulwa
akifafanua jambo katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha
mazingira ya biashara na uwekezaji kwa
viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
watendaji wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia Warsha ya Utetezi na
majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi
mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
watendaji wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia Warsha ya Utetezi na
majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi
mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam Shule ya biashara, Khalidi Swabiri (mwezeshaji) akitoa
mada katika Warsha ya Utetezi na
majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi
mkoani Simiyu, iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mjini Bariadi.
Meneja wa Mamlaka ya
Mapato(TRA) Mkoa wa Simiyu, Bw. Charles Mkumbwa akifafanua jambo katika Warsha ya Utetezi na
majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi
mkoani Simiyu iliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam Shule ya biashara,
Khalidi Swabiri (mwezeshaji)
akitoa mada katika Warsha ya Utetezi na majadiliano
katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi
mkoani Simiyu, iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali na sekta binafsi Mkoani Simiyu wakifuatilia Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
watendaji wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia Warsha ya Utetezi na
majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi
mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
watendaji wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia Warsha ya Utetezi na
majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi
mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi.
0 comments:
Post a Comment