Mkuu wa Mkoa wa Simiu, Mhe. Anthony Mtaka amepewa
tuzo ya elimu ya Tanzania Elimu Awards
na Taasisi ya Elimu Solutions, ikiwa
ni kutambua mchango wake kama kiongozi aliyefanya vizuri na mwenye mchango
mkubwa katika mapinduzi ya elimu Mkoani Simiyu.
Tuzo hiyo imekabidhiwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu
Solutions, Neithan Swed, Septemba 05, 2019 Mjini Bariadi wakati wa uzinduzi wa
Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliopata ufaulu hafifu(daraja
sifuri) katika mtihani wa Mock kwa lengo la kuwasaidia kuongeza ufaulu wao
katika Mtihani wa Taifa utakaofanyika mwezi Novemba 2019.
Swed amesema Taasisi hiyo imefuatilia na kuona juhudi
zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu katika mapinduzi ya elimu ikiwemo
ubunifu wa kuanzisha kambi za kitaaluma ambazo zimeonekana kuwa na mchango
mkubwa katika kuongeza ufaulu wa mkoa wa Simiyu kwa kipindi cha miaka mitatu
mfululizo kutoka mwaka 2016 hadi mwaka 2018.
“Anayoyafanya Mhe. Mtaka hayaishii Simiyu peke yake Tanzania
inayaona, tulifuatilia habari za kambi za kitaaluma na tukaangalia nafasi ya mkoa
katika matokeo na namna mlivyofanya vizuri, mmeweka alama kwenye Taifa na
tunatamani Mhe. Mtaka aziendeleze juhudi hizi zaidi ili mtoke kwenye kumi bora
mwende tatu bora na mwakani tupate mwanafunzi bora kutoka Simiyu atakayepata
tuzo hii” alisema Neithan Swed.
Katika hatua nyingine Swed amesema Taasisi ya Elimu
Solutions itatoa ufadhili kwa mwanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2019
atakayefanya vizuri katika mtihani wa Taifa na kumpeleka nchini China kuendelea
na masomo.
Akipokea tuzo hiyo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.
Anthony Mtaka ameishukuru Taasisi ya Elimu Solutions kwa kutambua juhudi
zinazofanywa na mkoa wa Simiyu na kutoa tuzo huku akibainisha kuwa mkoa wa
Simiyu unaithamini sana tuzo hiyo.
Aidha, Mtaka ameipongeza Taasisi ya Elimu Solutions namna
wanavyohamasisha maendeleo ya Elimu ya Watanzania ikiwa ni pamoja na kutoa
ufadhili kwa wanafunzi wanaofanya vizuri kwenda kusoma nje ya nchi.
Tuzo za Elimu Tanzania Elimu Awards zimetolewa na Taasisi
ya Elimu Solutions kwa wadau mbalimbali wa elimu waliochangia na kusaidia kuleta mabadiliko kwa ubunifu na juhudi
zao binafsi, taasisi zinazoihudumia sekta ya elimu; pia hutolewa kwa viongozi,
walimu, wanafunzi waliofanya vizuri kwenye elimu
MWISHO
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Solutions, Neithan Swed akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka tuzo ya elimu iliyotolewa na Taasisi hiyo kwake ikiwa ni kutambua mchango wake kama kiongozi aliyefanya vizuri na mwenye mchango mkubwa katika mapinduzi ya elimu Mkoani Simiyu
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akionesha tuzo ya elimu aliyopewa na Taasisi ya Elimu Solutions kwake ikiwa ni kutambua mchango wake kama kiongozi aliyefanya vizuri na mwenye mchango mkubwa katika mapinduzi ya elimu Mkoani Simiyu
Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Simiyu, Komredi Enock Yakobo akionesha tuzo ya elimu iliyotolewa
na Taasisi ya Elimu Solutions kwa Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ikiwa
ni kutambua mchango wake kama kiongozi aliyefanya vizuri na mwenye mchango
mkubwa katika mapinduzi ya elimu Mkoani Simiyu.
Afisa
Elimu Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akisoma maneno yaliyoandikwa kwenye tuzo
ya elimu iliyotolewa na Taasisi ya Elimu
Solutions kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ikiwa ni kutambua mchango wake kama kiongozi aliyefanya
vizuri na mwenye mchango mkubwa katika mapinduzi ya elimu Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Biashara wa Taasisi ya Elimu Solutions, Nice Alex akimkabidhi zawadi
ya fulana Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kumkabidhi
tuzo ya elimu ikiwa ni kutambua mchango wake kama kiongozi aliyefanya vizuri na
mwenye mchango mkubwa katika mapinduzi ya elimu Mkoani Simiyu.
Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akimkabidhi mmoja wa walimu walio
katika kambi maalum ya wanafunzi wa kidato cha nne alizokabidhiwa na Taasisi ya
Elimu Solutions.
Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akimkabidhi mmoja wa walimu walio
katika kambi maalum ya wanafunzi wa kidato cha nne alizokabidhiwa na Taasisi ya
Elimu Solutions.
0 comments:
Post a Comment