Wednesday, September 4, 2019

TAASISI YA AMANI GIRLS HOME YATOA VITENDEA KAZI KWA WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII SIMIYU


Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home limetoa msaada wa vitendea kazi kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii kwa  lengo la kuwasaidia kutekeleza majukumu yao ya kutoa elimu kwa jamii juu mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria kupitia mradi wa “BADILISHA TABIA TOKOMEZA MALARIA,” Mkoani Simiyu.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya vitendea kazi hivyo Meneja Miradi wa Amani Girls Home, Bw. Revocatus Sono, amevitaja vifaa hivyo kuwa ni baiskeli 46, makoti  ya mvua 46,  mabuti ya mvua 46, fulana na vitini vya kutolea elimu kwa jamii vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni tisa, ambavyo vimetolewa kwa wahudumu  wa afya ngazi ya jamii wapatao 46  kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Busega na Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Nao wahudumu wa afya ngazi ya jamii  wameishukuru Taasisi  ya Amani Girls Home kwa kutoa msaada wa vitendea kazi ambavyo wamesema vitawarahisihsia kazi na kuwawezesha kuwafikia wananchi wengi na kutoa elimu iliyokusudiwa kwa jamii ili kufikia lengo la kutokomeza kabisa ugonjwa wa Malaria mkoani Simiyu.

“Tunaishukuru Amani Girls Home kwa kutoa vitendea kazi hivi, awali tulianza kazi tukiwa hatuna vifaa ilikuwa ni changamoto kubwa kwa kuwa tuna mitaa mikubwa na hatukuweza kuwafikia walengwa wote, leo tumekabidhiwa vifaa zikiwemo baiskeli naamini vitatusaidia kufanya kazi yetu kwa wepesi katika kuifikia jamii” alisema Abadi James Mhudumu wa afya ngazi ya Jamii Kata ya Malambo Bariadi Mjini.

Mratibu wa Mpango wa Kudhibiti Malaria Mkoa wa Simiyu, Dkt. Mugune Maeka amewataka wahudumu wa afya ngazi ya jamii kuhakikisha wagonjwa wa malaria watakaowaibua katika jamii wanafikishwa katika vituo vya kutolea huduma, ili wapate matibabu sahihi na kwa wakati lengo likiwa ni kupunguza maambukizi ya malaria kutoka asilimia sita ya sasa na hatimaye  kufuta kabisa ugonjwa wa malaria.

Awali akizungumza na wahudumu hao, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Bw. Melkizedeck Humbe amewataka kutumia vitendea kazi  walivyopewa kwa malengo yaliyokusudiwa, huku akiahidi kuwa Serikali itaweka utaratibu wa kuendeleza juhudi za wadau wa afya katika mapambano dhidi ya malaria ili ugonjwa wa malaria ubaki kuwa historia katika mkoa wa Simiyu.

Katika hatua nyingine Humbe amewataka wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii kutoa elimu kwa jamii kutumia vituo vya kutolea huduma za  Afya kupata matibabu kila wanapoona dalili za ugonjwa badala ya kwenda kwa waganga wa jadi ili waweze kupata tiba sahihi kwa wakati sahihi.

Amesema Serikali imejenga vituo vya kutolea huduma za afya katika maeneo mbalimbali ikiwemo zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa zinaendelea kujengwa, hivyo ni vema jamii ikaelimishwa umuhimu wa kutumia vituo hivyo kupata huduma za tiba ya magonjwa mbalimbali ikiwemo  Malaria  badala ya kwenda kwa waganga wa jadi.

“Hospitali za wilaya zinajengwa, vituo vya afya vimejengwa, zahanati zimejengwa kawaelimisheni watu watumie vituo vya kutolea huduma za afya ajili ya kwenda kupima afya na kupata matibabu sahihi kwa wakati wanapokuwa wagonjwa, badala ya kwenda kwa waganga wa jadi ili tutokomeze kabisa malaria kwenye mkoa wetu” alisema Humbe.
MWISHO

Mkurugenzi wa Halmashauri Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe akiwakabidhi wahudumu wa afya ngazi ya jamii baiskeli kwa niaba ya wenzao ambao wote wamepewa baiskeli na vitendea kazi vingine na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home ambavyo vimekabidhiwa kwao  Septemba 04, Mjini Bariadi.

Mkurugenzi wa Halmashauri Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe akizungumza na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kutoka Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Busega wakati wa hafla ya makabidhiano ya vitendea kazi zikiwemo baiskeli vilivyotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home na kukabidhiwa Septemba 04, Mjini Bariadi.


 Baadhi ya  wahudumu wa afya ngazi ya jamii kutoka Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Busega wakimsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe(hayupo pichani)  wakati wa hafla ya makabidhiano ya vitendea kazi zikiwemo baiskeli vilivyotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home kwa ajili ya kutoa elimu juu ya vita dhidi ya malaria na kukabidhiwa kwa wahudumu hao Septemba 04, Mjini Bariadi.

Mkurugenzi wa Halmashauri Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe akimkabidhi mmoja wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii fulana kwa niaba ya wenzake 45 ambao wote wamepewa baiskeli na vitendea kazi vingine na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home kwa ajili ya kutoa elimu juu ya vita dhidi ya malaria na kukabidhiwa wahudumu hao Septemba 04, Mjini Bariadi.

Mkurugenzi wa Halmashauri Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe akimkabidhi mmoja wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii kitini cha kutolea elimu kwa jamii kwa niaba ya wenzake 45 ambao wote wamepewa baiskeli na vitendea kazi vingine na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home kwa ajili ya kutoa elimu juu ya vita dhidi ya malaria na kukabidhiwa wahudumu hao Septemba 04, Mjini Bariadi.

Mkurugenzi wa Halmashauri Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe akimkabidhi mmoja wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii kitini cha kutolea elimu kwa jamii kwa niaba ya wenzake 45 ambao wote wamepewa baiskeli na vitendea kazi vingine na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home kwa ajili ya kutoa elimu juu ya vita dhidi ya malaria na kukabidhiwa wahudumu hao Septemba 04, Mjini Bariadi.
Mratibu wa Mpango wa Kudhibiti Malaria Mkoa wa Simiyu, Dkt. Mugune Maeka akitoa taarifa ya hali ya malaria mkoani Simiyu, wakati wa makabidhiano ya vitendea kazi vya wahudumu wa afya ngazi ya jamii  zikiwemo baiskeli na makoti ya mvua, yaliyofanyika Septemba 04, Mjini Bariadi.

Baadhi ya baiskeli zilizotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home Wahudumu wa Afya ngazi ya jamii kutoka  Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Busega na Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home,  Septemba 04, Mjini Bariadi
Baadhi ya baiskeli zilizotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home Wahudumu wa Afya ngazi ya jamii kutoka  Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Busega na Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home,  Septemba 04, Mjini Bariadi.



Baadhi ya vitendea kazi vilivyotolewa pamoja na baiskeli na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home kwa Wahudumu wa Afya ngazi ya jamii kutoka  Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Busega na Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home,  Septemba 04, Mjini Bariadi kwa ajili ya kutoa elimu juu ya vita dhidi ya malaria .
Baadhi ya  wahudumu wa afya ngazi ya jamii kutoka Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Busega wakimsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe(hayupo pichani)  wakati wa hafla ya makabidhiano ya vitendea kazi zikiwemo baiskeli vilivyotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Amani Girls Home kwa ajili ya kutoa elimu juu ya vita dhidi ya malaria na kukabidhiwa kwa wahudumu hao Septemba 04, Mjini Bariadi

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!